Mezali 13 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Mutoto mwenye hekima anasikia maagizo ya baba yake, lakini mwenye kiburi hasikilizi maonyo.

2Mutu muzuri anapata uzuri kutokana na maneno yake, lakini mudanganyifu anaishi kwa kutesa kwa ukali.

3Anayechunga kinywa chake analinda maisha yake, mwenye midomo mirefu anajiletea maangamizi.

4Muvivu anatamani lakini hapati kitu chochote, wakati mwenye bidii anajaliwa kwa wingi.

5Mwenye haki anachukia uongo, lakini mwovu anatenda kwa kupatisha haya na mazarau.

6Haki inalinda wenye mwenendo sawa, lakini zambi inaangusha waovu.

7Kuna mutu anayejidai kuwa tajiri, kumbe hana kitu. Mwengine anajiona kuwa masikini wakati ana mali tele.

8Ukombozi wa uzima wa mutu ni mali yake, lakini masikini hana njia ya kujikomboa.

9Mwenye haki anaangaa kama vile taa inayowaka vizuri, lakini waovu ni kama taa inayozimika.

10Kiburi kinasababisha tu ugomvi, lakini kwa wanaokubali shauri jema kuna hekima.

11Mali ya harakaharaka inatoweka, lakini anayekusanya kidogokidogo ataiongeza.

12Tumaini la kungojangoja linaumiza moyo, lakini tazamio linalotimia ni musingi wa uzima.

13Anayezarau mashauri anajiletea maangamizi, lakini anayetii amri atapewa zawadi.

14Mafundisho ya wenye hekima ni chemichemi ya uzima; inamwezesha mutu kuepuka mitego ya kifo.

15Kuwa na akili kunaleta ukubali, lakini njia ya waovu ni ya taabu.

16Mwenye akili anatenda kila kitu kwa kufikiri, lakini mupumbafu anatembeza upumbafu wake.

17Mujumbe mubaya anawatumbukiza watu katika taabu, lakini mujumbe mwaminifu analeta amani.

18Umasikini na mazarau vinamupata yule asiyejali mafundisho, lakini mwenye kusikia maonyo anaheshimiwa.

19Ni jambo la kufurahisha unapopata kile unachotaka, kwa hiyo wapumbafu wanachukia kuepuka uovu.

20Anayeandamana na wenye hekima anapata hekima, lakini anayejiunga na wapumbafu atapata hasara.

21Wanaotenda zambi wanapatwa na hasara, lakini wenye haki wanafanikiwa.

22Mutu muzuri anawaachia wazao wake urizi, lakini mali ya mwenye zambi imelundikiwa wenye haki.

23Shamba la masikini linatoa mazao mengi, lakini linanyanganywa juu ya wale wanaopotosha haki.

24Asiyemwazibu mutoto wake hamupendi; lakini anayemupenda mwana wake atamwazibu kwa wakati.

25Mwenye haki yuko na chakula cha kumutoshelea, lakini tumbo la waovu linataabika kwa njaa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help