1Heri ungekuwa kaka yangu,
ambaye amenyonyeshwa na mama yangu!
Hivyo, hata kama ningekutana nawe inje,
ningekubusu na hakuna ambaye angenizarau.
2Ningekuongoza na kukufikisha ndani ya nyumba ya mama muzazi,
pahali ambapo ungenifundisha upendo.
Ningekupa divai nzuri iliyokolezwa,
ningekupa divai yangu ya makomamanga yangu.
3Mukono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu,
mukono wake wa kuume unanikumbatia.
4Ninawasihi, enyi wabinti wa Yerusalema,
musichochee wala kuamusha mapenzi,
mpaka wakati wake utakapofika.
Shairi la sitaWabinti5Ni nani huyu anayekuja kutoka katika jangwa,
akimwegemea mupenzi wake?
Masemi ya mukeMimi nilikuamusha chini ya muti wa mutofaa,
pale ambapo mama yako aliona uchungu,
pale ambapo mama yako alikuzaa.
6Unipige kama muhuri ndani ya moyo wako,
kama muhuri katika mikono yako.
Maana mapendo yana nguvu kama kifo,
nao wivu ni mukali kama kaburi.
Kuwaka kwake ni kama kuwaka kwa moto,
unawaka kama ulimi wa moto.
7Maji mengi hayawezi kuyazimisha hata kidogo,
mafuriko hayawezi kuyazimisha.
Mutu akijaribu kununua mapenzi,
na kutoa mali yake yote,
atakachopata ni mazarau mutupu.
Masemi ya wandugu za muke8Tuna dada mudogo,
ambaye bado hajaota maziba.
Basi, tutamufanyia dada yetu nini
siku atakapochumbiwa?
9Kama angalikuwa ukuta,
tungalimujengea munara wa feza;
na kama angalikuwa mulango,
tungaliupigilia kwa mbao za mierezi.
Masemi ya muke10Mimi nilikuwa ukuta,
na maziba yangu kama minara yake.
Mbele yake nilikuwa
kama mwenye kupata amani.
Masemi ya mume11Solomono alikuwa na shamba la mizabibu,
pahali panapoitwa Bali-Hamoni.
Alilipangisha kwa walinzi;
kila mumoja wao alilipa vikoroti elfu moja vya feza.
12Shamba langu la mizabibu ni shamba langu mwenyewe.
Basi, Solomono, wewe ukae na elfu zako za feza,
na kila mulinzi wa matunda akae na mia mbili zake.
13Ewe unayekuwa katika shamba,
warafiki zangu wanasikiliza sauti yako;
basi nami niisikilize tafazali!
Masemi ya muke14Kuja mbio, ewe mupenzi wangu,
kama paa au kitoto cha pongo
juu ya milima ya marasi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.