1Yawe akatoa ujumbe huu kwa njia ya nabii Yeremia juu ya inchi ya Babeli, ile inchi ya Wakaldea:
2Mutangaze kati ya mataifa,
munyanyue bendera na kutangaza,
musifiche jambo lolote. Museme:
Babeli umetekwa,
mungu Beli amepatishwa haya.
Merodaki amefazaishwa;
sanamu zake zimefezeheshwa,
miungu yake imefazaishwa.
3Kwa maana, taifa kutoka kaskazini limefika kuushambulia; litaifanya inchi yake kuwa uharibifu. Hakuna atakeyeishi humo; watu na nyama watakimbia mbali.
Kurudi kwa Waisraeli4Siku hizo na wakati huo, watu wa Israeli na watu wa Yuda watakusanyika pamoja na kuja wakilia na kutafuta Yawe, Mungu wao.
–Ni ujumbe wa Yawe.
5Watauliza njia ya kwenda Sayuni, na nyuso zao zikielekea huko, wakisema: Mukuje! Nao watajiunga na Yawe katika agano la milele ambalo halitasahauliwa hata kidogo.
6Watu wangu walikuwa kama kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha, wakawageuza kuelekea kwenye milima; walitembea toka mulima mpaka kilima, wakasahau makao yao.
7Watu wote waliowakuta waliwaua, na waadui zao wamesema: Sisi hatuna kosa, maana hao wamemukosea Yawe anayekuwa makao yao ya kweli; Yawe ambaye ni tegemeo la babu zao!
8Mukimbie kutoka Babeli! Mutoke inje ya ile inchi ya Wakaldea, mukuwe kama mabeberu mbele ya kundi.
9Maana, mimi nitachochea mataifa makubwa kutoka inchi ya kaskazini washambulie inchi ya Babeli. Watajitayarisha kuishambulia inchi ya Babeli na kuiteka. Mishale yao ni kama shujaa hodari asiyerudi mikono mitupu.
10Inchi ya Wakaldea itanyanganywa, na hao watakaoinyanganya watashiba.
–Ni ujumbe wa Yawe.
Kuanguka kwa Babeli11Enyi wanyanganyi wa mali yangu,
ijapokuwa munafurahi na kushangilia,
munarukaruka kama mwana-ngombe anayepepeta ngano,
na kulia kama farasi dume,
12lakini inchi yenu ya kuzaliwa itapatishwa haya;
hiyo inchi mama yenu, itafezeheshwa.
Babeli itakuwa ya mwisho kati ya mataifa,
itakuwa mbuga yenye kukauka na jangwa.
13Kwa sababu ya kasirani yangu Yawe,
Babeli haitakaliwa kabisa na watu,
lakini itakuwa jangwa kabisa;
kila mutu atakayepita karibu nayo atashangaa,
ataizomea kwa sababu ya mapigo yake.
14Enyi wafundi wote wapiga mishale,
mujipange kwa kuzunguka muji wa Babeli kwa vita;
mupige mishale, musiache mushale hata mumoja,
maana umenikosea mimi Yawe.
15Mupigie kelele za vita pande zote;
sasa Babeli umejitoa ukamatwe.
Vikingio vyote vimeanguka,
kuta zake zimebomolewa.
Ni malipizi ya Yawe.
Basi muulipize kisasi.
Muutendee kama vile ulivyotendea wengine.
16Muzuie watu wasipande mbegu Babeli,
wala wasivune wakati wa mavuno.
Kutokana na upanga wa uharibifu,
kila mumoja atawarudilia watu wake,
kila mumoja atakimbilia katika inchi yake.
17Israeli ni kama kondoo wanaowindwa na kufukuzwa na simba. Kwanza waliangamizwa na mufalme wa Asuria, na sasa Nebukadneza mufalme wa Babeli, amevunjavunja mifupa yake.
18Kwa hiyo Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi: Nitamwazibu mufalme wa Babeli na inchi yake, kama nilivyomwazibu mufalme wa Asuria.
19Nitawarudisha Waisraeli katika inchi yao, nao watakula mavuno yatakayolimwa juu ya mulima Karmeli na Basani na watatosheka kwa chakula kutoka milima ya Efuraimu na Gileadi.
20Siku hizo na wakati huo, uovu utatafutiwa katika inchi ya Israeli, lakini hautapatikana; zambi itatafutiwa katika inchi ya Yuda, lakini haitapatikana; maana mimi nitawasamehe wale ambao nimewaponyesha.
–Ni ujumbe wa Yawe.
21Mupande, muiendee inchi ya Merataimu,
muende kuishambulia;
muwashambulie wakaaji wa Pekodi
na kuwaangamiza kabisa watu wake.
–Ni ujumbe wa Yawe.–
Mufanye kila kitu nilichowaamuru.
22Kelele za vita zinasikilika katika inchi,
kuna uharibifu mukubwa.
23Jinsi gani huo muji uliokuwa nyundo iliyoponda dunia nzima
unavyoangushwa chini na kuvunjika!
Babeli umekuwa pori tupu
kati ya mataifa!
