2 Timoteo 3 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Maonyo ya siku za mwisho

1Ujue vizuri kwamba siku za mwisho zitakuwa nyakati za magumu.

2Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda feza, wenye kujisifu na wenye kiburi, wenye kukufuru, wasiotii wazazi wao, wasioshukuru na waovu.

3Hawatakuwa na upendo wala huruma. Watakuwa wenye kusingiziana, wasiojizuiza, wakali na wasiopenda mema.

4Watakuwa wenye kutoana, wenye kichwa kigumu, wenye majivuno na wenye kupenda tamaa ya vitu kuliko kumupenda Mungu.

5Kwa inje watajionyesha kama watu wenye kushikamana na ibada, lakini wanazarau uwezo wake. Ujiepushe na watu hao.

6Kwa maana kati yao kuna wamoja wanaojiingiza katika nyumba za watu na kuwashawishi wanawake wajinga wanaolemewa na mizigo ya zambi na kuvutwa na tamaa za namna nyingi.

7Wanawake wale wanataka kujifunza siku zote, lakini hawafikii kutambua ukweli.

8Watu wale wanapinga ukweli kama vile Yane na Yambure walivyopingana na Musa. Akili ya watu hao imepotoka, nayo imani yao imegeuka bure.

9Lakini hawataendelea mbali sana, kwa sababu upumbafu wao utaonekana wazi mbele ya watu wote, sawa ilivyokuwa kwa Yane na Yambure.

Maagizo ya mwisho

10Lakini wewe umefuata kabisa mufano wangu katika mafundisho yangu na mwenendo wangu, makusudi yangu, imani yangu, uvumilivu wangu, upendo wangu, ungojevu wangu,

11mateso na taabu yangu. Unajua mambo yote ambayo yalinitokea kule Antiokia, Ikonio na Listra. Mateso haya niliyavumilia, na Bwana akaniokoa katika yote.

12Nao wote wanaotaka kuishi maisha ya kumwabudu Mungu katika kuungana na Kristo Yesu, watateswa.

13Lakini watu waovu na wadanganyifu wataendelea katika maovu, wakipotosha watu wengine na kujipotosha wenyewe.

14Lakini wewe ushikamane na mambo yale uliyofundishwa na kuyaamini kabisa. Unajua ni nani aliyekufundisha.

15Tena, tangia utoto wako unajua Maandiko Matakatifu yanayoweza kukupatia hekima kusudi uokolewe kwa njia ya kumwamini Kristo Yesu.

16Maandiko yote Matakatifu yameandikwa kwa maongozi ya Mungu na yanafaa kwa kufundisha, kuonya, kuhakikisha na kuadibisha katika haki,

17kusudi mutu wa Mungu apate kukamilika na kuwa tayari kabisa kwa kutenda kila kazi njema.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help