1Yawe anasema hivi:
Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Moabu, hata kwa mane,
sitageuza nia yangu.
Wamemukosea heshima marehemu mufalme wa Edomu
kwa kuichoma mifupa yake kwa moto
kwa kujitengenezea chokaa!
2Basi, nitashusha moto juu ya inchi ya Moabu,
na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za muji wa Kerioti.
Waaskari watakapolalamika kwa sauti zao na kupiga baragumu,
watu wa Moabu watakufa katika makelele hayo ya vita.
3Nitamwua mutawala wa Moabu,
pamoja na waongozi wote wa inchi hiyo.
–Ni Yawe anayesema hivyo.
Yuda4Yawe anasema hivi:
Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Yuda, hata kwa mane,
sitageuza nia yangu.
Wamezarau sheria zangu,
wala hawakufuata masharti yangu.
Wamepotoshwa na miungu ileile babu zao waliyoifuata.
5Basi, nitashusha moto juu ya inchi ya Yuda,
na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za Yerusalema.
Hukumu ya Mungu juu ya Israeli6Yawe anasema hivi:
Kwa sababu ya makosa matatu ya Waisraeli, hata kwa mane,
sitageuza nia yangu.
Wameuzisha watu wa haki kuwa watumwa
kwa maana hawakuweza kulipa madeni yao;
na kuwauzisha wakosefu
wanaoshindwa kulipa deni la muguu mumoja wa mapapa.
7Wanagandamiza wazaifu,
na kuwabagua wamasikini wasipate haki zao.
Mutoto na baba yake wanalala na binti mujakazi mumoja,
hivyo wanalichafua jina langu takatifu.
8Juu ya kila mazabahu,
watu wanalalia nguo walizozitwaa kwa masikini
kama rehani ya madeni yao;
na katika nyumba ya Mungu wao,
wanakunywa divai waliyotwaa kwa wenye kuwa na madeni yao.
9Hata hivyo, enyi watu wangu,
kwa ajili yenu, niliwaangamiza kabisa Waamori
ambao walikuwa wakubwa kama mierezi,
wenye nguvu kama miti ya mialo.
Niliwaangamiza, matawi na mizizi.
10Niliwatoa ninyi kutoka inchi ya Misri,
nikawaongoza kupitia katika jangwa miaka makumi ine,
mpaka mukaitwaa inchi ya Waamori kuwa yenu.
11Nilichagua manabii kati ya wana wenu,
na wengine kati ya vijana wenu kuwa wanaziri.
Enyi Waisraeli,
haya ninayosema si ya kweli?
–Ni ujumbe wa Yawe.–
12Ninyi muliwakunywesha wanaziri divai,
na kuwaamuru manabii wasitoe unabii.
13Sasa basi, nitawagandamizia chini,
kama gari lililojaa ngano.
14Hata wale wenye kuwa hodari kwa kukimbia mbio hawataweza kutoroka;
wenye nguvu wataishiwa nguvu zao,
na waaskari watashindwa kuyaokoa maisha yao.
15Wapiga upinde katika vita hawataweza kusimama na nguvu;
wenye kuwa hodari kwa kukimbia mbio hawataweza kujiokoa,
wala waaskari wapanda-farasi hawatayaokoa maisha yao.
16Siku hiyo, hata waaskari hodari sana
watakimbia mbio bila chochote.
–Ni ujumbe wa Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.