Wafilipi 1 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Salamu

1Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa ndugu yetu Timoteo, sisi watumishi wa Yesu Kristo. Tunawaandikia watu wote wa Mungu wanaoungana na Yesu Kristo, wanaoishi Filipi, pamoja na wazee wa kanisa na wasaidizi.

2Tunawatakia neema na amani toka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo.

Paulo anaombea kanisa la Filipi

3Ninamushukuru Mungu wangu kwa ajili yenu kila mara ninapowakumbuka.

4Kila wakati ninapowaombea ninyi, ninaomba kwa furaha,

5kwa namna munashirikiana nami katika kazi ya kutangaza Habari Njema, tangu mwanzo mpaka sasa.

6Ninajua hakika kwamba Mungu aliyeanza kazi hii njema ndani yenu, ataitimiza mpaka siku ile ya kurudi kwa Yesu Kristo.

7Ni haki kwangu kuwa na mafikiri haya kwa ajili yenu ninyi wote, kwa sababu ninawakumbuka kila mara. Kwa maana mumeshiriki pamoja nami katika neema ile Mungu aliyonipatia, ingawa sasa niko katika kifungo hata na wakati nilipokuwa huru kutetea na kuimarisha Habari Njema.

8Mungu ni mushuhuda wangu kwamba ninawapenda sana ninyi wote na moyo wa upendo mukubwa wa Yesu Kristo.

9Na kitu ninachoomba kwa Mungu, ni kwamba upendo wenu uzidi kuongezeka katika ufahamu wa kweli na usikilivu kamili,

10kusudi mupate kutambua mambo yanayokuwa bora zaidi. Kwa hivi mutakuwa safi pasipo kosa kwa Siku ile ya kurudia kwa Kristo.

11Maisha yenu yatajazwa matendo ya haki ambayo Yesu Kristo anayowajalia, kwa ajili ya utukufu na sifa ya Mungu.

Kuishi kwa ajili ya Kristo

12Wandugu zangu, ninataka mujue kwamba mambo yaliyonifikia yamesaidia kwa kuendelesha Habari Njema.

13Kutokana na hayo, walinzi wote wa nyumba ya mufalme pamoja na wengine wote, wanajua kwamba niko katika kifungo kwa sababu ninamutumikia Kristo.

14Kwa ajili ya kufungwa kwangu, wandugu wengi wamemwamini Bwana na kuwa na bidii sana ya kutangaza Neno la Mungu pasipo woga.

15Ni kweli kwamba wengi kati yao wanahubiri habari za Kristo kwa wivu na ugomvi, lakini wengine wanahubiri katika nia nzuri.

16Hawa wanahubiri kwa upendo, kwa maana wanajua kwamba Mungu amenipatia kazi ya kuitetea Habari Njema.

17Wale wengine wanatangaza habari za Kristo na roho ya mapingano na nia yao ni mbaya, wanafikiri kwamba wataniongezea mateso katika kifungo.

18Basi si kitu! Ikiwa nia yao ni mbaya au ni nzuri habari za Kristo zinatangazwa kwa namna mbalimbali, kwa hiyo ninafurahi. Na nitaendelea kufurahi tena,

19kwa maana ninajua kwamba kwa ajili ya maombi yenu na kwa musaada wa Roho wa Yesu Kristo nitakombolewa.

20Kwa maana kama vile ninavyongojea na kutumainia sana, sitafezeheka hata kidogo. Lakini tangia sasa na hata siku zote, nitamutukuza Kristo kwa uhodari katika maisha yangu, ikiwa nitaishi au nitakufa.

21Hivi kwangu kuishi ni kwa ajili ya Kristo na kufa ni faida.

22Lakini ikiwa kama kuendelea kuishi ni kwa lazima kwa ajili ya kazi yangu, basi sijui nichague nini.

23Maana ninasongwa na mambo mawili. Ninatamani kujiendea na kukaa pamoja na Kristo, maana hili ndilo jambo bora zaidi.

24Lakini jambo la lazima zaidi kwa ajili yenu, mimi niendelee kuishi.

25Basi niko na uhakika juu ya jambo hili nami ninajua kwamba nitabaki. Nitakaa pamoja nanyi kwa kuwasaidia kusudi mupate kuendelea na kuwa na furaha katika imani.

26Halafu, nitakaporudia tena kwenu, mutajivuna zaidi kwa ajili yangu katika kuungana kwenu na Yesu Kristo.

27Kitu cha lazima ni kwamba mukuwe na mwenendo unaolingana na mafundisho ya Habari Njema ya Kristo. Kwa hivi hata kama nikikuja kuwaona au hata kama nisipokuja, nipate tu kusikia kwamba munasimama imara katika nia moja, na kwamba wote pamoja munapigana vita kwa ajili ya imani inayotokana na Habari Njema.

28Musiogope waadui zenu hata kidogo. Hii itakuwa kitambulisho kwao kwa kuhakikisha kwamba wanapotea, lakini kwenu ni kwamba munaokolewa. Na hii inatoka kwa Mungu.

29Kwa maana Mungu amewapa ninyi neema ya kumutumikia Kristo, na si kwa kumwamini tu, lakini vilevile kwa kuteswa kwa ajili yake.

30Sasa munashiriki pamoja nami katika vita. Ninyi muliniona nikipigana vita ile na hata sasa munasikia kama ninapigana vita ile.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help