Wimbo wa Solomono 8 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Heri ungekuwa kaka yangu,

ambaye amenyonyeshwa na mama yangu!

Hivyo, hata kama ningekutana nawe inje,

ningekubusu na hakuna ambaye angenizarau.

2Ningekuongoza na kukufikisha ndani ya nyumba ya mama muzazi,

pahali ambapo ungenifundisha upendo.

Ningekupa divai nzuri iliyokolezwa,

ningekupa divai yangu ya makomamanga yangu.

3Mukono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu,

mukono wake wa kuume unanikumbatia.

4Ninawasihi, enyi wabinti wa Yerusalema,

musichochee wala kuamusha mapenzi,

mpaka wakati wake utakapofika.

Shairi la sitaWabinti

5Ni nani huyu anayekuja kutoka katika jangwa,

akimwegemea mupenzi wake?

Masemi ya muke

Mimi nilikuamusha chini ya muti wa mutofaa,

pale ambapo mama yako aliona uchungu,

pale ambapo mama yako alikuzaa.

6Unipige kama muhuri ndani ya moyo wako,

kama muhuri katika mikono yako.

Maana mapendo yana nguvu kama kifo,

nao wivu ni mukali kama kaburi.

Kuwaka kwake ni kama kuwaka kwa moto,

unawaka kama ulimi wa moto.

7Maji mengi hayawezi kuyazimisha hata kidogo,

mafuriko hayawezi kuyazimisha.

Mutu akijaribu kununua mapenzi,

na kutoa mali yake yote,

atakachopata ni mazarau mutupu.

Masemi ya wandugu za muke

8Tuna dada mudogo,

ambaye bado hajaota maziba.

Basi, tutamufanyia dada yetu nini

siku atakapochumbiwa?

9Kama angalikuwa ukuta,

tungalimujengea munara wa feza;

na kama angalikuwa mulango,

tungaliupigilia kwa mbao za mierezi.

Masemi ya muke

10Mimi nilikuwa ukuta,

na maziba yangu kama minara yake.

Mbele yake nilikuwa

kama mwenye kupata amani.

Masemi ya mume

11Solomono alikuwa na shamba la mizabibu,

pahali panapoitwa Bali-Hamoni.

Alilipangisha kwa walinzi;

kila mumoja wao alilipa vikoroti elfu moja vya feza.

12Shamba langu la mizabibu ni shamba langu mwenyewe.

Basi, Solomono, wewe ukae na elfu zako za feza,

na kila mulinzi wa matunda akae na mia mbili zake.

13Ewe unayekuwa katika shamba,

warafiki zangu wanasikiliza sauti yako;

basi nami niisikilize tafazali!

Masemi ya muke

14Kuja mbio, ewe mupenzi wangu,

kama paa au kitoto cha pongo

juu ya milima ya marasi.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help