Marko 11 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Yesu anaingia Yerusalema(Mat 21.1-11; Lk 19.28-40; Yn 12.12-19)

1Yesu na wanafunzi wake wakakaribia kufika Yerusalema, upande wa kijiji cha Betefage na cha Betania, karibu na mulima wa Mizeituni. Yesu akawatuma wawili katika wanafunzi wake,

2akiwaambia: “Mwende katika kijiji kinachokuwa mbele yenu. Wakati mutakapofika kule, mutaona mwana-punda amefungwa, na hakuna mutu aliyekwisha kupanda juu yake. Mumufungue na kumuleta hapa.

3Na kama mutu akiwauliza: ‘Kwa sababu gani munafanya hivi? Mumwambie kwamba Bwana yuko na lazima ya kumutumia, atamurudisha hapa nyuma kidogo.’ ”

4Basi wakaenda, wakaona mwana-punda amefungwa inje, karibu na mulango wa nyumba pembeni ya barabara. Walipokuwa wakimufungua,

5watu waliokuwa pale wakawauliza: “Munafanya nini? Kwa nini munamufungua mwana-punda huyu?”

6Wakawajibu sawa vile Yesu alivyowaambia, nao watu wale wakawaruhusu kwenda.

7Wakamuletea Yesu yule mwana-punda na kutandika nguo zao juu yake. Kisha Yesu akaikaa juu yake.

8Watu wengi wakatandika nguo zao katika njia na wengine wakatandika matawi waliyokata katika mashamba.

9Watu waliotangulia mbele ya Yesu na wale waliofuata nyuma yake wakaanza kulalamika kwa sauti kubwa, wakisema: “Mungu asifiwe! Abarikiwe huyu anayekuja kwa jina la Bwana!

10Ubarikiwe ufalme unaokuja, ndio ufalme wa babu yetu Daudi! Mungu asifiwe juu mbinguni!”

11Yesu akafika Yerusalema na kuingia ndani ya hekalu. Alipokwisha kuangalia vitu vyote pande zote, akaondoka na kwenda Betania pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili, kwa sababu ilikuwa imekwisha kuwa magaribi.

Yesu analaani muti was matunda ya tini(Mat 21.18-19)

12Kesho yake, walipotoka Betania, Yesu akasikia njaa.

13Akaona kwa mbali muti wa tini wenye majani mengi. Basi akaenda kuangalia kama atapata matunda juu ya muti ule. Lakini alipofika karibu nao, hakuona kitu juu yake isipokuwa majani matupu, kwa sababu haikukuwa wakati wake wa kutoa matunda.

14Halafu Yesu akalaani muti ule, akisema: “Tangia sasa hata milele, mutu asipate tena tunda tokea juu yako.”

Nao wanafunzi wake wakasikia maneno hayo aliyosema.

Yesu anafukuza wachuuzi katika hekalu(Mat 21.12-17; Lk 19.45-48; Yn 2.13-22)

15Kisha wakafika Yerusalema. Yesu alipoingia ndani ya hekalu, akaanza kufukuza watu waliokuwa wakiuzishia na kununulia vitu vyao ndani ya hekalu. Akapindua meza za wale waliobadilisha feza na viti vya wachuuzi wa njiwa.

16Vilevile akawakataza watu kukatiliza na mizigo yao katika kiwanja cha hekalu.

17Kisha akawafundisha maneno haya: “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya maombi kwa mataifa yote.’ Lakini ninyi mumeigeuza kuwa nafasi ya kukutania ya wanyanganyi!”

18Wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria walipopata habari hii, wakatafuta njia ya kumwua Yesu. Lakini walimwogopa, kwa sababu kundi lote la watu walishangaa na mafundisho yake.

19Ilipokuwa magaribi, Yesu na wanafunzi wake wakatoka katika muji ule.

Mafundisho kutoka muti wa tini uliolaaniwa(Mat 21.20-22)

20Kesho yake asubui, walipokuwa wakipita, wakaona ule muti wa tini, nao ulikuwa umekauka wote, hata mizizi yake.

21Petro akakumbuka mambo yaliyotokea mbele, akamwambia Yesu: “Mwalimu, angalia, ule muti wa tini ulioulaani umekauka.”

22Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Mumwamini Mungu.

23Kweli ninawaambia: ‘Mutu anaweza kuuambia mulima huu kwamba uondoke hapa na kujitupa katika bahari.’ Na ikiwa anasema maneno yale bila shaka katika moyo wake, lakini akiamini kama jambo lile litafanyika, hakika litafanyika kwake.

24Ni kwa hiyo ninawaambia kwamba munapoomba kwa ajili ya hitaji la kitu fulani, mwamini kama mumekwisha kukipokea, na kwa njia hiyo mutakipewa.

25Na munaposimama kwa kuomba, mukiwa na neno na mutu mwingine, mumusamehe, kusudi Baba yenu anayekuwa mbinguni, awasamehe vilevile makosa yenu.”

Mamlaka ya Yesu yanatoka wapi?(Mat 21.23-27; Lk 20.1-8)

27Yesu na wanafunzi wake wakafika tena Yerusalema. Yesu alipokuwa akitembea katika hekalu, wakubwa wa makuhani, walimu wa Sheria pamoja na wasimamizi wa watu, wakamufikia.

28Wakamwuliza: “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Na ni nani aliyekupa mamlaka haya?”

29Yesu akawajibu: “Nitawauliza ulizo moja tu. Kama mukinijibu, mimi vilevile nitawaambia ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.

30Yoane alipata mamlaka ya kubatiza kutoka kwa nani? Kwa Mungu au kwa watu? Munijibu.”

31Nao wakaanza kupiga mafikiri pamoja na kusema: “Kama tukijibu kwamba mamlaka yake yalitoka kwa Mungu, atatuuliza: ‘Kwa sababu gani hamukumwamini?’

32Vilevile hatuwezi kusema kama yalitoka kwa watu…” (Waliogopa kundi la watu kwa maana wote walisadiki kama Yoane alikuwa nabii wa kweli).

33Basi wakamujibu Yesu: “Hatujui.”

Naye akawaambia: “Nami vilevile sitawaambia ninyi ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help