Hesabu 34 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mipaka ya inchi

1Yawe akamwambia Musa:

2Uwaamuru Waisraeli ukisema: Mutakapoingia Kanana, inchi ambayo ninawapa ikuwe inchi yenu, mipaka ya eneo lenu lote itakuwa kama hivi.

3Upande wa kusini mupaka wenu utakuwa kutoka jangwa la Sini kupitia upande wa Edomu. Utaanzia mashariki upande wa kusini mwisho wa bahari ya Chumvi.

4Kisha utapinda kusini kuelekea mupando wa Akarabimu na kupitia Sini mpaka Kadesi-Barnea, upande wa kusini. Kutoka pale, mupaka utapinda kuelekea kaskazini-magaribi mpaka Hasari-Adari na kupita mpaka Azimoni.

5Kutoka Azimoni utapinda kuelekea kijito cha Misri kwenye mupaka wa Misri na kuishia bahari ya Mediteranea.

6Mupaka wenu wa upande wa magaribi utakuwa bahari ya Mediteranea.

7Mupaka wenu wa upande wa kaskazini utakuwa kama hivi: kutoka bahari ya Mediteranea, mpaka kwenye mulima Hori,

8na kutoka mulima Hori, mpaka kwenye njia inayokwenda Hamati, na kuendelea mpaka Sedadi,

9kupitia Zifuroni na kuishia Hazari-Enani. Huo utakuwa mupaka wenu wa kaskazini.

10Mupaka wenu wa upande wa mashariki mutauweka kutoka Hazari-Enani mpaka Sefamu.

11Kutoka Sefamu utaelekea kusini mpaka Ribla, upande wa mashariki wa Aini; kisha mupaka huo utakwenda chini mpaka kwenye muteremuko wa upande wa mashariki wa ziwa la Kinereti,

12halafu utateremuka kufuata muto Yordani mpaka bahari ya Chumvi hii ndiyo itakuwa inchi yako kama vile mupaka unavyokuwa.

13Basi, Musa akawaambia Waisraeli: Hii ndiyo inchi mutakayoirizi kwa kupiga kura, inchi ambayo Yawe ameagiza ipewe kwa makabila tisa na nusu. Ang. Yos 14.1-5

14Kabila la Rubeni na la Gadi, na nusu ya kabila la Manase yamepata urizi wao kulingana na ukoo zao.

15Makabila hayo mawili na nusu yamepata urizi wao ngambo ya muto Yordani upande wa mashariki, kuelekea Yeriko, jua linakotokea.

Viongozi watakaosimamia mugawanyo wa inchi

16Yawe akamwambia Musa:

17Kuhani Eleazari na Yoshua mwana wa Nuni ndio watakaowagawanyia watu inchi kuwa mali yao.

18Utatwaa vilevile kiongozi mumoja kutoka kila kabila kwa kusaidia katika ugawanyaji wa inchi.

19Haya ndiyo majina yao:

Kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune.

20Kabila la Simeoni, Semweli mwana wa Amihudi.

21Kabila la Benjamina, Elidadi mwana wa Kisiloni.

22Kabila la Dani, Buki mwana wa Yogli.

23Kabila la Manase mwana wa Yosefu, Hanieli mwana wa Efodi.

24Kabila la Efuraimu mwana wa Yosefu, Kemueli mwana wa Sifutani.

25Kabila la Zebuluni, Elisafani mwana wa Parnaki.

26Kabila la Isakari, Paltieli mwana wa Azani.

27Kabila la Aseri, Ahihudi mwana wa Selomi

28Kabila la Nafutali, Pedaheli mwana wa Amihudi.

29Hawa ndio watu ambao Yawe aliwaamuru wawagawanyie watu Waisraeli inchi ya Kanana kuwa mali yao.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help