1Lakini jambo hilo halikumupendeza Yona hata kidogo, akakasirika sana.
2Kwa hiyo akaomba: Yawe, si hayo ndiyo mambo yaleyale niliyowaza utayafanya nilipokuwa katika inchi yangu? Ndiyo maana nilifanya haraka kukimbilia Tarsisi. Nilijua kwamba wewe ni Mungu ambaye umejaa huruma na rehema, haukasiriki upesi, wewe ni mwingi wa wema, na tayari kubadilisha nia yako kusudi usiazibu.
3Basi, sasa ee Yawe, ninakusihi uniondoe uzima wangu, maana ni vizuri kwangu kufa kuliko kuishi.
4Naye Yawe akamujibu Yona: Unazani kwamba unafanya vema kukasirika?
5Halafu Yona akatoka inje ya muji, akajiikalia upande wa mashariki wa muji huo. Pale, akajijengea kibanda, akaikaa chini ya kivuli chake akingojea apate kuona jambo litakaloupata muji wa Ninawe.
6Mungu, Yawe akaamuru mumea uote na kukomaa. Akauotesha kwa kumupatia Yona kivuli cha kumupunguzia taabu aliyokuwa nayo. Yona akaufurahia sana mumea huo.
7Lakini kesho yake kulipopambazuka, Mungu akaamuru mududu uharibu mumea huo. Ukanyauka.
8Jua lilipotokea, Mungu akaleta upepo mukali kutoka upande wa jangwa, jua likamuchoma sana Yona juu ya kichwa, karibu azimie. Akatamani kufa, akisema: Ni vizuri kwangu kufa kuliko kuishi.
9Lakini Mungu akamwuliza Yona: Unazani unafanya vema kuukasirikia mumea huo? Yona akajibu: Ndiyo, ninafanya vema kukasirika – kukasirika hata kufa!
10Basi Mungu akamwambia: Mumea huu uliota na kukomaa kwa usiku mumoja, na usiku uliofuata ukanyauka. Wewe haukuufanyia kitu chochote, wala haukuuotesha. Mbona unausikilia huruma?
11Basi, haifai kwangu kuuhurumia Ninawe, ule muji mukubwa wenye watu elfu mia moja na makumi mbili, wasioweza kutambua linalokuwa jema na baya; na nyama wengi wasiokuwa na hesabu?
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.