1Zaburi ya Solomono.
Ee Mungu, umujalie mufalme uwezo wa kufuata sheria yako,
umupe mwana wa mufalme haki yako.
2Atawale taifa lako kwa haki,
na wamasikini wako kwa sheria yako.
3Milima ilete ustawi kwa watu wako,
vilima vijae haki.
4Mufalme awatetee wamasikini wa taifa,
awasaidie wakosefu,
na kuwaangamiza watesaji.
5Mufalme aishi muda murefu kama jua,
na kama mwezi, kwa vizazi vyote.
6Akuwe kama manyunyu yanayolowanisha mashamba,
kama mvua inayonyeshea udongo.
7Haki istawi maisha yake yote,
na amani kwa wingi mpaka mwezi ukome.
8Atawale kutoka bahari hata bahari,
kutoka muto Furati hata miisho ya dunia.
9Waadui zake wanaokaa katika jangwa wanyenyekee mbele yake,
wapinzani wake walambule vumbi.
10Wafalme wa Tarsisi na visiwa wamulipe kodi,
wafalme wa Sheba na Seba wamuletee zawadi.
11Wafalme wote wa dunia wamuheshimu,
watu wa mataifa yote wamutumikie.
12Atamukomboa mukosefu anayemwomba,
na masikini asiyekuwa na wa kumusaidia.
13Atawahurumia wazaifu na wakosefu,
atayaokoa maisha yao wenye shida.
14Atawatoa katika mateso na ukali,
maana maisha yao ni ya bei kubwa kwake.
15Mufalme aishi maisha marefu;
apokee zawadi ya zahabu kutoka Sheba;
watu wamwombee kwa Mungu siku zote,
na kumutakia baraka muchana kutwa.
16Inchi itoe mazao kwa wingi,
vilima vijae mavuno kama ya Lebanoni,
na watu wa miji wastawi kama majani.
17Jina la mufalme litukuzwe siku zote;
utukufu wake udumu muda wote jua litakapokuwa.
Kwake mataifa yote yabarikiwe;
watu wote wamwite mwenye heri!
18Atukuzwe Yawe, Mungu wa Israeli,
ambaye peke yake anafanya miujiza.
19Jina lake tukufu litukuzwe milele;
utukufu wake ujae katika ulimwengu wote!
Amina, Amina!
20Mwisho wa maombi ya Daudi mwana wa Yese.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.