1Yawe akazungumuza na Musa, kisha kufa kwa wana wawili wa Haruni wakati ule walipomukaribia.
2Akamwambia: Umwambie ndugu yako Haruni asiingie katika Pahali Patakatifu nyuma ya pazia wakati usiokubaliwa. Asiingie pahali pale maana ndipo nitakapotokea katika wingu juu ya kiti cha rehema. Asipotii, atakufa. .
9Ataleta yule beberu ambaye kura ilimwangukia kwa ajili ya Yawe na kumutolea sadaka kwa ajili ya zambi.
10Lakini yule beberu aliyeangukiwa na kura kwa ajili ya Azazeli atatolewa mbele ya Yawe akiwa muzima. Kwa kufanya ibada ya upatanisho, kuhani atamwacha aende katika jangwa kwa Azazeli, kwa ajili ya zambi za jamii.
11Haruni atatoa ngombe dume wa sadaka ya zambi kwa ajili yake mwenyewe, na kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya jamaa yake, kisha atachinja ngombe dume yule wa sadaka ya zambi.
12Halafu atatwaa chetezo na kutwaa makaa toka kwenye mazabahu mbele ya Yawe na mikono miwili ya ubani uliosagwa vizuri sana na atauleta ndani ya pazia.
13Kusudi asikufe, ataleta ubani ule mbele ya Yawe na kuutia katika moto kusudi moshi wa ubani ule ufunike kifuniko cha Sanduku la Agano.
14Atatwaa sehemu ya damu ya yule ngombe dume na kunyunyiza kwa kidole chake upande wa mashariki juu ya kiti cha rehema kisha atainyunyizia mbele ya Sanduku la Agano mara saba kwa kidole chake.
15Halafu atachinja yule beberu wa sadaka ya zambi kwa ajili ya watu wote. Damu ya mbuzi huyo ataileta ndani ya Pahali Patakatifu Sana na kufanya kama vile alivyofanya na damu ya yule ngombe dume; atainyunyiza juu ya kiti cha rehema, upande wake wa mbele. Ang. Ebr 9.12
16Hivyo atafanya ibada ya upatanisho kwa ajili ya Pahali Patakatifu kwa sababu ya uchafu, makosa na zambi zote za Waisraeli. Ndivyo atakavyofanya vilevile kwa ajili ya hema la mukutano linalokuwa kati ya watu hao wanaokuwa wachafu.
17Wakati Haruni anafanya ibada ya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe, jamaa yake na jamii nzima ya Israeli, kusikuwe hata mutu yeyote ndani ya hema la mukutano mpaka wakati atakapokuwa amemaliza na kutoka inje.
18Kisha atatoka na kwenda kwenye mazabahu inayokuwa mbele ya Yawe na kufanya ibada ya upatanisho. Atatwaa sehemu ya damu ya yule ngombe dume na ya yule mbuzi na kupakaa pembe za mazabahu pande zote.
19Atainyunyizia mazabahu hiyo damu kwa kidole chake mara saba na hivyo ataisafisha na kuitakasa toka uchafu wote wa watu wa Israeli.
20Kisha Haruni kumaliza kutakasa Pahali Patakatifu, hema la mukutano na mazabahu, ndipo atamutoa yule beberu kwa ajili ya Azazeli, akiwa muzima.
21Haruni ataweka mikono yake juu ya kichwa cha huyo beberu muzima na kuungama juu yake zambi zote za watu wa Israeli, makosa yao yote na zambi zao zote; naye ataziweka zote juu ya kichwa cha yule mbuzi. Kisha atamwacha huyo beberu aende katika jangwa akipelekwa kule na mutu yeyote anayekuwa tayari.
22Atamwacha huyo beberu aende katika jangwa, pahali pasipokuwa watu, akiwa amebeba maovu yao yote.
23Kisha Haruni atarudi ndani ya hema la mukutano, atavua na kuziacha mule zile nguo alizovaa alipoingia katika Pahali Patakatifu Sana. Ang. Eze 44.19
24Ataoga mule katika Pahali Patakatifu na kuvaa nguo zake. Atatoka na kutolea sadaka yake ya kuteketezwa, na sadaka ya kuteketezwa ya watu wa Israeli, kwa kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote.
25Mafuta ya sadaka kwa ajili ya zambi atayateketeza juu ya mazabahu.
26Yule mutu aliyepeleka yule beberu kwa Azazeli kwanza atafua nguo zake na kuoga ndipo atakapoweza kuingia ndani ya kambi.
27Yule ngombe dume na mbuzi waliotolewa sadaka kwa ajili ya zambi ambao damu yao ilipelekwa katika Pahali Patakatifu kwa kufanya ibada ya upatanisho, watapelekwa inje ya kambi na kuteketezwa kwa moto. Ngozi zao, nyama na mavi yao, vyote vitateketezwa kwa moto. Ang. Ebr 13.11
28Yule mutu atakayewateketeza atafua nguo zake na kuoga, ndipo atakapoweza kuingia katika kambi.
29Hili ni sharti la kufuata siku zote: Siku ya kumi ya mwezi wa saba, ninyi wenyewe na hata wageni wanaoishi kati yenu, munapaswa kufunga kula siku hiyo na kuacha kufanya kazi. Law 23.26-32; Hes 29.7-11
30Mutafanya hivyo kwa sababu siku hiyo ndiyo siku ambayo mutafanyiwa ibada ya upatanisho, musafishwe zambi zenu, nanyi mutakuwa safi mbele ya Yawe.
31Siku hiyo ni siku ya mapumziko kamili nanyi mutafunga. Hili ni sharti la kufuata siku zote.
32Kuhani aliyepakwa mafuta na kutakaswa ashike nafasi ya baba yake, ndiye atakayefanya ibada ya upatanisho akiwa amevaa nguo takatifu ya kitani.
33Atafanya ibada ya upatanisho kwa ajili ya Pahali Patakatifu Sana, kwa ajili ya hema la mukutano, mazabahu, makuhani, na kwa ajili ya jamii nzima ya Israeli.
34Hili ni sharti la kufuata siku zote. Linapaswa kufuatwa kwa kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili ya watu wa Israeli mara moja kila mwaka na kusamehewa zambi zao.
Musa akafanya yote kama vile alivyoamuriwa na Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.