1Barua hii inatoka kwangu mimi muzee. Ninakuandikia wewe mama uliyechaguliwa na Mungu, pamoja na watoto wako ninaowapenda hakika. Wala si mimi peke tu ninayewapenda, lakini vilevile wale wote wanaojua ule ukweli wanawapenda ninyi,
2kwa sababu ukweli huu unakaa ndani yetu nao utakuwa pamoja nasi hata milele.
3Mungu Baba pamoja na Yesu Kristo, Mwana wa Baba, watatujalia neema, huruma na amani katika ukweli na upendo.
Kuishi katika ukweli na upendo4Nilifurahi sana kuona kwamba wamoja kati ya watoto wako wanaishi katika ukweli kama vile Baba alivyotuamuru.
5Na sasa Mama, ninakusihi: tupendane. Basi hii si amri mupya ninayokuandikia, lakini ni amri ile tuliyopokea tangu mwanzo.
6Na upendo ni kuishi katika kutii amri za Mungu. Hii ndiyo ile amri muliyoisikia tangu mwanzo: muishi katika upendo.
7Kwa maana wadanganyifu wengi wametokea katika dunia. Watu hawa hawakubali kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili wa kimutu. Yule asiyekubali vile ni mudanganyifu na mupinga Kristo.
8Basi, mujiangalie wenyewe, kusudi musipoteze matunda ya kazi yenu, lakini mupokee zawadi kamili.
9Kila mutu atakayeenda mbali na asiyedumu katika mafundisho ya Kristo, mutu yule hashirikiani na Mungu. Lakini yule anayedumu katika mafundisho yale, anashirikiana na Baba na Mwana vilevile.
10Mutu akikuja kwenu, naye asipowafundisha mafundisho haya, musimukaribishe ndani ya nyumba yenu, wala musimusalimie;
11maana mwenye kumusalimia anashirikiana naye katika matendo yake mabaya.
Salamu za mwisho12Nina maneno mengi ya kuwaambia, lakini sitaki kuyaandika ndani ya barua. Ninatumaini nitawatembelea na kusemezana pamoja nanyi uso kwa uso, kusudi tupate kujazwa na furaha kabisa.
13Upokee salamu za watoto wa dada yako aliyechaguliwa na Mungu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.