1Kwa mwisho, wandugu, sisi tumewafundisha namna gani munavyopaswa kuishi kusudi mupate kumupendeza Mungu. Na kweli, ni vile munavyoishi. Na sasa, tunawaomba na kuwasihi kwa jina la Bwana Yesu, muendelee mbele vizuri zaidi katika mwenendo ule.
2Kwa maana munajua maagizo gani tuliyowatolea kutoka kwa Bwana Yesu.
3Kitu Mungu anachotaka ni kwamba mukuwe watakatifu na muepuke mambo ya uasherati.
4Kila mwanaume anapaswa kujua namna ya kuishi na muke wake katika hali ya utakatifu na ya heshima,
5bila kujiachilia kutawaliwa na tamaa mbaya kama vile wapagani wasioamini Mungu.
6Kuelekea maneno hayo, mutu yeyote asimukosee ndugu yake wala kumudanganya. Tumekwisha kuwaambia na kuwahakikishia mbele kwamba Bwana atawaazibu wale wanaofanya mambo kama hayo.
7Kwa maana Mungu hakutuita kusudi tuishi katika uchafu, lakini katika utakatifu.
8Basi kwa hiyo, yeye anayekataa mafundisho haya hamukatai mutu, lakini anamukataa Mungu anayewapa ninyi Roho wake Mutakatifu.
9Na kuelekea upendo wa wandugu waamini, si lazima kwenu kuwaandikia neno lolote, kwa maana Mungu yeye mwenyewe amewafundisha ninyi kupendana.
10Ni vile mulivyojionyesha mbele ya wandugu wote wa kanisa la Makedonia. Na sasa tunawasihi ninyi wandugu, muendelee mbele vizuri zaidi katika jambo lile.
11Mufanye bidii sana mupate kuishi katika amani. Mushugulike na mambo yenu ninyi wenyewe na kufanya kazi kwa mikono yenu wenyewe sawa vile tulivyokwisha kuwaagiza.
12Hivi mutakuwa na mwenendo wa heshima mbele ya watu wasiokuwa wa Kristo, wala hamutahitaji kusaidiwa na mutu yeyote.
Kurudia kwa Bwana13Wandugu, hatutaki mukose kujua habari zinazowaelekea wale waliokufa, kusudi musikuwe na huzuni sawa vile watu wasiokuwa na tumaini la kufufuka.
14Tunaamini kwamba Yesu alikufa na alifufuliwa, na kwa hiyo tunaamini vilevile kwamba Mungu atawafufua pamoja na Yesu wale waliokufa wakimwamini Yesu.
15Kwa maana, kufuatana na mafundisho ya Bwana, tunawaambia hivi: sisi tutakaokutiwa wazima wakati Bwana atakaporudia, hatutawatangulia wale waliokufa.
16Kwa sababu amri itakapotoka na sauti ya malaika mukubwa itakaposikilika, na baragumu ya Mungu itakapolia, Bwana mwenyewe atashuka toka mbinguni. Halafu wale waliokufa wakimwamini Kristo watafufuliwa kwanza.
17Na kisha sisi tutakaokutiwa wazima wakati ule, tutanyanyuliwa pamoja nao katika mawingu kwa kukutana na Bwana katika anga. Na hivi tutakaa siku zote pamoja na Bwana.
18Basi ninyi mufarijiane kwa maneno haya.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.