1Na hivi mufalme na Hamani wakaenda kula karamu na malkia Esteri.
2Katika siku ya pili, walipokuwa wanakunywa divai, mufalme akamwuliza tena Esteri: “Sasa, malkia Esteri, unataka nini? Uniambie, nawe utapata. Ombi lako ni nini? Hata kama ni nusu ya ufalme wangu, utapewa.”
3Malkia Esteri akamujibu: “Kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ewe mufalme, na ikikupendeza kunitimizia ombi langu, hitaji yangu ni mimi niishi na watu wangu vilevile.
4Maana, mimi na watu wangu tumeuzishwa kusudi tuuawe, tuangamizwe na kuteketezwa kabisa. Kama tungeuzishwa tu kuwa watumwa na wajakazi, ningekaa kimya wala nisingekusumbua. Ingawa tutateswa hakuna adui atakayeweza kulipa hasara hii kwa mufalme.”
5Hapo mufalme Ahasuero akamwuliza malkia Esteri: “Ni nani huyo anayesubutu kufanya jambo kama hilo? Yuko wapi mutu huyo?”
6Esteri akamujibu: “Adui yetu mukubwa na mutesaji wetu, ni huyu mwovu Hamani!” Hapo Hamani akashikwa na hofu mbele ya malkia na mufalme.
7Mufalme akasimama kwa hasira, akatoka ndani ya chumba kwenye karamu ya divai na kwenda inje kwenye bustani ya nyumba ya kifalme. Hamani alipoona kwamba mufalme amekusudia kumwazibu, akabaki nyuma kwa kumusihi malkia Esteri ayaponyeshe maisha yake.
8Kisha mufalme akarudi kutoka katika bustani, na mara alipoingia ndani ya chumba walimokuwa wanakunywa divai, akamukuta Hamani amejitupa karibu na kiti ambamo Esteri alikuwa ameikaa. Kuona hivyo, mufalme akasema kwa sauti kubwa: “Hivi mutu huyu anataka kumushika kwa nguvu malkia mbele yangu, tena ndani ya nyumba ya kifalme?” Mara tu mbele mufalme hajamaliza kusema, matowashi wakamufunika Hamani uso.
9Harbona, mumoja wa wale matowashi waliomutumikia mufalme, akasema: “Hamani amesubutu hata kutengeneza muti wa kumutundikia Mordekayi ambaye aliyaokoa maisha yako, ewe mufalme. Muti huo, wenye urefu wa metre makumi mbili na mbili, bado uko kule katika nyumba yake.” Hapo mufalme akaamuru: “Mumutundike Hamani juu ya muti uleule.”
10Naye, Hamani akauawa pale kwenye muti aliokuwa amemutayarishia Mordekayi. Basi, hasira ya mufalme ikapoa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.