2 Watesalonika 3 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mutuombee

1Kwa mwisho wandugu, mutuombee, kusudi neno la Bwana lisambae upesi na kutukuzwa, kama vile inavyokuwa kwenu.

2Vilevile mumwombe Mungu kusudi atuopoe toka mikono ya watu wabaya na waovu. Kwa maana si watu wote wanaokubali kuamini Habari Njema.

3Lakini Bwana ni mwaminifu, atawaimarisha na kuwakinga na yule Mwovu.

4Bwana anatupatia tumaini kwa ajili yenu kwamba munafanya na mutaendelea kufanya yale tunayowaagiza.

5Bwana aongoze mafikiri yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.

Inafaa kutumika kazi

6Wandugu, tunawaagiza katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo kwamba mujitenge na wandugu wote wanaokuwa wavivu na wasiofuata mafundisho tuliyowapa.

7Munajua vizuri ninyi wenyewe namna munavyopaswa kuiga mufano wetu. Kwa maana sisi hatukukuwa wavivu wakati tulipoishi pamoja nanyi.

8Sisi hatukukula chakula cha mutu kwa bure, lakini tulitumika na kuchoka sana. Tulitumika muchana na usiku kusudi tusilemee hata mutu mumoja kati yenu.

9Tulifanya vile si kwa sababu hatukukuwa na haki ya kupokea musaada wenu, lakini kwa sababu tulitaka sisi wenyewe kuwa kwenu mufano wa kuiga.

10Kwa maana, wakati tulipokuwa kwenu, tulikuwa tunawaagiza hivi: “Mutu yeyote asiyetaka kutumika, na hapaswi kula vilevile.”

11Tunasema hivi kwa sababu tumepata habari kwamba wamoja kati yenu ni wavivu; hawatumiki, isipokuwa tu kujiingiza katika maneno ya wengine.

12Tunawaagiza watu wale na kuwaonya kwa jina la Bwana Yesu Kristo kwamba watumike katika utulivu kwa kujitoshelea wenyewe katika maisha yao.

13Lakini ninyi, wandugu, musichoke kutenda mema.

14Kama mutu hataki kushika maagizo tunayowatolea katika barua hii, mumwangalie vizuri mutu yule, musishirikiane naye, kusudi apate haya.

15Musimuhesabu kama vile adui, lakini mumwonye kama vile ndugu.

Baraka na salamu

16Bwana wa amani mwenyewe awape amani siku zote na kwa njia zote. Bwana akuwe pamoja nanyi wote.

17Hii ni salamu ninayoiandika kwa mukono wangu mimi Paulo mwenyewe. Hii ndiyo sahihi yangu katika kila barua yangu, na mwandiko wangu.

18Tunawatakia ninyi wote neema kutoka kwa Yesu Kristo.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help