1Wimbo wa Safari za kidini. Wa Daudi.
Nilifurahi waliponiambia:
“Twende kwenye nyumba ya Yawe.”
2Sasa tuko tumesimama
kwenye milango yako, ee Yerusalema!
3Yerusalema ni muji uliojengwa
kusudi makundi ya watu yakutane humo.
4Humo ndimo makabila yanamofika,
ndiyo, makabila ya Yawe,
kwa kumushukuru Yawe kama Waisraeli walivyoagiza.
5Humo kulikuwa viti vya kifalme kwa kuamua maneno,
ndivyo viti vya ukoo wa Daudi.
6Muuombee Yerusalema amani mukisema:
“Wote wanaokupenda wakae katika amani!
7Ndani ya kuta zinazokuzunguka kuwe amani,
nao usalama ukuwe ndani ya nyumba zako nzuri!”
8Kwa ajili ya jamaa na wandugu zangu,
ee Yerusalema, ninakutakia amani!
9Kwa ajili ya nyumba ya Yawe, Mungu wetu,
ninakuombea upate uheri!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.