Isaya 2 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Amani ya kudumu(Mika 4.1-3)

1Haya ndiyo mambo Isaya mwana wa Amozi aliyofunuliwa juu ya inchi ya Yuda na Yerusalema.

2Katika siku zinazokuja,

itatukia kwamba mulima wa nyumba ya Yawe

utaimarishwa kupita milima yote,

utainuliwa juu ya vilima vyote.

Mataifa yote yatajaa kule,

3watu wengi wataenda kule na kusema,

Mukuje tupandie kwenye mulima wa Yawe,

tuende kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo,

apate kutufundisha njia zake,

nasi tutafuata mapito yake.

Maana sheria itakuja kutoka Sayuni;

neno la Yawe kutoka Yerusalema.

4Mungu atafanya hukumu kati ya mataifa;

ataamua maneno kati ya watu wengi.

Watu watafua panga za vita kuwa majembe

na mikuki yao kuwa visu vya kuvuna.

Taifa halitapigana na taifa lingine

wala hayatafanya tena mazoezi ya vita.

5Sasa, enyi wazao wa Yakobo, mukuje,

tutembee katika mwangaza wa Yawe.

Kiburi kitaondolewa

6Sasa, ee Mungu, umewatupa watu wako, wazao wa Yakobo.

Maana kweli wachawi kutoka mashariki wamejaa kati yao;

kuna waaguzi kama vile kwa Wafilistini.

Wanashirikiana na watu wageni.

7Inchi yao imejaa feza na zahabu,

akiba yao ni kubwa zaidi.

Inchi yao imejaa farasi,

magari yao ya vita hayana hesabu.

8Inchi yao imejaa sanamu za miungu,

watu wake wanaabudu kazi ya mikono yao,

vitu walivyotengeneza wao wenyewe.

9Kwa hiyo, kila mutu atapata haya na kufezeheshwa.

Usiwasamehe hata kidogo, ee Mungu!

10Muingie chini ya jiwe,

mujifiche katika mavumbi,

kwa kuepuka kitisho cha Yawe,

mbali na mwangaza wa utukufu wake.

11Macho yenye kiburi ya wanadamu yatanyenyekezwa,

watu wenye majivuno watashushwa chini,

na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.

12Kweli, siku ya Yawe wa majeshi inakuja

juu ya wote wenye kiburi na majivuno,

juu ya wote wanaojitukuza,

13juu ya miti ya mierezi yote ya Lebanoni ambayo ni mirefu na mizuri,

juu ya miti ya mialo yote katika inchi ya Basani,

14juu ya milima yote mirefu,

juu ya vilima vyote vinavyoinuka juu sana;

15juu ya minara yote mirefu,

juu ya kuta zote ndefu,

16juu ya mashua yote makubwa ya Tarsisi,

na juu ya mashua yote mazuri.

17Kiburi cha wanadamu kitashushwa,

majivuno ya watu yatanyenyekezwa,

na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.

18Sanamu zote za miungu zitatoweka kabisa.

19Muingie katika mapango chini ya mawe,

katika mashimo ndani ya udongo,

kwa kuepuka kitisho cha Yawe,

mbali na mwangaza wa utukufu wake,

atakapokuja kuogopesha dunia.

20Siku hiyo, watu watawatupia panya na popo

sanamu za feza na zahabu

walizojitengenezea kusudi waziabudu.

21Nao wataingia katika mapango chini ya mawe

na kwenye nyufa za mawe,

kwa kuepuka kitisho cha Yawe,

mbali na mwangaza wa utukufu wake,

atakapokuja kuogopesha dunia.

22Usimutumainie mwanadamu,

uzima wake ni kama pumzi tu.

Yeye anafaa kitu gani?

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help