1Nitaimba juu ya rafiki yangu, wimbo wa rafiki yangu na shamba lake la mizabibu:
Rafiki yangu alikuwa na shamba la mizabibu
juu ya kilima chenye udongo muzuri.
2Alililima vizuri na kuondoa mawe yote,
akapanda humo mizabibu bora,
alijenga munara wa ulinzi katikati yake,
akachimba kikamulio cha divai.
Kisha akatazamia lizae zabibu nzuri.
Lakini likazaa zabibu chungu.
3Kwa hiyo rafiki yangu anasema hivi:
Enyi wakaaji wa Yerusalema na watu wa Yuda,
tafazali mukuwe waamuzi kati yangu na shamba langu.
4Ni kitu gani nilichokosa kulifanyia shamba langu?
Nilipotazamia lizae zabibu nzuri,
mbona basi, likazaa zabibu chungu?
5Na sasa nitawaambia jinsi
nitakavyolifanya hilo shamba langu.
Nitaubomoa upango wake,
nalo litaharibiwa.
Nitaubomoa ukuta wake,
nalo litakanyagwakanyagwa.
6Nitalifanya ukiwa kabisa,
mizabibu yake haitasafishwa matawi wala kupaliliwa.
Litaota michongoma na miiba.
Tena nitayaamuru mawingu
yasinyeshe mvua juu yake.
7Shamba la mizabibu la Yawe wa majeshi
ni taifa la Waisraeli,
na mizabibu mizuri aliyoipanda ni watu wa Yuda.
Yeye alitazamia watu wafuate sheria yake,
akaona mauaji;
alitazamia haki,
alisikia kilio!
Maovu watu wanayotenda8Ole kwao wanaoongeza nyumba juu ya nyumba,
wanaoongeza mashamba juu ya mashamba yao,
mpaka kila sehemu inakuwa mali yao,
na hakuna nafasi kwa wengine katika inchi.
9Nimemusikia Yawe wa majeshi akisema hivi:
Hakika nyumba nyingi zitabaki tupu,
zile kubwa na nzuri zitabaki wazi bila wakaaji.
10Shamba la mizabibu lenye hektari kumi
litatoa litre makumi tano tu za divai;
anayepanda kilo mia moja za mbegu
atavuna kilo kumi tu.
11Ole kwao wanaoamuka asubui mapema
wapate kukimbilia kinywaji cha kulewesha;
wanaokesha hata usiku,
mpaka divai iwaleweshe!
12Katika karamu zao, hapakosekani vinubi,
zeze, ngoma, filimbi na divai.
Lakini hawajali matendo ya Yawe,
wala kutambua kazi za mikono yake.
13Kwa hiyo, watu wangu watapelekwa katika uhamisho
kwa sababu ya ukosefu wao wa akili.
Wakubwa wao watakufa na njaa,
watu wengi watakufa na kiu.
14Kuzimu inawangoja kwa hamu kubwa,
imepanua kinywa chake mpaka mwisho.
Waheshimiwa pamoja na watu wengine wa Yerusalema
wanaingia humo makundi kwa makundi,
vilevile na wote wanaushangilia kwa furaha.
15Kila mutu atafezeheshwa,
na wenye kiburi wote watapatishwa haya.
16Lakini Yawe wa majeshi anatukuzwa
wakati sheria yake inafuatwa.
Utakatifu wa Mungu Mutakatifu unaonyeshwa
wakati haki inatendwa.
17Wana-kondoo watakula majani kule,
kama vile katika shamba la kuwakulishia.
Wana-mbuzi wanono watatafuta chakula chao kule kule.
18Ole kwao wanaokokota uovu kama kwa kamba;
wanaoburura zambi kama wanavyokokota gari.
19Wanasema:
Muache Yawe afanye haraka,
tunataka kuona yale aliyosema atayafanya!
Mutakatifu wa Israeli atimize basi kusudi lake
kusudi tuone ana mipango gani!
20Ole kwao wanaosema ubaya ni uzuri
na uzuri ni ubaya.
Wanasema giza ni mwangaza
na mwangaza ni giza.
Wanasema kichungu ni kitamu
na kitamu ni kichungu.
21Ole kwao wanaojiona kuwa wenye hekima na akili.
22Ole kwao wanaokuwa wafundi wa kunywa divai,
wanaokuwa hodari sana wa kuchanganya vinywaji vya kulewesha.
23Kwa ajili ya kituliro kidogo wanawaachilia wenye kosa
na kuwanyima wasiokuwa na kosa haki yao.
24Kwa hiyo, kama vile moto unavyoteketeza nyasi,
kama vile majani yanavyotoweka ndani ya moto,
ndivyo mizizi yao itakavyooza,
na maua yao yatakavyopeperushwa juu kama mavumbi.
Maana wameacha sheria ya Yawe wa majeshi,
wamezarau neno la yule Mutakatifu wa Israeli.
25Kwa hiyo hasira ya Yawe iliwawakia watu wake,
akaunyoosha mukono wake juu yao, akawaazibu.
Milima ikatetemeka,
maiti zao zikakuwa kama takataka katika barabara za muji.
Hata hivyo, hasira yake haijatulia,
angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.
26Yawe ananyunyua bendera kwa kuita taifa la mbali;
anawapigia filimbi watu kutoka miisho ya dunia;
nao wanakuja mbio na kufika haraka!
27Hawachoki wala hawajikwai;
hawasinzii wala hawalali;
hakuna mukaba wao uliofunguka
wala kamba ya kiatu iliyokatika.
28Mishale yao ni mikali sana,
pinde zao zimevutwa tayari.
Kwato za farasi wao ni ngumu kama mawe;
mwendo wa magurudumu ya magari ni kama wa upepo mukali.
29Waaskari wao wananguruma kama simba;
wananguruma kama simba wakali
ambao wamekamata nyama wao
na kuwapeleka mbali
ambapo hakuna anayeweza kuwanyanganya.
30Siku hiyo, watanguruma juu ya Israeli
kama uvumi wa bahari iliyochafuka.
Atakayeiangalia inchi kavu
ataona giza tupu na taabu,
mwangaza utafunikwa na mawingu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.