1“Musiwahukumu wengine kusudi Mungu asiwahukumu ninyi vilevile.
2Kwa maana mutahukumiwa kufuatana na namna munavyowahukumu wengine, na kipimo kile munachowapimia wengine ndicho kitakachotumiwa kwenu vilevile.
3Namna gani unaona vumbi inayokuwa ndani ya jicho la ndugu yako, lakini haufikiri juu ya nguzo inayokuwa ndani ya jicho lako?
4Au namna gani unaweza kumwambia ndugu yako kwamba aache umwondoe vumbi inayokuwa ndani ya jicho lake, wakati ndani ya jicho lako mwenyewe mungali ile nguzo?
5Wewe munafiki, ondosha kwanza nguzo kutoka ndani ya jicho lako, kisha utaweza kuona waziwazi na kuweza kuondoa ile vumbi inayokuwa ndani ya jicho la ndugu yako.
6“Musiwape imbwa vitu vitakatifu, kusudi wasiwageukie na kuwararua, wala musiwatupie nguruwe ushanga zenu za bei kusudi wasizikanyagekanyage.
Kuomba na kupewa(Lk 11.9-13)7“Muombe, nanyi mutapewa; mutafute, nanyi mutapata; mupige hodi, nanyi mutafunguliwa mulango.
8Kwa maana kila mutu anayeomba, anapewa; naye anayetafuta, anapata, naye anayepiga hodi, anafunguliwa.
9Ni nani kati yenu anayeweza kumupa mutoto wake jiwe kama akimwomba mukate?
10Au nani anaweza kumupa nyoka kama akimwomba samaki?
11Basi ikiwa ninyi munaokuwa waovu munajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, zaidi sana Baba yenu anayekuwa mbinguni atawapa wale wanaomwomba vitu vizuri zaidi.
12“Basi jambo lolote munalotaka wengine wawatendee, ninyi mulitende kwao vilevile, kwa maana kile ndicho kifungo cha Sheria ya Musa na mafundisho ya manabii.
Milango miwili(Lk 13.24)13“Muingie kwa kupitia mulango unaokuwa mwembamba. Kwa maana njia inayoongoza kufikia kwenye lufu ni kubwa, nao mulango unaoiingilia ni mupana, nao watu wanaoipitia ni wengi.
14Lakini njia inayoongoza kufikia kwenye uzima ni yenye kusongamana na mulango unaoiingilia ni mwembamba, nao watu wanaoifuata ni wachache tu.
Muti unajulikana kwa njia ya matunda yake(Lk 6.43-44)15“Mufanye angalisho na manabii wa uongo; kwa maana wanakuja kwenu wakionekana kwa inje kama vile kondoo, lakini ndani, wao ni kama imbwa wakali wa pori.
16Mutawatambua kwa matendo yao. Watu hawachumi matunda ya mizabibu au ya tini toka juu ya miti ya miiba.
17Na ni vile inavyokuwa: kila muti muzuri unazaa matunda mazuri, lakini kila muti mubaya unazaa matunda mabaya.
18Muti muzuri hauwezi kutoa matunda mabaya, wala muti mubaya hauwezi kutoa matunda mazuri.
19Kila muti usiozaa matunda mazuri unakatwa na kutupwa katika moto.
20Basi kwa hiyo, mutawatambua manabii wa uongo kwa njia ya matendo yao.
Wafusi wa kweli wa Yesu(Lk 13.25-27)21“Si kila mutu anayeniita ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa mbinguni, lakini yule tu anayefanya mapenzi ya Baba yangu anayekuwa mbinguni.
22Siku ile ya hukumu itakapotimia, wengi wataniambia: ‘Bwana, Bwana, sisi hatukutangaza ujumbe wa Mungu? Nasi hatukufukuza pepo kwa jina lako na kufanya maajabu mengi kwa jina lako?’
23Halafu mimi nitawaambia hivi waziwazi: ‘Sikuwajua ninyi hata siku moja. Mutoke karibu nami, ninyi watenda maovu.’
Mufano wa wajengaji wawili(Lk 6.47-49)24“Basi kila mutu anayesikia hayo maneno yangu na kuyashika, anafananishwa na mutu mwenye akili aliyejenga nyumba yake juu ya jiwe.
25Mvua ikanyesha, mito ikajaa, nao upepo ukavuma na kuishambulia nyumba ile, lakini haikuanguka, kwa sababu musingi wake ulikuwa umejengwa juu ya jiwe.
26“Lakini kila mutu anayesikia maneno ninayotoka kusema bila kuyashika, anafananishwa na mutu mupumbafu aliyejenga nyumba yake juu ya udongo wenye kichanga.
27Mvua ikanyesha, mito ikajaa, upepo ukavuma na kupiga nyumba ile, nayo ikaanguka na kubomoka kabisa.”
Mamlaka ya Yesu28Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, makundi ya watu wakashangaa sana kwa kuona namna alivyowafundisha;
29kwa maana hakuwafundisha sawa vile walimu wao wa Sheria, lakini kama vile mutu mwenye mamlaka.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.