Yeremia 22 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Ujumbe juu ya jamaa ya kifalme ya Yuda

1Yawe anasema hivi: Kwenda kwa jamaa ya kifalme ya Yuda, na utoe ujumbe huu kule:

2Wewe mufalme wa Yuda unayetawala kwa kiti cha kifalme cha Daudi pamoja na wakubwa wa serikali yako na watu wako wanaopita katika milango hii, musikilize neno la Yawe.

3Yawe anasema hivi: Mufuate sheria yangu na kutenda kwa haki. Muokoe kila mutu aliyenyanganywa mali zake toka katika mikono ya mutesaji. Musiwatendee vibaya au kwa ukali wageni, wayatima na wajane, wala musimwange damu ya mutu asiyekuwa na kosa kwa nafasi hii.

4Kama mukishika neno hili nililowaambia, basi wafalme watakaotawala kwa kiti cha kifalme cha Daudi wataendelea kuingia wakipitia milango ya nyumba hii ya kifalme. Watapita pamoja na wakubwa wa serikali yao na watu wao, wakipanda juu ya farasi na magari yenye kukokotwa na farasi.

5Lakini kama hamutatii maneno haya, ninaapa kwa nafsi yangu mwenyewe kwamba nafasi hii itakuwa mabomoko.

–Ni ujumbe wa Yawe.

6Yawe anasema hivi juu ya nyumba ya kifalme ya Yuda:

Ingawa unaonekana vizuri kama inchi ya Gileadi,

kama vichwa vya milima ya Lebanoni,

ninaapa kwamba nitakufanya kuwa jangwa,

ukuwe muji usiokaliwa na watu.

7Nitawatayarisha waangamizaji wakufikie,

kila mumoja akishika silaha yake.

Watazikata nguzo zako nzuri za mierezi,

na kuzitumbukiza katika moto.

8Na watu wengi wa mataifa watapita karibu na muji huu, kila mumoja atamwuliza mwenzake: Kwa nini Yawe ameutendea muji huu mukubwa hivi?

9Nao watajibiana hivi: Ni kwa sababu wakaaji wake walivunja agano la Yawe, Mungu wao, wakaabudu miungu mingine na kuitumikia.

Ujumbe juu ya Salumu

10Musimulilie yule aliyekufa,

musiomboleze kwa ajili yake.

Lakini mumulilie kwa uchungu yule anayekwenda mbali

kwa sababu hatarudi tena kuiona inchi yake.

11Maana, Yawe anasema hivi juu ya Salumu mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda aliyetawala kwa pahali pa baba yake Yosia, na ambaye aliondoka pahali hapa: Salumu hatarudi tena pahali hapa,

12lakini atakufia kulekule alipelekwa katika utumwa. Yeye hataiona tena inchi hii.

Ujumbe juu ya Yoyakimu

13Ole kwako Yoyakimu,

wewe unayejijengea nyumba kwa njia isiyokuwa ya haki,

na kuiwekea magorofi kwa njia isiyofuata sheria ya Mungu.

Unayewatumikisha watu bure

pasipo kuwalipa mishahara yao.

14Wewe unayesema:

Nitajijengea nyumba kubwa,

yenye vyumba vikubwa vya magorofi.

Kisha unaifanyia madirisha,

ukafunika kuta zake kwa mbao za mierezi,

na kuipaka rangi nyekundu!

15Unazani umekuwa mufalme

kwa kujenga na mierezi?

Baba yako alikula na kunywa,

alifuata sheria yangu na kutenda mambo ya haki,

na mambo yake yaliendeka vizuri.

16Aliwapatia haki wamasikini na wakosefu,

na mambo yake yaliendeka vizuri.

Si hivi ndivyo kunijua mimi?

–Ni ujumbe wa Yawe.–

17Lakini macho yako wewe na moyo wako,

vinaelekea tu mapato yasiyokuwa ya haki.

Unamwanga damu ya wasiokuwa na kosa,

nawe unawatesa watu na kuwatendea kwa ukali.

18Kwa hiyo, Yawe anasema hivi juu ya Yoyakimu mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda:

Wakati atakapokufa,

hakuna atakayeomboleza juu yake, akisema:

Yowe, ndugu yangu!

Yowe, dada yangu!

Wala hakuna atakayemulilia, akisema:

Yowe, bwana wetu!

Yowe, muheshimiwa wetu!

19Yeye atazikwa sawa nyama:

atakokotwa na kutupiliwa mbali,

inje ya milango ya Yerusalema.

Hasira itakayoupata Yerusalema

20Enyi watu wa Yerusalema,

mupande kwa milima ya Lebanoni mupige kelele,

munyanyue sauti zenu huko kwenye uwanja wa Basani;

mulalamike kutoka milima ya Abarimu,

maana wapenzi wenu wote wameangamizwa.

21Yawe aliongea nanyi mulipokuwa katika ustawi,

lakini ninyi mukasema: Hatutasikiliza.

Hii ndiyo tabia yenu tangu utoto wenu,

hamujatii sauti ya Yawe.

22Waongozi wenu watapeperushwa na upepo,

wapenzi wenu watapelekwa katika uhamisho.

Halafu mutapata haya na kufazaika,

kwa sababu ya uovu wenu wote.

23Enyi wakaaji wote wa Lebanoni,

ninyi munaokaa salama kati ya miti ya mierezi,

mutaugua sana

wakati mutakaposhikwa na uchungu unaokuwa

kama wa mwanamuke anayezaa!

Hukumu ya Mungu juu ya Konia

24Yawe anasema hivi: Kama vile ninavyoishi, hata kama wewe Konia mwana wa Yoyakimu, mufalme wa Yuda, ungekuwa wa lazima kwangu kama vile pete yangu ya muhuri ninayovaa kwa mukono wangu wa kuume, ningekuvua.

25Nitakutoa katika mikono ya wale wanaovizia maisha yako, ndiyo mikono ya wale unaowaogopa, hata katika mikono ya Nabukadneza, mufalme wa Babeli na watu wake.

26Nitakupeleka mbali katika inchi ya kigeni, wewe pamoja na mama yako muzazi. Mutakuwa watumwa katika inchi hiyo ambamo ninyi wote wawili hamukuzaliwa, nanyi mutakufia kulekule.

27Mutatamani kwa hamu kubwa kurudi katika inchi hii, lakini hamutarudi.

28Mbona huyu mutu Konia,

amekuwa kama chungu kilichovunjika,

ambacho kinazarauliwa na kutupwa inje?

Kwa nini yeye na watoto wake wamefukuzwa,

wametupwa katika inchi wasiyoijua?

29Ee inchi, ee inchi, ee inchi!

Sikia neno la Yawe!

30Yawe anasema hivi:

Muandike mutu huyu kwamba hana watoto,

ni mutu ambaye hatafanikiwa katika maisha yake.

Maana hakuna hata mumoja wa wazao wake

atakayekiikalia kiti cha kifalme cha Daudi

na kutawala tena katika Yuda.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help