1“Kisha, tukageuka, tukapanda kuelekea Basani. Mufalme Ogi akatoka na watu wake wote kwa kupigana nasi karibu na muji wa Edirei.
2Lakini Yawe akaniambia: ‘Usimwogope, maana nimemutia katika mikono yako pamoja na watu wake na inchi yake. Utamutendea kama vile ulivyomutendea Sihoni mufalme wa Waamori aliyekaa kule Hesiboni’.
3“Basi, Yawe akamutia katika mikono yetu mufalme Ogi wa Basani na watu wake, tukawaangamiza hata hakukubakia mutu yeyote.
4Tukateka miji yake yote; hakuna hata muji mumoja ambao hatukuuteka. Kwa jumla tuliteka miji makumi sita, ni kusema eneo lote la Argobu ambalo lilitawaliwa na mufalme Ogi wa Basani.
5Miji yote hii ilikuwa na makimbilio yenye kuta ndefu zilizokuwa na milango na vifungio. Kulikuwa vilevile vijiji vingi ambavyo havikuzungukwa na kuta.
6Tuliteketeza kila kitu huko, tukaharibu kila muji na kuua wanaume, wanawake na watoto kama vile tulivyofanya katika miji ya mufalme Sihoni wa Hesiboni.
7Lakini mifugo yote na mali tukaviteka.
8“Wakati huo tukatwaa inchi hiyo ya wale wafalme wawili wa Waamori waliokuwa wanakaa ngambo ya muto Yordani, katikati ya muto Arnoni na mulima Hermoni.
9(Wasidoni wanaita mulima huo Sirioni, nao Waamori wanauita Seniri.)
10Tukateka miji yote katika sehemu za mabonde, za mwinuko, na vilevile eneo lote la Gileadi na Basani mpaka Saleka na Edirei, miji ya mufalme Ogi huko Basani.”
11(Mufalme Ogi ndiye peke yake aliyebakia kati ya Warefai. Kitanda chake kilichotengenezwa kwa chuma, kilikuwa na urefu wa metre ine na upana wa karibu metre mbili. Kitanda hicho kipo katika muji wa Waamori wa Raba.)
Makabila yaliyokaa mashariki ya Yordani(Hes 32.1-42)12“Tulipoitwaa inchi hiyo, nikawapa makabila ya Rubeni na Gadi eneo la kuanzia upande wa kaskazini wa Aroeri karibu na Arnoni na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake.
13Kisha nikalipatia nusu ya lile kabila la Manase sehemu iliyobaki ya Gileadi pamoja na Basani yote iliyotawaliwa na Ogi, ni kusema eneo lote la Argobu. Inchi yote ya Basani ilijulikana kama vile inchi ya Warefai.
14Yairi, mutu wa kabila la Manase, alitwaa eneo lote la inchi ya Argobu, ni kusema Basani, mpaka kwenye mupaka wa Gesuri na Maka. Vijiji vyote alivipa jina lake, na mpaka leo vinajulikana kama vile ‘Vijiji vya Yairi’.
15Watu wa ukoo wa Makiri wa kabila la Manase nikawapa Gileadi,
16na watu wa makabila ya Rubeni na Gadi nikawapa inchi yote kutoka Gileadi mpaka muto Arnoni. Mupaka wao wa kusini ulikuwa muto ule na wa kaskazini ulikuwa muto Yaboki ambao ndio unaopakana na inchi ya Waamori.
17Upande wa magaribi, inchi yao ilienea mpaka muto Yordani. Toka ziwa Galilaya upande wa kaskazini, ukashuka mpaka kwenye bahari ya Araba, ni kusema bahari ya Chumvi, mpaka kwenye miteremuko ya Pisiga, upande wa mashariki.
18“Wakati ule niliwapa maagizo haya: ‘Yawe, Mungu wenu amewapa inchi hii upande wa mashariki wa muto Yordani ikuwe mali yenu. Sasa ninyi mashujaa kati ya wandugu zenu, mutwae silaha muvuke muto Yordani mukiwa mbele ya wandugu zenu Waisraeli.
19Lakini wake zenu, watoto wenu na nyama wenu – ninajua muko na mifugo mingi – watabaki kwenye miji niliyowapa.
20Muwasaidie wandugu zenu Waisraeli mpaka Yawe atakapowajalia watulie pahali pao kama vile nanyi mulivyotulia, ni kusema nao vilevile warizi inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapatia huko ngambo ya Yordani. Nyuma ya hayo, mutaweza kurudia katika inchi yenu hii ambayo nimewapa ikuwe yenu!’
21“Kisha nikamwamuru Yoshua: ‘Wewe umeona kwa macho yako mambo yote ambayo Yawe, Mungu wako, amewatendea wafalme hawa wawili, Sihoni na Ogi. Basi, yeye atawatendea vile vile wafalme wa inchi zote mutakazopitia.
22Musiwaogope maana Yawe, Mungu wenu, ndiye atakayepigana kwa ajili yenu.’
Musa anakatazwa kuingia Kanana23“Wakati huo nikamusihi Yawe nikisema:
24‘Ee Bwana wetu Yawe, ninajua umenionyesha mimi mutumishi wako mwanzo tu wa ukubwa wako na uwezo wako. Maana, kuna mungu gani huko mbinguni au katika dunia anayeweza kufanya mambo makubwa na ya ajabu kama vile ulivyofanya wewe?
25Ninakuomba nivuke muto Yordani, niione inchi hiyo nzuri upande wa magaribi wa Yordani, hakika, inchi nzuri ya kupendeza ya milima, pamoja na milima ya Lebanoni’.
26“Lakini Yawe akanikasirikia kwa sababu yenu, akakataa kunisikiliza. Pahali pake akaniambia: ‘Inatosha! Usiseme tena jambo hili.
27Panda mpaka kwenye kilele cha mulima Pisiga, uangalie vizuri upande wa magaribi, kaskazini, kusini na mashariki, na kuiona inchi hiyo; lakini wewe hautavuka huu muto Yordani.
28Lakini umupe Yoshua maagizo, umutie moyo na kumwimarisha, maana yeye ndiye atakayewaongoza watu hawa mpaka ngambo, kurizi inchi utakayoiona’.
29“Basi, tukabaki hapa katika bonde mbele ya Beti-Peori.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.