Hosea 2 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Waisraeli watarudishiwa tena hali yao ya mbele

1Lakini hesabu ya Waisraeli itakuwa kubwa kama muchanga wa bahari ambao haupimiki wala hauhesabiki. Pale ambapo Mungu aliwaambia: Ninyi si watu wangu, sasa atawaambia: Ninyi ni watoto wa Mungu Mwenye Uzima.

2Watu wa Yuda na Waisraeli wataungana pamoja na kumuchagua mwongozi wao mumoja; nao watastawi katika inchi yao. Hiyo itakuwa siku kubwa ya Yezereheli.

3Basi, muwaite wakaka zenu, “Watu wangu”, na wadada zenu, “Waliohurumiwa”.

Muke muzinzi – taifa potovu la Israeli

4Mumushitaki mama yenu, mumushitaki,

maana sasa yeye si muke wangu

wala mimi si mume wake.

Mumushitaki aondoe vitambulisho vya uasherati juu ya uso wake,

ajiepushe na mapambo ya uzinzi juu ya kifua chake.

5Kama sivyo, nitamuvua nguo abaki uchi,

nitamufanya akuwe sawa vile alivyozaliwa.

Nitamufanya akuwe utupu sawa jangwa,

akauke sawa inchi kavu.

Nitamwua kwa kiu.

6Na watoto wake sitawahurumia,

maana ni watoto wa uzinzi.

7Mama yao amefanya uzinzi,

aliyebeba mimba yao amefanya mambo ya haya.

Alisema: Nitaambatana na wapenzi wangu,

ambao wananipatia chakula na maji,

nguo za sufu na kitani, pamoja na mafuta na divai.

8Basi, nitafunga njia yake kwa miiba,

nitamuzungushia ukuta,

asipate njia ya kutokea inje.

9Atawafuata wapenzi wake,

lakini hatawapata;

atawatafuta,

lakini hatawaona.

Kwa hiyo atasema:

Nitarudi kwa mume wangu wa kwanza;

maana zamani nilikuwa na raha kuliko sasa.

10Hakujua kwamba ni mimi

niliyemupa ngano, divai na mafuta,

niliyemujalia feza na zahabu kwa wingi,

ambazo alimupelekea mungu Bali.

11Kwa hiyo wakati wa mavuno nitaitwaa ngano yangu,

nitaiondoa divai yangu kwa wakati wake.

Nitamunyanganya nguo zangu za sufu na kitani,

ambazo zilitumika kuufunika uchi wake.

12Nitamuvua nguo abaki uchi mbele ya wapenzi wake,

wala hakuna mutu atakayeweza kunizuia.

13Nitakomesha furaha zake zote,

sikukuu zake za mwandamo wa mwezi na za Sabato,

na sikukuu zote zilizoamriwa.

14Nitaiharibu mizabibu yake na tini zake,

anayosema ni malipo kutoka kwa wapenzi wake.

Nitaifanya ikuwe pori,

nao nyama wa pori wataikula.

15Nitamulipiza kwa ajili ya siku alizoabudu sanamu za mungu Bali,

kwa ajili ya muda alioutumia kuzifukizia ubani,

akajipamba kwa pete zake na ushanga,

na kuwaendea wapenzi wake,

akanisahau mimi.

–Ni ujumbe wa Yawe.

Upendo wa Yawe kwa watu wake

16Kwa hiyo, nitamushawishi,

nitamupeleka katika jangwa

na kusema naye kwa upole.

17Huko nitamurudishia mashamba yake ya mizabibu.

Bonde la Akori litakuwa mulango wa tumaini.

Ataniitikia vizuri kama vile alipokuwa kijana,

kama wakati alipotoka katika inchi ya Misri.

18Siku hiyo, wewe utaniita “Mume wangu”, na sio tena “Bali wangu”.

–Ni ujumbe wa Yawe.–

19Maana, nitalifanya jina la Bali lisitajike tena katika kinywa chako.

20Nitafanya agano na nyama wa pori, ndege pamoja na vyote vinavyotambaa, kusudi wasikuumize. Nitaondoa upinde, upanga na silaha za vita katika inchi, na kukufanya uishi kwa usalama.

21Nitakufanya muke wangu milele; ukuwe wangu kwa sheria na haki, kwa wema na huruma.

22Kweli, nitakuoa kwa uaminifu, nawe utanijua mimi Yawe.

23Siku hiyo,

nitajibu kwa mahitaji ya mbingu ya kunyesha mvua,

mbingu nazo zitajibu kwa mahitaji ya udongo.

–Ni ujumbe wa Yawe.–

24Udongo utajibu mahitaji ya ngano, divai na mafuta,

navyo vyote vitajibu kwa mahitaji ya Yezereheli.

25Nitamwotesha Yezereheli katika inchi;

nitamuhurumia yule aliyeitwa “Asiyehurumiwa”,

na wale walioitwa “Si wangu”,

nitawaambia: “Ninyi ni watu wangu”.

Nao watasema: Wewe ni Mungu wetu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help