1Halafu Hana aliomba na kusema:
Ninamushangilia Yawe ndani ya moyo wangu.
Ninamutukuza Yawe anayekuwa nguvu yangu.
Ninawachekelea waadui zangu;
maana ninaufurahia wokovu wako.
2Hakuna anayekuwa mutakatifu kama Yawe;
hakuna yeyote anayekuwa kama yeye;
hakuna anayekuwa jiwe la kufichamia kama Mungu wetu.
3Muache kujisifu,
muache kusema kwa kiburi.
Maana anayejua ni Yawe.
Yeye anayapima matendo yote.
4Pinde za wenye nguvu, zimevunjika.
Lakini wazaifu wanaendelea kupata nguvu.
5Wale ambao zamani walikuwa na chakula tele,
sasa wanafanya kazi wapate chakula.
Lakini waliokuwa na njaa,
sasa hawana njaa tena.
Mwanamuke tasa, amezaa watoto saba.
Lakini mama mwenye watoto wengi,
sasa ameachwa bila mutoto.
6Yawe anaua na kufufua,
yeye anawashusha katika kuzimu
naye anawarudisha tena.
7Yawe anawafanya wamoja wakuwe wamasikini,
na wengine wakuwe watajiri.
Anawashusha wamoja,
na kuwainua wengine.
8Anawainua wazaifu toka katika mavumbi,
anawanyanyua wakosefu toka katika majivu,
na kuwaikalisha pamoja na wakubwa,
na kuwarizisha viti vya heshima.
Maana, minara ya dunia ni ya Yawe;
yeye ameisimika dunia juu ya minara yake.
9Anayalinda maisha ya waaminifu wake,
lakini anaangamiza maisha ya waovu katika giza.
Maana, mwanadamu hapati ushindi kwa nguvu zake.
10Waadui za Yawe watavunjwa vipandevipande;
atanguruma juu yao kama radi mbinguni.
Yawe ataihukumu dunia yote,
atamupa nguvu mufalme wake,
na atautukuza uwezo wa muchaguliwa wake.
11Kisha, Elekana akarudi kwake Rama. Lakini mutoto Samweli akabaki Shilo kwa kumutumikia Yawe chini ya uongozi wa kuhani Eli.
Wana wa Eli12Wana wa Eli walikuwa wapotovu sana. Hawakumujali Yawe
13wala juu ya vitu ambavyo watu walipaswa kuwapa makuhani. Kila mara mutu alipokuwa anatolea sadaka yake, mutumishi wa kuhani alikuja na kanya yenye meno matatu; na wakati nyama ikiwa bado inatokota,
14huyo mutumishi alichomeka kanya ile ndani ya chungu, nyama yoyote inayonyanyuliwa na kanya ile ilikuwa mali ya kuhani. Waisraeli wote waliokwenda Shilo kutolea sadaka zao walitendewa hivyo.
15Zaidi ya hayo, hata mbele mafuta hayajateketezwa kwa moto, mutumishi wa kuhani anakuja na kumwambia yule mutu anayetolea sadaka: “Mumutoshee kuhani nyama ya kuchoma maana yeye hatapokea nyama yako iliyotokoteshwa, lakini inayokuwa mbichi.”
16Na kama mutu huyo akimujibu: “Ngojea kwanza niteketeze mafuta halafu utakamata kadiri unataka”, hapo huyo mutumishi wa kuhani anamujibu: “Hapana, unapaswa kunipatia sasa hivi. Kama sivyo, nitaitwaa kwa nguvu.”
17Zambi hii ya vijana hao wa Eli ilikuwa kubwa sana mbele ya Yawe. Maana, vijana hao walizarau matoleo ya Yawe.
Samweli kule Shilo18Wakati ule, kijana Samweli aliendelea kumutumikia Yawe, akiwa amevaa kizibao cha kitani.
19Kila mwaka mama yake alimufumia nguo ndogo, na kumupelekea alipokuwa akienda na mume wake kutolea sadaka ya kila mwaka.
