1Yawe akamwambia Musa: Anza safari uondoke hapa, wewe na watu hao uliowatoa katika inchi ya Misri. Muende katika inchi niliyowapia Abrahamu, Isaka na Yakobo, nikisema: Nitawapa wazao wenu inchi hii. Ang. Mwa 12.7; 26.3; 28.13
2Nitamutuma malaika awaongoze. Nitawafukuza Wakanana, Waamori, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
3Muende katika inchi hiyo inayotiririka maziwa na asali. Lakini kwa sababu ninyi ni wenye vichwa vigumu sitakwenda pamoja nanyi, nisiwaangamize katika njia.
4Watu wakalia waliposikia habari hizi mbaya, wala hakuna aliyevaa mapambo yake.
5Walifanya hivyo maana Yawe alikuwa amemwambia Musa: Uwaambie Waisraeli: Ninyi ni watu wenye vichwa vigumu. Nikienda pamoja nanyi kwa muda mufupi tu, nitawaangamiza. Hivyo muvue mapambo yenu kusudi nijue namna ya kuwatendea.
6Basi, Waisraeli wakavua mapambo yao tangu walipoondoka kwenye mulima Horebu.
Hema la mukutano7Musa alikuwa na desturi ya kuchukua lile hema na kulisimika inje ya kambi. Hema hilo alilipa jina, hema la mukutano. Mutu yeyote aliyetaka shauri kwa Yawe alikwenda kwenye hema la mukutano inje ya kambi.
8Kila mara Musa alipotoka kwenda kwenye hema hilo, kila mutu alisimama kwenye mulango wa hema yake na kumwangalia Musa mpaka alipoingia ndani ya hilo hema.
9Wakati Musa alipoingia ndani ya hilo hema, munara wa wingu ulitua kwenye mulango wa hema, na Yawe akaongea naye.
10Watu wote walipouona ule munara wa wingu umesimama kwenye mulango wa hema, kila mumoja wao alisimama na kuabudu kwenye mulango wa hema lake.
11Hivi ndivyo Yawe alivyokuwa akiongea na Musa uso kwa uso, kama mutu na rafiki yake. Kisha Musa alirudi tena katika kambi. Naye kijana Yoshua mwana wa Nuni ambaye alikuwa mutumishi wake hakuondoka ndani ya hema.
Yawe anaahidi kuwa na watu wake12Musa akamwambia Yawe: Wewe unaniambia: Uwaongoze watu hawa, lakini haujanijulisha ni nani utakayemutuma anisaidie. Hata hivyo umesema kwamba unanijua kwa jina langu na vilevile kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako.
13Sasa basi, ninakusihi, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, unionyeshe sasa njia zako, kusudi nipate kukujua na kupata kukubaliwa mbele yako. Ninaomba ukumbuke vilevile kwamba taifa hili ni watu wako.
14Mungu akasema: Mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nawe na nitakupa raha.
15Musa akasema: Kama wewe peke yako hautakwenda pamoja nami, basi, usituondoe pahali hapa.
16Maana namna gani itajulikana kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako, mimi na watu wako kama usipokwenda pamoja nasi? Ukienda pamoja nasi itatufanya mimi na watu wako kuwa watu wa pekee kati ya watu wote katika dunia.
17Yawe akamwambia Musa: Kwa sababu umepata kukubaliwa mbele yangu, nami ninakujua kwa jina lako, jambo hilihili ulilolisema nitalifanya.
18Musa akasema: Ninakusihi unionyeshe utukufu wako.
19Yawe akamujibu: Nitapita mbele yako na kukuonyesha uzuri wangu wote nikilitangaza jina langu, Yawe. Mimi nitamuhurumia yule ninayependa kumuhurumia; nitamurehemu yule ninayependa kumurehemu. Ang. Rom 9.15
20Lakini hautaweza kuniona uso maana hakuna mwanadamu yeyote atakayeniona na kuishi.
21Kisha Yawe akamwambia Musa: Kuna pahali karibu nami ambapo utasimama juu ya jiwe.
22Utukufu wangu utakapokuwa unapita, nitakutia katika pango chini ya jiwe na kukufunika kwa mukono wangu, mpaka nitakapokuwa nimepita.
23Halafu nitaondoa mukono wangu nawe utaona mugongo wangu, lakini uso wangu hautauona.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.