1Yakobo akawaita wana wake, akasema: “Mukusanyike pamoja niwaambie mambo yatakayowapata siku zinazokuja.
2“Mukusanyike musikie, enyi wana wa Yakobo,
munisikilize mimi Israeli, baba yenu.
3“Wewe Rubeni ni muzaliwa wangu wa kwanza,
nguvu yangu na tunda la ujana wangu.
Wewe unawapita wandugu zako kwa ukubwa na nguvu.
4Wewe ni kama maji ya mafuriko.
Lakini hautakuwa wa kwanza tena,
maana ulipanda juu ya kitanda changu mimi baba yako,
wewe ulikichafua;
hakika wewe ulipanda juu yake!
5“Simeoni na Lawi ni wandugu:
wanatumia silaha zao kutesa kwa ukali,
6lakini mimi sitashiriki mashauri yao mabaya.
Ee roho yangu, usishiriki mikutano yao,
maana, katika hasira yao, walimwua mutu,
kwa mapenzi yao walikata mushipa wa ngombe.
7Ninalaani hasira yao kali sana
na kasirani yao isiyokuwa na huruma.
Nitawatawanya katika inchi ya Yakobo,
nitawasambaza katika inchi ya Israeli.
8“Wewe Yuda, wandugu zako watakusifu.
Mukono wako utashika shingo la waadui zako,
na wandugu zako watainama mbele yako.
9Wewe Yuda, mwana wangu, ni kama mwana-simba
ambaye amepata mawindo yake akapanda juu,
kama simba mukali anajinyoosha na kulala chini.
Simba dike, nani anayesubutu kumwamusha?
10Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda,
wala bakora ya utawala kwenye miguu yake,
mpaka atakapofika yule ambaye ni yake;
ambaye mataifa yatamutii.
11Atafunga punda wake katika muzabibu
na mwana-punda wake kwenye muzabibu bora.
Atafua nguo zake katika divai,
na kanzu zake katika divai nyekundu.
12Macho yake ni mekundu kwa divai,
meno yake ni meupe kwa maziwa.
13“Zebuluni ataishi pembeni ya bahari,
kivuko chake kitakuwa pahali pa kuegesha mashua.
Mupaka wa inchi yake ni Sidona.
14“Isakari ni kama punda mwenye nguvu,
anayejilaza kati ya mizigo yake.
15Aliona kwamba pahali pa kupumzikia ni pazuri,
na kwamba inchi ni ya kupendeza,
akauinamisha mugongo wake kubeba muzigo,
akakuwa mutumwa kwa kufanya kazi za kinguvu.
16“Dani atakuwa mwamuzi wa watu wake,
kama moja ya makabila ya Israeli.
17Atakuwa kama nyoka katika njia,
nyoka mwenye sumu kando ya njia,
anayeuma visigino vya farasi,
naye mupanda-farasi anaanguka machali.
18“Ee Yawe, ninangojea uniokoe!
19“Gadi atashambuliwa na wanyanganyi,
lakini yeye atawafuata nyuma na kuwashambulia.
20“Inchi ya Aseri itatoa mavuno kwa wingi,
naye atatoa chakula kinachofaa kwa mufalme.
21“Nafutali ni kama pongo anayekuwa huru,
anayezaa watoto wanaokuwa wazuri.
22“Yosefu ni kama muti unaozaa,
muti unaozaa kando ya chemichemi,
matawi yake yanatanda kwenye ukuta.
23Wapiga mishale walimushambulia vikali,
wakamutupia mishale na kumusumbua sana.
24Lakini upinde wake bado imara,
na mikono yake imepewa nguvu,
kwa uwezo wa Mwenye Nguvu wa Yakobo,
kwa jina la Muchungaji, Mulinzi wa Israeli.
25Mungu wa baba yako atakusaidia,
Mungu Mwenye Nguvu atakubariki,
upate baraka za mvua toka juu mbinguni,
baraka za maji ya vilindi vinavyokuwa chini,
baraka za uzazi wa wamama na nyama.
26Baraka za baba yako zishinde baraka za milima ya milele,
zikuwe bora kuliko vilima vya kale.
Baraka hizo zikuwe juu ya kichwa cha Yosefu,
juu ya paji lake yeye aliyekuwa ametengwa na wandugu zake.
27“Benjamina ni imbwa mwitu mukali,
asubui anakula mawindo yake,
na magaribi anagawanya vitu alivyonyanganya.”
28Hayo ndiyo makabila kumi na mawili ya Israeli, na hayo ndiyo maneno baba yao aliyowaambia alipowabariki, kila mumoja wao kama alivyostahili.
Kifo cha Yakobo29Kisha Israeli akawaagiza wana wake hivi: “Mimi niko karibu kufa na kwenda kukutana na watu wangu. Munizike pamoja na wazee wangu katika pango linalokuwa katika shamba la Efuroni Muhiti,
30kule Makipela, upande wa mashariki wa Mamure, katika inchi ya Kanana. Abrahamu alinunua pango na shamba hilo kwa Efuroni, Muhiti, likuwe lake la kuzikia.
31Kule ndiko walikozikwa Abrahamu na muke wake Sara, kule ndiko walikozika Isaka na muke wake Rebeka, na kule ndiko nilikomuzika Lea.
32Shamba hilo na pango lake lilinunuliwa kwa Wahiti.”
33Yakobo alipomaliza kuwaagiza wana wake, akarudisha miguu yake juu ya kitanda, akakufa na kukutana na wazee wake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.