1Neno hili ni la kweli; kama mutu anatamani kazi ya musimamizi wa kanisa anatamani kazi nzuri.
2Basi musimamizi wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno lolote. Sherti akuwe na muke mumoja tu, akuwe mukadirifu, mwenye akili, akuwe mwema na mwenye kupenda kukaribisha wageni na mwenye kujua kufundisha.
3Hapaswi kuwa mulevi wala mupiganaji, lakini akuwe mupole mwenye kupenda amani, wala asikuwe mutu wa kupenda feza.
4Anapaswa kuwa mutu mwenye kuongoza jamaa yake vizuri na kuadibisha watoto wake kusudi wakuwe wenye utii na wenye heshima kabisa.
5Kwa maana mutu anayeshindwa na kuongoza jamaa yake mwenyewe, namna gani ataweza kuchunga kanisa la Mungu?
6Yeye hapaswi kuwa mwamini mupya; kusudi asitawaliwe na kiburi na kuhukumiwa kama vile Shetani alivyokuwa.
7Vilevile inafaa akuwe mutu mwenye kushuhudiwa vizuri na watu wa inje ya kanisa, kusudi asizarauliwe na kunaswa katika mutego wa Shetani.
Mapaswa ya wasaidizi wa kanisa8Vilevile wasaidizi wanaotumika katika kanisa wanapaswa kuwa watu wenye heshima. Hawapaswi kuwa wenye nia mbili katika masemi yao wala wenye kunywa pombe kwa uwingi wala wenye kutafuta mali kwa njia isiyokuwa sawa;
9wanapaswa kushikamana kwa zamiri safi na ukweli wa imani uliofunuliwa.
10Inafaa wapimwe kwanza, na kisha kama hawakuonekana na kosa, wataweza kutumika kama wasaidizi wa kanisa.
11Wanawake wao wanapaswa kuwa na adabu vilevile, wasikuwe wasingiziaji wa uongo, lakini wakuwe wakadirifu na waaminifu katika mambo yote.
12Inafaa wasaidizi wa kanisa wakuwe kila mutu na muke mumoja tu, na wanapaswa kuwa watu wenye kuongoza vizuri watoto wao pamoja na jamaa zao.
13Wasaidizi wanaotumika vizuri kazi zao, wanajiheshimisha, na wanaweza kutangaza kwa uhodari habari za imani tunayokuwa nayo katika kuungana na Kristo Yesu.
Jambo kubwa la siri14Ninakuandikia barua hii, ijapokuwa ninatumaini kuja kukuona kisha muda kidogo.
15Lakini, kama nikikawia kufika, utaweza hivi kujua mwenendo unaopaswa kuwa nao katika nyumba ya Mungu, maana yake katika jamaa ya Mungu Mwenye Uzima. Yeye ndiye anayekuwa nguzo na musingi wa kweli.
16Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa:
Yeye alitokea kwa mufano wa mutu,
alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki.
Alionekana na wamalaika.
Alitangazwa katikati ya mataifa.
Aliaminiwa popote katika dunia.
Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.