24Ewe Babeli, nilikutegea mutego ukanaswa,
wala haukujua kitu juu yake;
ulipatikana, ukakamatwa,
kwa sababu ulishindana nami Yawe.
25Nimefungua gala yangu ya silaha,
nikatoa humo silaha za kasirani yangu,
maana mimi Bwana wa wote, Yawe wa majeshi,
nina kazi ya kufanya
katika inchi ya Wakaldea.
26Mukuje kumushambulia kutoka kila upande;
muzifungue gala zake za chakula;
mumulundikie malundo ya ngano!
Muiangamize kabisa inchi hii;
musiache kitu chochote!
27Muwaue waaskari wake hodari;
muache washukie kwenye machinjo.
Ole kwao, maana siku yao imetimia,
wakati wao wa kuazibiwa umefika!
28Sikiliza! Wakimbizi na wenye kutoroka kutoka inchi ya Babeli wanakuja kutangaza huko Sayuni jinsi Yawe, Mungu wetu, alivyolipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake.
29Muwaite wapiga mishale waishambulie Babeli. Mupeleke kila mutu anayejua kuvuta upinde. Muuzunguke muji kusikuwe mutu yeyote atakayetoroka. Muulipize kadiri ya matendo yake yote; muutendee kama ulivyowatendea wengine, maana kwa kiburi ulinizarau mimi Yawe, Mutakatifu wa Israeli.
30Kwa hiyo, vijana wake watauawa katika mabarabara yake, na makundi yake yote ya waaskari yataangamizwa siku hiyo.
–Ni ujumbe wa Yawe.
31Mimi, ninapigana nawe, ewe mwenye kiburi.
–Ni ujumbe wa Bwana wa wote, Yawe wa majeshi.–
Maana siku yako ya azabu imefika,
wakati nitakapokuazibu umetimia.
32Mwenye kiburi atajikwaa na kuanguka,
wala hakutakuwa mutu wa kumwinua.
Nitawasha moto katika miji yake,
nao utateketeza kila kitu kandokando yake.
33Yawe wa majeshi anasema hivi: Watu wa Israeli wanagandamizwa pamoja na watu wa Yuda. Wale waliokamata mateka wamewabana sana na wanakataa kuwaachilia.
34Lakini mimi, Mukombozi wao ni mwenye nguvu. Yawe wa majeshi ndilo jina langu. Hakika nitatetea maneno yao kusudi nilete amani katika inchi yao, lakini taabu kwa wakaaji wa Babeli.
35Upanga ukuwe juu ya Wakaldea,
juu ya wakaaji wa Babeli
na wakubwa na wenye hekima wake!
–Ni ujumbe wa Yawe.–
36Upanga ukuwe juu ya waaguzi,
kusudi wakuwe wapumbafu!
Upanga ukuwe juu ya mashujaa,
kusudi waangamizwe!
37Upanga ukuwe juu ya farasi wake na magari yake,
juu ya majeshi yake yote ya mushahara,
kusudi wakuwe sawa na wanawake!
Upanga ukuwe juu ya hazina zake zote
kusudi zinyanganywe.
38Jua kali liyapige maji,
kusudi yapate kukauka!
Maana Babeli ni inchi inayojaa sanamu za miungu,
watu ni wenda-wazimu kwa sababu ya miungu yao.
39Kwa hiyo nyama wa pori, imbwa wa pori pamoja na mbuni, watakaa Babeli. Hakutakaliwa hata kidogo na watu wa vizazi vyote vinavyokuja.
40Kama vile mimi Yawe nilivyoiangamiza miji ya Sodoma na Gomora na miji ya jirani, vilevile hakutakuwa mutu yeyote atakayeishi humo. Kweli, hakuna mutu yeyote atakeyekaa huko.
–Ni ujumbe wa Yawe.
41Muangalie! Watu wanakuja toka inchi ya kaskazini;
taifa kubwa na wafalme wengi
linajitayarisha kutoka mbali kwa miisho ya dunia.
42Wameshika pinde zao na mikuki;
ni watu wakali wasiokuwa na huruma.
Vishindo vyao ni kama uvumi wa bahari,
wamepanda juu ya farasi.
Wamejipanga tayari kwa vita
na wewe Babeli!
43Mufalme wa Babeli amesikia habari zao.
Kwa hiyo, mikono yake ikaregea.
Ameshikwa na huzuni na uchungu,
kama mama anayezaa.
44Kama vile simba anavyotoka ndani ya vichaka vya muto Yordani na kuingia kwenye mbuga, ndivyo nitakavyowafukuza kwa rafla watu wake kutoka kwake. Nami nitamuweka huko mutawala yeyote nitakayemuchagua. Maana, ni nani anayeweza kulinganishwa nami? Nani anayeweza kunishitaki? Ni muchungaji gani anayeweza kunipinga?
45Kwa hiyo, musikilize mupango ambao Yawe amepanga juu ya Babeli pamoja na mambo aliyokusudia kuifanyia inchi ya Wakaldea: Hakika, watoto wao wadogo watakokotwa na kukamatwa; kweli kutakuwa mushangao mukubwa katika makao yao!
46Kwa kishindo cha kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka, na kilio chake kitasikilika kati ya mataifa mengine.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.