Zaburi 8 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Utukufu wa Mungu na cheo cha mwanadamu

1Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa watu wa Gati. Zaburi ya Daudi.

2Ee Yawe, Bwana wetu,

jina lako linatukuzwa sana katika dunia yote!

Utukufu wako unaenea mpaka juu ya mbingu!

3Kutoka maneno ya watoto wadogo, hata wachanga,

unaimarisha nguvu mbele ya waadui zako

na kuwakomesha waasi na wapinzani wako.

4Nikiangalia mbingu uliyoumba kwa vidole vyako,

mwezi na nyota ulizozisimika huko,

5mutu ni nini, ee Mungu, hata umufikirie?

Mwanadamu ni nini hata umujali?

6Umemufanya kuwa karibu sawa na Mungu,

umemujaza utukufu na heshima.

7Ulimupa utawala juu ya vyote ulivyoviumba;

uliweka viumbe vyote chini ya mamlaka yake:

8kondoo, ngombe,

na nyama wa pori,

9ndege, samaki,

na viumbe vyote vya bahari.

10Ee Yawe, Bwana wetu,

jina lako linatukuzwa sana katika dunia yote!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help