1Akatengeneza mazabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto. Mazabahu hiyo ilikuwa ya muraba, metre mbili na sentimetre makumi mbili kwa metre mbili na sentimetre makumi mbili, na urefu kwenda juu metre moja na sentimetre makumi mbili.
2Katika kila pembe ya mazabahu hiyo akatengeneza upembe uliokuwa umeundwa kutokana na mazabahu yenyewe. Mazabahu hiyo yote akaipakaa shaba.
3Akatengeneza vilevile vyombo vyote kwa ajili ya mazabahu: vyungu, majembe, mabeseni, kanya na visahani vya kutwalia moto. Vyombo vyake vyote akavitengeneza kwa shaba.
4Akatengeneza wavu wa shaba, akautia chini ya ukingo wa mazabahu mpaka katikati ya mazabahu.
5Katika pembe ine akatengeneza pete ine za kubebea hiyo mazabahu.
6Akatengeneza miti ya mujohoro na kuipakaa shaba.
7Akaitia ile miti katika zile pete zilizokuwa kando ya mazabahu kwa kuibebea. Mazabahu hiyo iliyotengenezwa kwa mbao ilikuwa wazi ndani.
8Kisha akatengeneza birika la shaba na tako lake la shaba. Birika hilo lilitengenezwa kwa kutumia vioo vya shaba vya wanawake waliotumika kwenye mulango wa hema la mukutano. Upango wa hema la mukutano(Kut 27.9-19)
9Kisha akatengenezea hema upango. Mapazia ya upande wa kusini wa upango yalikuwa ya kitani safi iliyosokotwa na yenye urefu wa metre makumi ine na ine;
10nayo yalishikiliwa na nguzo makumi mbili za shaba zenye vikalio makumi mbili vya shaba. Lakini vifungio vya nguzo hizo na kamba zake vilikuwa vya feza.
11Upande wa kaskazini urefu wa pazia ulikuwa metre makumi ine na ine, na nguzo zake makumi mbili za shaba, lakini vifungio vya nguzo hizo na kamba zake vilikuwa vya feza.
12Upande wa magaribi ulikuwa na pazia yenye urefu wa metre makumi mbili na mbili, nguzo zake kumi na vikalio vyake kumi. Vifungio vya nguzo na kamba zake vilikuwa vya feza.
13Upande wa mashariki, kulikuwa mulango, uliokuwa na upana wa metre makumi mbili na mbili.
14Pazia la kila upande wa mulango lilikuwa na upana wa metre sita na nusu, pamoja na nguzo tatu na vikalio vyake vitatu.
15Upande mwingine vilevile ulikuwa na pazia yenye upana wa metre sita na nusu, pamoja na nguzo tatu na vikalio vyake vitatu.
16Mapazia yote kuzunguka upango yalikuwa ya kitani safi iliyosokotwa.
17Vikalio vyote vya nguzo vilikuwa vya shaba, lakini vifungio vya nguzo hizo na kamba zake vilikuwa vya feza. Vifungio vyake vilikuwa vya feza; vilevile nguzo zake zote zilishikamanishwa kwa fito za feza.
18Pazia la mulango wa upango lilitengenezwa kwa sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa, na kupambwa vizuri. Nalo lilikuwa na urefu wa metre tisa na urefu kwenda juu metre mbili, kulingana na mapazia ya upango.
19Vilevile nguzo zake zilikuwa ine na vikalio vine vya shaba. Vifungio vyake vilikuwa vya feza, hata nguzo zake na kamba zake vilikuwa vya feza.
20Misumari yote ya hema na ya upango kandokando ya hema vilikuwa vya shaba.
21Hii ndiyo hesabu ya vifaa vilivyotumika katika kujenga hema la kuchunga vile vibao vya agano. Hesabu hii ilitayarishwa na Walawi kwa amri ya Musa, chini ya uongozi wa Itamari mwana wa kuhani Haruni.
22Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huri, wa kabila la Yuda, alifanya kila kitu ambacho Yawe alimwamuru Musa.
23Alisaidiwa na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, fundi mukubwa wa kutia mapambo, kufanya michoro na kupamba kwa nyuzi za sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu na kitani safi iliyosokotwa.
24Zahabu yote waliyomutolea Yawe kwa ajili ya kujenga hema takatifu ilikuwa na uzito wa kilo mia nane makumi saba na saba na grama mia tatu kulingana na vipimo vya hema takatifu.
25Feza waliyochanga hao waliohesabiwa ilikuwa ya uzito wa kilo elfu tatu kumi na saba na grama mia saba makuni tano kulingana na vipimo vya hema takatifu.
26Kila mutu aliyehesabiwa tangu umri wa miaka makumi mbili na moja na zaidi alitoa muchango wake wa feza grama tano. Wanaume wote waliohesabiwa walikuwa elfu mia sita na tatu na mia tano na makuni tano. Ang. Mat 17.24
27Kilo elfu tatu za feza zilitumika kwa kutengeneza vile vikalio mia moja vya hema takatifu na lile pazia, ni kusema kilo makumi tatu kwa kila kikalio.
28Zile kilo kumi na saba na grama makumi saba na tano zilizobakia, zilitumika kwa kutengeneza vifungio vya nguzo na kuvipakaa vichwa vya nguzo na kutengeneza kamba.
29Jumla ya muchango wa shaba Waisraeli waliomutolea Yawe ilikuwa na uzito wa kilo elfu mbili mia moja makumi mbili na ine.
30Bezaleli akatumia shaba hiyo kwa kutengeneza vikalio vya mulango wa hema la mukutano, mazabahu ya shaba pamoja na wavu wake wa shaba, vyombo vyote vya mazabahu,
31vikalio vya upango uliolizunguka hema la mukutano na vya mulango wa upango na misumari yote ya hema takatifu na ya upango.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.