20Eli aliwabariki Elekana na muke wake, akisema: “Yawe akupe wewe Elekana watoto wengine kwa mwanamuke huyu kusudi wakamate nafasi ya yule uliyemupa Yawe.” Kisha wao walirudi kwao.
21Yawe alimusikilia Hana huruma naye akajaliwa kupata watoto wa kiume watatu na wabinti wawili. Mutoto Samweli akaendelea kukomaa mbele ya Yawe.
Eli na wana wake22Wakati ule, Eli alikuwa muzee sana. Aliposikia yote ambayo wana wake walikuwa wanawatendea Waisraeli, jinsi walivyokuwa wanalala na wanawake waliokuwa wanatumika kwenye mulango wa Hema ya Kusanyiko,
23aliwauliza: “Kwa nini munafanya mambo haya? Ninasikia kutoka kwa watu wote juu ya maovu munayoyafanya.
24Musifanye hivyo wana wangu, kwa sababu mambo hayo ninayoyasikia kutoka kwa watu wa Yawe ni mabaya.
25Mutu akimukosea mwenzake, anaweza kuombewa kwa Mungu, kusudi Mungu amusamehe. Lakini mutu akimukosea Yawe nani anayeweza kumwombea musamaha?” Lakini watoto hao hawakumusikiliza baba yao, maana Yawe alikwisha kata shauri la kuwaua.
26Mutoto Samweli aliendelea kukomaa, akazidi kupendwa na Yawe na watu.
Unabii juu ya jamaa ya Eli27Siku moja, mutu wa Yawe alimwendea Eli, akamwambia: “Yawe amesema hivi: Nilijijulisha kwa jamaa ya Haruni, babu yako, walipokuwa watumwa wa mufalme wa Misri katika inchi ya Misri.
28Kati ya makabila yote ya Israeli nilimuchagua Haruni na jamaa yake kuwa makuhani wangu, wanitumikie kwenye mazabahu, wafukize ubani na kuvaa kizibao mbele yangu. Nikaipatia jamaa ya babu yako sadaka zangu ambazo Waisraeli walinitolea kwa moto.
29Kwa nini basi, umezionea wivu matoleo na sadaka nilizowaamuru watu waniletee, nawe ukawaheshimu watoto wako kuliko mimi kwa kujinenepesha wenyewe kwa kula sehemu nzuri za sadaka ambazo watu wangu wa Israeli wananitolea?
30Kwa hiyo, ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli, ni huu: Niliahidi kwamba jamaa yako na jamaa ya babu yako mutakuja mbele yangu kunitumikia milele; lakini sasa jambo hilo likuwe mbali nami. Nitawaheshimu wale wanaoniheshimu, na wale wanaonizarau, nitawazarau. –Ni ujumbe wa Yawe.–
31Angalia siku zinakuja ambapo nitawaua vijana wote wanaume katika jamaa yako na katika ukoo wako, hata hakutakuwa mwanaume yeyote atakayeishi na kuwa muzee.
32Utakuwa na wasiwasi na utawaonea wenzako wivu kwa zile baraka zote ambazo nitawapa watu wengine wa Israeli, lakini hakuna mutu katika jamaa yako atakayeishi na kuwa muzee.
33Mutu wako ambaye sitamwangamiza kutoka mazabahu yangu atakuwa ameponyoka kusudi nipofushe macho yake, naye atakufa moyo na wazao wake watauawa kifo kibaya.
34Na litakalowapata watoto wako wawili, Hofuni na Finehasi, ni hili: Wote wawili watakufa siku moja. Hiki kitakuwa ni kitambulisho kwako.
35Kisha, nitajiinulia kuhani mwingine mwaminifu atakayefanya kulingana na yale yanayokuwa ndani ya moyo na akili yangu. Nitamujengea ukoo imara, naye atatumika siku zote mbele ya mufalme wangu muchaguliwa.
36Yeyote atakayebakia katika jamaa yako atamwendea kuhani yule na kumwomba kikoroti cha feza au mukate, na kumwambia: Ninakuomba uniweke kwenye nafasi moja ya kuhani kusudi niweze kupata tu kipande cha mukate.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.