Ezra UTANGULIZI - Swahili Congo Revised Bible 2002
UTANGULIZIKitabu hiki kimepewa jina la mutu ambaye alikuwa mumoja kati ya viongozi wa Wayuda wakati waliporudi kutoka katika uhamisho. Kinaanza na tangazo lililotolewa na mufalme Kiro wa Persia kwa kuwaruhusu watu wa Israeli warudie kwao kujenga upya hekalu la Yerusalema (sura 1). Kisha tunapewa hesabu kubwa ya hao wakimbizi ambao walianza safari ya kurudi kwao (sura 2). Shuguli yao ya kwanza kule Yerusalema ilikuwa kupata ile mazabahu ya sadaka na kuanzisha tena ibada kwa Mungu (sura 3). Matayarisho hayo hata hivyo yalisababisha upinzani kutoka kwa waadui na kwa sababu hiyo kukakuwa barua mbalimbali kwa wakubwa wa Persia ambao walihakikisha kwamba ruhusa ilikuwa imekwisha kutolewa (sura 4-6). Sehemu ya pili ya kitabu inaeleza jinsi kuhani Ezra, akiwa ametumwa na mufalme Artasasta, alivyofufua na kutengeneza maisha ya dini kule Yerusalema (sura 7-10).