Marko 9 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Na Yesu akaongeza kusema: “Kweli ninawaambia: wamoja kati ya watu wanaokuwa hapa hawatakufa mbele hawajaona Ufalme wa Mungu ukikuja kwa uwezo.”

Yesu anageuzwa sura(Mat 17.1-13; Lk 9.28-36)

2Nyuma ya siku sita, Yesu aliwatwaa Petro, Yakobo na Yoane, na kuwapeleka kwenye mulima murefu pekee yao. Na kule sura ya Yesu ikageuka mbele yao.

3Nguo zake zikageuka nyeupe sana na kumetameta, wala katika dunia hakuna fundi wa kufua anayeweza kuziangarisha kama vile.

4Halafu wale wanafunzi watatu wakawaona Elia na Musa wakisemezana na Yesu.

5Basi Petro akamwambia Yesu: “Mwalimu, ni vizuri kuona kwamba sisi tuko hapa. Tujenge vibanda vitatu, kimoja chako, kimoja cha Musa na kingine cha Elia.”

6Petro hakujua la kusema kwa maana yeye na wenzake waliogopa.

7Halafu wingu likatokea na kuwafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa. Mumusikilize!”

8Mara moja wanafunzi waliangalia pande zao zote, hawakumwona mutu mwingine pamoja nao, isipokuwa Yesu peke yake.

9Walipokuwa wakishuka toka kwa mulima, Yesu akawaamuru: “Musimwelezee mutu mambo muliyoona mpaka Mwana wa Mutu atakapofufuka.”

10Wao walitii agizo hilo, lakini wakaanza kuulizana: “Maana ya kufufuka huku ni gani?”

11Kisha wakamwuliza Yesu: “Kwa nini walimu wa Sheria wanasema kama sherti Elia arudi kwanza?”

12Yesu akawajibu: “Hakika Elia anapaswa kurudi kwanza kutengeneza mambo yote. Lakini sababu gani Maandiko Matakatifu yanasema vilevile kwamba Mwana wa Mutu atateswa sana na kuzarauliwa?

13Lakini ninawaambia kama Elia amekwisha kurudi, na watu walimutendea yote waliyotaka, kama Maandiko yanavyosema juu yake.”

Yesu anaponyesha mutoto mwenye pepo wa bubu(Mat 17.14-21; Lk 9.37-43a)

14Waliporudi kwenye wanafunzi wengine, wakaona kundi la watu wengi wakiwazunguka na walimu wa Sheria wakibishana nao.

15Mara moja, watu walipomwona Yesu, wakashangaa sana, wakakimbia kwenda kumusalimia.

16Yesu akawauliza wanafunzi wake: “Munabishana nao juu ya nini?”

17Na mutu mumoja kati ya kundi akamujibu: “Mwalimu, nimemuleta mwana wangu kwako, kwa maana yuko na pepo wa bubu.

18Kila wakati yule pepo anapomukamata, anamwangusha chini, na mutoto anatoka pofu na kusaga meno, nao mwili wake unakauka. Niliomba wanafunzi wako wamufukuze yule pepo, lakini hawakuweza.”

19Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu! Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Muniletee mutoto hapa.”

20Halafu wakamuleta mutoto kwake. Na mara moja yule pepo alipomwona Yesu, akamutikisatikisa yule mutoto kwa nguvu hata akaanguka chini, akagaagaa chini na kutoka pofu.

21Yesu akamwuliza baba ya mutoto: “Amekuwa na hali hii tangu wakati gani?”

Baba yake akamujibu: “Ni tangu utoto wake.

22Na mara nyingi huyu pepo anamutupa katika moto na ndani ya maji, kusudi amwue. Lakini kama unaweza kufanya kitu, utuhurumie na kutusaidia.”

23Yesu akamwambia: “Kwa sababu gani unasema: ‘Kama unaweza?’ Yote yanawezekana kwa yule anayeamini.”

24Mara moja baba ya mutoto akasema kwa nguvu: “Ninaamini! Lakini unisaidie kwa ajili ya kukosa kuamini!”

25Wakati Yesu alipoona watu wengi wanazidi kukusanyika mbiombio, akamukaripia yule pepo na kumwambia: “Wewe pepo wa bubu na wa kiziwi, ninakuamuru utoke ndani ya mutu huyu wala usimurudilie tena!”

