1 Wafalme UTANGULIZI - Swahili Congo Revised Bible 2002
UTANGULIZIKitabu hiki ni maendeleo ya pale kitabu cha 2 Samweli kilipokwisha. Kinaanza na kueleza mambo ya mwisho ya Daudi na kukamata madaraka ya ufalme kwa upande wa Solomono. Kisha tunaelezwa mambo mbalimbali ya utawala wa Solomono, kilele cha habari hizo kikiwa ujenzi na kutakaswa kwa hekalu. Kisha tunaelezwa jinsi utawala ule mukubwa wa Daudi ulivyogawanyika na kuwa sehemu mbili zilizotengana: ufalme wa kaskazini, ni kusema Israeli, na ufalme wa kusini, ni kusema Yuda.Vitabu hivyo vya Wafalme vinatupatia mambo mbalimbali ya wafalme wa Israeli vilevile na mambo mengine. Lakini mambo hayo hayatolewi tu kama historia. Vitabu vinaonyesha namna ilivyokuwa ya lazima kabisa kwa wafalme kuwa waaminifu kwa Mungu. Manabii mbalimbali waliwakumbusha wafalme juu ya jambo hilo. Nabii mumoja mwenye sifa aliyekuwa na mapaswa hayo ni Elia (sura 17.1–19.21).Kitabu hiki kinaweza kugawanyika katika sehemu mbili kubwa:Sura 1-11: Utawala wa Solomono.Sura 12-22: Historia za tawala za Yuda na Israeli karne ya kwanza nyuma ya kutengana mpaka wakati wa mufalme Ahazi.