1Maombi ya Musa, mutu wa Mungu.
Ee Bwana, tangia vizazi vyote,
wewe umekuwa usalama wetu.
2Mbele milima haijakuwa,
mbele haujauumba ulimwengu,
wewe ndiwe Mungu, milele na milele.
3Unawarudisha watu katika mavumbi walimotoka,
ukisema: “Wanadamu, murudi!”
4Kwako miaka elfu moja ni kama siku moja tu,
ni kama jana ambayo imekwisha pita,
ni kama makesha ya usiku mumoja.
5Unatowesha mbali watu kama ndoto!
Wanadamu ni kama majani yanayochipuka asubui:
6asubui yanachipuka na kuchanua,
magaribi yamekwisha nyauka na kukauka.
7Hasira yako inatuangamiza;
tunatishwa na kasirani yako.
8Maovu yetu umeyaweka mbele yako;
zambi zetu za siri ziko wazi mbele yako.
9Kwa hasira yako maisha yetu yanatoweka,
yanaisha kama pumzi.
10Muda wa maisha yetu ni miaka makumi saba,
au tukikuwa wenye afya, miaka makumi nane;
lakini yote ni shida na taabu!
Siku zinapita mbio, nasi tunatoweka!
11Nani anayetambua uzito wa hasira yako?
Nani anayeona matokeo ya kasirani yako?
12Utufundishe ufupi wa maisha yetu
kusudi tuweze kuwa na hekima.
13Ee Yawe, urudie!
Utakasirika mpaka wakati gani?
Utuonee huruma sisi watumishi wako.
14Utushibishe wema wako kila asubui,
tupate kushangilia na kufurahi maisha yetu yote.
15Utujalie sasa miaka mingi ya furaha,
kama ulivyotupa miaka mingi ya shida na taabu.
16Utuonyeshe matendo yako sisi watumishi wako;
uwaonyeshe wazao wetu utukufu wako.
17Utuonyeshe uzuri wako, ee Bwana, Mungu wetu;
uimarishe kazi zetu,
uziimarishe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.