Zaburi 56 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Kumutumainia Mungu

1Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa njiwa anayekaa mbali kwenye ukimya. Mashairi ya Daudi nyuma ya kukamatwa na Wafilistini kule Gati.

2Ee Mungu,

unionee huruma,

maana watu wananishambulia.

Muchana kutwa waadui wananitesa.

3Muchana kutwa waadui zangu wananishambulia;

ni wengi sana hao wanaonipiga vita.

4Ee Mungu Mukubwa, wakati ninapoogopa,

mimi ninakutumainia wewe.

5Ninamutumainia Mungu na kusifu neno lake;

ninamutumainia Mungu, wala siogopi.

Mwanadamu zaifu atanifanya nini?

6Muchana kutwa wanatunga maneno juu yangu;

mawazo yao yote ni ya kunizuru.

7Wanakutana kwa kufanya mipango na kunivizia;

wanachunguza yote ninayofanya;

wanafikiri kwa shabaha ya kunizuru.

8Ee Mungu, uwalipe kwa kadiri ya uovu wao,

uwaangushe hao waovu kwa hasira yako.

9Wewe unajua kutangatanga kwangu;

unaweka machozi yangu ndani ya chupa.

Yote yanakuwa katika kitabu chako.

10Kila mara ninapokuomba musaada wako,

waadui zangu wanarudishwa nyuma.

Ninajua kweli Mungu yuko upande wangu.

11Ninamutumainia Mungu na kusifu neno lake;

ninamutumainia Yawe na kusifu neno lake.

12Ninamutumainia Mungu, wala siogopi.

Mutu atanifanya nini?

13Ee Mungu, nitatimiza ahadi zangu kwako;

nitakutolea sadaka za shukrani,

14maana umeniokoa katika kifo,

umenilinda nisianguke chini,

nipate kuishi mbele yako, ee Mungu,

katika mwangaza wa uzima.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help