1Watu wamoja walishuka toka Yudea kwenda Antiokia, nao wakaanza kuwafundisha wandugu waamini kwamba hawawezi kuokoka ikiwa hawatahiriwi sawa vile inavyoagizwa katika Sheria ya Musa.
2Basi Paulo na Barnaba wakapingana na kubishana nao vikali sana juu ya jambo hili. Na kwa hiyo wandugu waamini wakaagiza Paulo na Barnaba pamoja na watu wengine kati yao waende Yerusalema kusemezana na mitume na wazee wa kanisa la kule juu ya maneno yale.
3Kanisa liliwapatia vitu walivyohitaji kwa ajili ya safari ile, nao wakapita katika inchi ya Foinikia na katika Samaria. Na kule wakaeleza namna watu wa mataifa mengine walivyomugeukia Mungu. Habari hii ikafurahisha sana wandugu waamini wote.
4Walipofika Yerusalema, wakakaribishwa na kanisa pamoja na mitume na wazee, nao wakawaelezea mambo yote Mungu aliyofanya kwa njia yao.
5Lakini wanafunzi wamoja waliokuwa katika chama cha Wafarisayo wakasimama na kusema: “Sherti watu wa mataifa mengine walioamini watahiriwe na kuagizwa wafuate Sheria ya Musa.”
6Halafu mitume na wazee wa kanisa wakakusanyika kusudi wachunguze neno hili.
7Mabishano yalipoendelea, Petro akasimama na kusema: “Wandugu zangu, munajua kwamba Mungu alinichagua pale zamani kati yenu kusudi nihubiri Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine wapate kuisikia na kuamini.
8Naye Mungu anayejua mafikiri ya mutu, alihakikisha kwamba amewakubali watu wa mataifa mengine kwa njia ya kuwapatia Roho Mutakatifu sawa vile alivyotupatia sisi.
9Yeye hakufanya ubaguzi kati yetu na wao; ametakasa mioyo yao kwa sababu walimwamini.
10Basi sasa, kwa nini munataka kumupima Mungu kwa kuwabebesha muzigo ambao wala babu zetu, wala sisi wenyewe hatukuweza kuubeba?
11Haipaswi kuwa vile, kwa maana sisi na wao vilevile tunaamini kwamba sisi wote tunaokolewa kwa neema ya Bwana Yesu.”
12Basi mukutano wote ukabaki kimya ukisikiliza maelezo ya Barnaba na Paulo juu ya vitambulisho na maajabu yote Mungu aliyofanya kwa njia yao katikati ya watu wa mataifa mengine.
13Nao walipomaliza kusema, Yakobo akajibu, akisema: “Wandugu zangu, munisikilize!
14Simoni anatoka kutuelezea namna Mungu alivyowashugulikia watu wa mataifa mengine pale mbele kusudi ajichagulie wamoja kati yao kuwa watu wake wa pekee.
15Na jambo hilo linapatana na maneno haya ya manabii yaliyoandikwa katika Maandiko Matakatifu:
16‘Nyuma ya mambo haya nitarudi,
nitaimarisha tena ufalme wa Daudi,
nitausimamisha tena
sawa wanavyojenga tena
nyumba iliyoanguka,
17kusudi watu wote wengine wamugeukie Bwana,
watu wa mataifa yote wapate kuwa watu wangu wa pekee.
18Ni vile Bwana anavyosema, yeye aliyejulisha mambo haya tangu zamani za kale.’ ”
19Yakobo akaendelea kusema: “Ni kwa sababu hii, mimi ninaona kwamba haifai tuwasumbue watu wa mataifa mengine wanaomugeukia Mungu.
20Lakini inafaa tuwaandikie kwa kuwaambia kwamba wajitenge na vitu vilivyochafuliwa kwa kutambikia sanamu, waepuke uasherati na wasikule nyamafu wala damu.
21Kwa maana tangu zamani Sheria ya Musa inasomwa kila siku ya Sabato katika nyumba za kuabudia na kuhubiriwa katika kila muji.”
Barua iliyotumwa kwa wanafunzi wa mataifa22Halafu mitume na wazee wakakata shauri pamoja na kanisa lote la Yerusalema kwamba wachague watu wamoja kati yao na kuwatuma kwenda Antiokia pamoja na Paulo na Barnaba. Wakachagua Yuda aliyeitwa vilevile Barisaba, pamoja na Sila. Watu hawa wawili walihesabiwa na wandugu waamini kuwa wenye heshima sana.
23Nao wakawatuma na barua iliyoandikwa hivi:
“Sisi mitume na wazee wa kanisa na wandugu zenu, tunawasalimu ninyi wandugu zetu waamini wa mataifa mengine munaokuwa katika muji wa Antiokia na katika jimbo la Suria na la Kilikia.
24Tumesikia kwamba watu fulani waliotoka huku kwetu pasipo ruhusa yetu wamewasumbua ninyi na maneno na kuwatia katika wasiwasi.
25Kwa sababu hii sisi tumekata shauri kwa nia moja, tukapatana kuchagua watu wamoja na kuwatuma kwenu. Watu hawa watawafikia pamoja na wapendwa wetu, Barnaba na Paulo,
26waliotoa maisha yao kwa ajili ya kumutumikia Bwana wetu Yesu Kristo.
27Ni hivi tunawatuma kwenu Yuda na Sila, nao watawaelezea waziwazi kwa kinywa maneno haya tunayowaandikia.
28Kwa maana kutokana na shauri la Roho Mutakatifu na shauri letu wenyewe tumeamua kwamba hatutawabebesha muzigo mwingine muzito kupita mapaswa haya ya lazima:
29musikule vyakula vilivyotolewa kwa kutambikia sanamu; musikule damu wala nyamafu; na muepuke uasherati. Mutafanya vema kama mukijitenga na mambo haya. Salamu kwenu.”
30Kisha kuagana, wale wajumbe wakaondoka na kwenda Antiokia. Kule wakakusanya kundi lote la waamini, wakawapa barua ile.
31Nao walipoisoma wakafurahi kwa ajili ya maneno ya kuwatia moyo yaliyoandikwa ndani yake.
32Na kufuatana na vile Yuda na Sila walivyokuwa manabii, wakawaonya kwa maneno mengi na kuwajenga moyo.
33Kisha kukaa kule kwa muda, wandugu waamini wakawaaga na kuwatakia amani wakawaruhusu kurudi kwa wale waliowatuma.
35Naye Paulo na Barnaba wakabakia Antiokia, na kule wao pamoja na watu wengine wengi walifundisha na kuhubiri neno la Bwana.
Paulo na Barnaba wanatengana36Nyuma ya siku chache, Paulo akamwambia Barnaba: “Turudi sasa kwa kuwaangalia wandugu waamini katika miji ambamo tulihubiri neno la Bwana, kusudi tuone kama wako katika hali gani.”
37Barnaba alitaka waende pamoja na Yoane, aliyeitwa vilevile Marko.
38Lakini Paulo hakuona vizuri kwenda naye kwa sababu alikuwa ameachana nao katika inchi ya Pamfilia, akikataa kuendelea nao katika kazi.
39Kwa hiyo Paulo na Barnaba wakabishana vikali hata wakatengana. Barnaba akaondoka pamoja na Marko, wakaingia ndani ya chombo na kwenda katika kisanga cha Kipuro.
40Naye Paulo akachagua kwenda na Sila, nao wandugu waamini walipokwisha kuwaombea neema kwa Mungu, wakaondoka.
41Akapita katika jimbo la Suria na Kilikia, na kule akayatia makanisa nguvu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.