1Ninamupenda Yawe,
kwa maana ananisikia,
maana amesikia kilio cha ombi langu.
2Yeye amenitegea sikio,
hivyo nitamwomba muda wote wa maisha yangu.
3Hatari ya kifo ilinizunguka,
vitisho vya kaburi vilinishika;
nilisongwa na mahangaiko na huzuni.
4Kisha nikamulilia Yawe:
“Ee Yawe, tafazali uniokoe!”
5Yawe ni mwenye huruma na haki;
Mungu wetu ni mwenye rehema.
6Yawe anawalinda wajinga;
nilipokuwa nimegandamizwa aliniokoa.
7Ukuwe na utulivu mukubwa, ee nafsi yangu,
kwa vyote Yawe amenitendea.
8Ameniokoa toka kifo na kufuta machozi yangu;
akanilinda nisianguke.
9Nitatembea mbele ya Yawe,
katika inchi ya watu wenye kuwa wazima.
10Nilikuwa na imani hata niliposema:
“Mimi nimetaabika sana.”
11Hata nilisema kwa hofu yangu:
“Wanadamu wote hawawezi kutumainiwa!”
12Nitamurudishia Yawe nini,
kwa vyote alivyonitendea?
13Nitamutolea sadaka ya divai
kwa kumushukuru maana ameniokoa.
Nitaomba kwa jina la Yawe.
14Nitamutimizia Yawe viapo vyangu,
mbele ya watu wake wote.
15Kifo cha waaminifu wa Yawe
si jambo dogo mbele yake.
16Ee Yawe, mimi ni mutumishi wako,
mutumishi wako, mutoto wa mujakazi wako.
Umenifungulia vifungo vyangu.
17Nitakutolea sadaka za shukrani.
Nitaomba kwa jina la Yawe.
18Nitatimizia ahadi zangu kwa Yawe,
mbele ya watu wake wote,
19katika kiwanja cha hekalu lake,
katikati yako, ee Yerusalema.
Haleluia!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.