1Katika maono mengine, niliona pembe ine.
2Nami nikamwuliza yule malaika aliyezungumuza nami: Pembe hizi zina maana gani? Yeye akanijibu: Pembe hizi zina maana ya yale mataifa ambayo yaliwatawanya watu wa Yuda, Israeli na Yerusalema.
3Kisha, Yawe akanionyesha wafuachuma wane.
4Nami nikauliza: Watu hawa wanakuja kufanya nini? Yeye akanijibu: Watu hawa wamekuja kuyatisha na kuyaangamiza yale mataifa yenye nguvu ambayo yaliishambulia inchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.
Maono ya tatu: Kamba ya kupima5Katika maono mengine, nilimwona mutu aliyekuwa na kamba ya kupima katika mukono wake.
6Basi, nikamwuliza: Unakwenda wapi? Naye akanijibu: Ninakwenda kuupima urefu na upana wa Yerusalema.
7Yule malaika aliyezungumuza nami akaenda kukutana na malaika mwingine ambaye alikuwa anakuja kwake.
8Basi, huyo malaika aliyezungumuza nami akamwambia yule mwenzake: Kimbia umwambie yule kijana kwamba si lazima Yerusalema ukuwe na kuta, kama sivyo hapatakuwa nafasi ya kuwatoshelea wakaaji wake wengi na nyama watakaokuwa ndani yake.
9Yawe anasema kwamba yeye mwenyewe atakuwa ukuta wa moto kwa kuulinda muji huo pande zote, naye atakaa mule kwa utukufu wake.
Waliohamishwa wanaitwa warudie kwao10Yawe anasema hivi: Mukimbie kutoka katika inchi ya kaskazini ambako mimi nilikuwa nimewatawanya kila upande.
11Haraka! Ninyi wote munaokaa katika inchi ya Babeli, mukimbilie Sayuni!
12Yawe wa majeshi, ambaye kwa utukufu wake amenituma, anasema hivi juu ya mataifa yaliyowakamata mateka watu wake: Hakika, anayewagusa ninyi anagusa mboni ya jicho langu.
13Kweli, nitawashambulia wale waliowakamata mateka, nao watakamatwa mateka na wale waliowafanya watumwa wao. Halafu kwa hiyo mutajua kwamba Yawe wa majeshi ndiye aliyenituma.
14Yawe anasema hivi: Enyi watu wa Sayuni, muimbe na kufurahi kwa maana ninakuja na kukaa kati yenu.
15Mataifa mengi yatajiunga nami Yawe, nao watakuwa watu wangu; nami nitakaa kati yenu. Halafu mutajua kwamba Yawe wa majeshi ndiye aliyenituma kwenu.
16Watu wa Yuda watakuwa tena mali ya pekee ya Yawe katika inchi takatifu, na Yerusalema itakuwa tena muji wake aliouchagua.
17Enyi wanadamu wote, munyamaze mbele ya Yawe, maana, yeye anakuja kutoka makao yake matakatifu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.