1Sikia! Hayo yote nimeyaona kwa macho yangu.
Nimeyasikia kwa masikio yangu mwenyewe na kuelewa.
2Yote munayoyajua, mimi vilevile ninayajua.
Mimi si mutu wa akili ndogo kuliko ninyi.
3Lakini ningependa kusema na Mungu Mwenye Uwezo,
ninatamani kujitetea mbele ya Mungu.
4Lakini ninyi munapakaa uongo chokaa,
ninyi wote ni waganga wasiofaa kitu.
5Heri mungekaa kimya kabisa,
muonekane kwamba muna hekima!
6Musikilize basi utetezi wangu,
munisikilize ninapojitetea.
7Munazani munamutumikia Mungu
kwa kusema uongo na udanganyifu?
8Munajaribu kumupendeza Mungu?
Mutamutetea Mungu katika tribinali?
9Akiwachunguza, ninyi mutapona?
Au munazani munaweza kumudanganya Mungu kama watu?
10Hakika yeye atawakaripia
kama mukionyesha upendeleo kwa siri.
11Utukufu wake hauwatishi?
Hamupatwi na hofu juu yake?
12Masemi yenu ni mezali za majivu,
maneno yenu ni ukuta wa udongo.
13Munyamaze, nami niseme.
Kitu kitakachonipata, kinipate.
14Niko tayari hata kuhatarisha maisha yangu.
15Mungu aniue akitaka; sina la kupoteza.
Hata hivyo nitautetea mwenendo wangu mbele yake.
16Kama nikiweza kwa hiyo nitakuwa nimeshinda,
maana mutu mwovu hawezi kwenda mbele yake.
17Musikilize kwa uangalifu maneno yangu,
maelezo yangu yatue katika masikio yenu.
18Maneno yangu nimeyatarisha jinsi inavyofaa.
Ninajua kwamba sina kosa.
19Nani atakayebishana nami?
Niko tayari kunyamaza na kufa.
20Mungu wangu, unijalie tu mambo haya mawili,
nami sitajificha mbali na wewe:
21kwanza uniondolee mukono wako unaonipiga,
na usiniogopeshe kwa kitisho chako.
22Uanze kusema maneno yako nami nikujibu.
Au mimi nianze, nawe unijibu.
23Makosa na zambi zangu ni ngapi?
Unijulishe kosa na zambi yangu.
24Mbona unageuza uso wako mbali nami?
Kwa nini unanitendea kama adui yako?
25Utatikisatikisa jani linalopeperushwa,
au kukimbiza nyasi iliyokauka?
26Wewe umetoa mashitaki makali juu yangu,
na kunibebesha zambi za ujana wangu.
27Unanifunga minyororo kwenye miguu,
unachunguza njia zangu zote,
umeichapa miguu yangu.
28Nami ninaisha kama muti uliooza,
kama nguo iliyokuliwa na nondo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.