1Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa Yedutuni. Zaburi ya Daudi.
2Kwa Mungu peke yake ninapata utulivu,
wokovu wangu unatoka kwake.
3Yeye peke yake ndiye kikingio na wokovu wangu,
yeye ni kimbilio langu, sitatikisika.
4Mpaka wakati gani mutanishambulia mimi?
Mpaka wakati gani ninyi wote mutanipiga,
mimi ninayekuwa kama kiambaza kilichoinama,
kama ukuta unaoanza kubomoka?
5Mumepanga kuniangusha toka nafasi yangu ya heshima;
furaha yenu ni kusema uongo.
Kwa maneno, munabariki,
lakini ndani ya moyo munalaani.
6Kwa Mungu peke yake ninapata utulivu;
tumaini langu linatoka kwake.
7Yeye peke yake ndiye kikingio na wokovu wangu,
yeye ni kimbilio langu, sitatikisika.
8Wokovu na utukufu wangu vinatoka kwa Mungu;
kikingio changu chenye nguvu na kimbilio langu ni Mungu.
9Enyi watu, mutumainie Mungu siku zote;
mumufungulie yanayokuwa ndani ya moyo wenu.
Yeye ndiye kimbilio letu.
10Wanadamu wote ni kama pumzi tu;
wote, wakubwa kwa wadogo, hawafai kitu.
Wakipimwa wote pamoja,
pumzi ni nzito kuliko wao.
11Musitegemee kutesa,
musijisifie mali ya wizi;
kama mali zikiongezeka, musizitegemee.
12Mungu amesema mara na mara,
nami nimesikia tena na tena
kwamba uwezo ni wa Mungu.
13Nao wema ni wa Bwana wetu;
anamulipa kila mutu kadiri ya matendo yake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.