26Yule pepo akalalamika, akamutikisatikisa mutoto kwa nguvu na kutoka ndani yake. Mutoto akaonekana sawa amekufa, hata watu wengi wakaanza kusema kwamba amekufa.

27Lakini Yesu akamushika mukono, akamwinua, naye akasimama.

28Yesu alipokwisha kuingia ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamwuliza hivi wakiwa peke yao: “Sababu gani sisi hatukuweza kumufukuza yule pepo?”

29Yesu akawajibu: “Pepo wa namna hii wanaweza kufukuzwa tu kwa njia ya maombi.”

Yesu anajulisha tena habari za kufa na kufufuka kwake(Mat 17.22-23; Lk 9.43b-45)

30Yesu na wanafunzi wake wakatoka kule na kupitia jimbo la Galilaya. Yesu hakutaka mutu ajue pahali walipokuwa,

31kwa sababu alikuwa akiwafundisha wanafunzi wake, akiwaambia: “Mwana wa Mutu atatolewa katika mikono ya watu, nao watamwua, na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.”

32Lakini wanafunzi hawakufahamu maana ya mafundisho hayo. Wakaogopa kumwuliza neno.

Ni nani anayekuwa mukubwa katika Ufalme wa Mungu?(Mat 18.1-5; Lk 9.46-48)

33Walipofika Kapernaumu na kuingia ndani ya nyumba, Yesu akawauliza wanafunzi wake: “Mulibishana juu ya nini katika njia?”

34Lakini wakanyamaza, kwa sababu walikuwa wakibishana katika njia kwamba nani anayekuwa mukubwa kati yao.

35Basi Yesu akaikaa, akawaita wanafunzi wake kumi na wawili na kuwaambia: “Mutu anayetaka kuwa wa kwanza anapaswa kujiweka wa mwisho kuliko wote na kuwa mutumishi wa wote.”

36Kisha akatwaa mutoto mudogo, akamuweka mbele yao na kumukumbatia. Naye akawaambia:

37“Anayemupokea mutoto mudogo kama huyu kwa ajili yangu, ananipokea mimi. Na anayenipokea, hanipokei mimi tu, lakini anamupokea vilevile yule aliyenituma.”

Asiyekuwa adui yetu ni wa kundi letu(Lk 9.49-50)

38Yoane akamwambia Yesu: “Mwalimu, tulimwona mutu mumoja akifukuza pepo kwa jina lako, nasi tulimukataza kwa sababu yeye si wa kikundi chetu.”

39Lakini Yesu akajibu: “Musimukataze, kwa maana hakuna mutu anayefanya miujiza kwa jina langu, ambaye anaweza nyuma kidogo kusema vibaya juu yangu.

40Ni vile kwa maana asiyekuwa adui yetu, ni wa upande wetu.

41Na yeyote atakayewapa kikombe cha maji kwa ajili yangu, kwa sababu ninyi ni watu wa Kristo, kweli ninawaambia, mutu yule hatakosa kupewa zawadi yake.”

Hatari ya zambi(Mat 18.6-9; Lk 17.1-2)

42“Yeyote atakayeangusha mumoja wa hawa wadogo wanaoniamini, ingelikuwa heri afungiwe jiwe kubwa la kusagia katika shingo na kutupwa ndani ya bahari.

43Kama mukono wako ukikukosesha, uukate! Ni heri kwako kuingia kwenye uzima wa kweli ukiwa na mukono mumoja, kuliko kuwa na mikono miwili na kwenda katika jehenamu ndani ya moto usiozimika.

45Kama muguu wako ukikukosesha, uukate. Ni heri kwako kuingia kwenye uzima wa kweli ukiwa na muguu mumoja, kuliko kuwa na miguu miwili na kutupwa katika moto wa jehenamu.

47Kama jicho lako likikukosesha, uliongoe. Ni heri kwako kuingia katika Ufalme wa Mungu ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili na kutupwa katika jehenamu.

48Mule muna vidudu visivyokufa, na moto usiozimika.

49“Kwa maana kila mutu atatiwa chumvi kwa moto.

50“Chumvi ni kitu kizuri. Lakini chumvi ikipoteza onjo lake, itatiwa nini kusudi ipate tena kukolea?

“Muwe na chumvi ndani yenu na muishi pamoja kwa amani.”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help