Ezekieli 8 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Ibada za sanamu katika Yerusalema

1Katika mwaka wa sita, siku ya tano ya mwezi wa sita tangu tulipopelekwa katika uhamisho, nilikuwa nikiikaa ndani ya nyumba yangu pamoja na wazee wa Yuda. Basi, kwa rafla nikajazwa na uwezo wa Yawe.

2Nilipoangalia, nikaona kitu kilichofanana na mwanadamu. Sehemu yake ya chini, iliyoonekana kama ndio kiuno chake, ilikuwa kama moto. Toka kiuno chake kwenda juu alimetameta kama vile shaba.

5Kisha Mungu akaniambia: Wewe mwanadamu, angalia upande wa kaskazini. Nami nikaangalia upande wa kaskazini, na huko upande wa kaskazini wa mulango wa mazabahu, niliona ile sanamu iliyomuchukiza Mungu.

6Basi, Mungu akaniambia hivi: Wewe mwanadamu, unaona mambo wanayofanya, machukizo makubwa Waisraeli wanayofanya kusudi wapate kunifukuza kutoka katika hekalu langu? Tena utaona machukizo mengine makubwa zaidi.

7Kisha akanipeleka mpaka kwenye mulango wa kuingilia ndani ya uwanja. Nilipoangalia nikaona tundu juu ya ukuta.

8Naye akaniambia hivi: Wewe mwanadamu, toboa ukuta huu. Nami, nikatoboa, nikaona kulikuwa mulango.

9Tena akaniambia: Ingia ndani uangalie machukizo mabaya wanayofanya humo.

10Basi, nikaingia, nikaona vitu vya kuchukiza vimechorwa kuzunguka ukuta: kila aina ya nyama wanaotambaa, vidudu, na sanamu zote za miungu ya Waisraeli.

11Na mbele yao kulikuwa wazee makumi saba wa taifa la Waisraeli pamoja na Yazania mwana wa Safanu. Kila mumoja alikuwa na chetezo katika mukono, na moshi wa ubani ulipanda juu.

12Kisha Mungu akaniambia: Wewe mwanadamu, umeona mambo wazee wa Waisraeli wanayotenda kwa uficho, kila mutu katika chumba chake cha sanamu. Wanasema: Yawe hatuoni. Yawe ameiacha inchi.

13Tena akaniambia: Utaona tena machukizo makubwa zaidi wanayotenda.

14Kisha akanipeleka mpaka kwenye mulango wa upande wa kaskazini wa nyumba ya Yawe. Huko kulikuwa wanawake wameikaa wakimwombolezea mungu Tamuzi.

15Mungu akaniambia: Wewe mwanadamu, umeyaona hayo? Utaona tena machukizo mengine makubwa kuliko hayo.

16Kisha akanipeleka mpaka katika uwanja wa ndani wa nyumba ya Yawe. Huko kwenye mulango wa hekalu, kati ya baraza na mazabahu, kulikuwa wanaume yapata makumi mbili na watano, wakigeuzia mugongo wao upande wa hekalu, na nyuso zao zikielekea upande wa mashariki. Walikuwa wanaabudu jua wakielekea upande wa mashariki.

17Mungu akaniambia: Wewe mwanadamu, umeyaona mambo hayo? Hata hivyo, watu wa Yuda wanaona machukizo hayo kuwa ni kidogo. Wanajaza mateso makali katika inchi na kuzidi kunikasirikisha. Angalia jinsi wananichukiza!

18Kwa sababu ya mambo hayo watasikia uzito wa kasirani yangu. Sitamwacha hata mutu mumoja aponyoke wala sitamwonea huruma mutu yeyote. Hata wakinililia kwa sauti kubwa mimi sitawasikiliza.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help