1Mumusifu Mungu katika pahali pake patakatifu,
mumusifu juu mbinguni kwenye uwezo wake!
2Mumusifu kwa sababu ya matendo yake makubwa,
mumusifu kwa ajili ya utukufu wake mukubwa!
3Mumusifu kwa mulio wa baragumu,
mumusifu kwa zeze na kinubi!
4Mumusifu kwa ngoma na michezo,
mumusifu kwa filimbi na kinanda!
5Mumusifu kwa matoazi ya sauti kubwa,
mumusifu kwa matoazi yenye kuvuma sana!
6Kila kiumbe chenye uzima kimusifu Yawe!
Mumusifu Yawe!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.