1Mwaka wa saba tangu kuhamishwa kwetu, siku ya kumi ya mwezi wa tano, wazee wamoja wa Waisraeli walikuja kumwuliza Yawe shauri, wakaikaa mbele yangu.
2Basi, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
3Wewe mwanadamu, sema na hao wazee wa Waisraeli. Uwaambie kwamba:
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mumekuja kuniuliza shauri? Kama vile ninavyoishi, sitakubali kuulizwa shauri na ninyi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
4Wewe mwanadamu, uko tayari kuwahukumu watu hawa? Basi, uwahukumu. Uwajulishe mambo wazee wao waliyofanya.
5Uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ile nilipowachagua Waisraeli niliwaapia wazao wa Yakobo. Nilijijulisha kwao katika inchi ya Misri, nikawaapia nikisema: Mimi ni Yawe, Mungu wenu. Ang. Kut 6.2-8
6Siku hiyo niliwaapia kwamba nitawatoa katika inchi ya Misri na kuwapeleka mpaka kwenye inchi niliyowachagulia, inchi ya maziwa na asali na inchi nzuri kuliko inchi zote.
7Niliwaambia: Mutupilie mbali machukizo yote munayoyapenda; musijichafue na sanamu za miungu ya Misri, kwa maana mimi ni Yawe, Mungu wenu.
8Lakini waliniasi, hawakutaka kunisikiliza. Hakuna hata mumoja kati yao aliyetupilia mbali machukizo yale waliyoyapenda, wala hawakuachana na sanamu za miungu ya Misri. Basi, nikafikiri kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuitimiza hasira yangu juu yao wakiwa kulekule katika inchi ya Misri.
9Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa wanaoishi nao, hao walioona nikijijulisha kwa Waisraeli wakati wa kuwatoa katika inchi ya Misri.
10Basi, mimi niliwatoa katika inchi ya Misri, nikawapeleka katika jangwa.
11Niliwapa masharti yangu na kuwafundisha maagizo yangu ambayo mutu akiyafuata ataishi. Ang. Law 18.5
12Niliwapa vilevile Sabato zangu zikuwe kitambulisho kati yangu na wao, wapate kujua kwamba mimi ni Yawe ninayewatakasa. Ang. Kut 31.13-17
13Lakini Waisraeli waliniasi kule katika jangwa; hawakuyafuata masharti yangu, lakini walikataa maagizo yangu ambayo mutu akiyafuata ataishi. Sabato zangu walizikufuru siku zote, nami nikasema kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuwaangamiza kulekule katika jangwa.
14Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa ambao waliona jinsi nilivyowatoa Waisraeli katika inchi ya Misri.
15Hata hivyo, niliwaapia kulekule katika jangwa kwamba sitawaingiza katika inchi niliyowapa, inchi ya maziwa na asali na inchi nzuri kuliko inchi zote. Ang. Hes 14.26-35
16Nilifanya hivyo kwa sababu waliyakataa maagizo yangu, hawakufuata masharti yangu, wakazikufuru Sabato zangu; maana walijitoa kwa moyo juu ya sanamu za miungu yao.
17Lakini nikawaonea huruma, sikuwaangamiza kule katika jangwa.
18Niliwaonya wazao wao kule katika jangwa: Musifuate masharti ya wazee wenu, musishike maagizo yao wala musijichafue kwa kuziabudu sanamu za miungu yao.
19Mimi Yawe ni Mungu wenu. Mufuate masharti yangu, mushike maagizo yangu kwa uangalifu.
20Mufanye Sabato zangu kuwa takatifu, kusudi zikuwe kitambulisho cha agano langu nanyi. Hizo zitawakumbusha kwamba mimi Yawe ni Mungu wenu.
21Lakini hata wazao wao hao waliniasi. Hawakufuata masharti yangu, hawakushika wala kutimiza maagizo yangu ambayo mutu akiyashika, ataishi. Walizikufuru Sabato zangu. Basi nikasema kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuitimiza hasira yangu juu yao kule katika jangwa.
22Lakini nilizuiza mukono wangu kwa sababu ya heshima ya jina langu kusudi nisizarauliwe kati ya watu wa mataifa walioona nikiwatoa katika inchi ya Misri.
23Hata hivyo, niliapa kulekule katika jangwa kwamba ningewapeleka katika inchi za mbali na kuwafanya waishi kati ya mataifa ya kigeni, Ang. Law 26.33
24kwa sababu hawakufuata maagizo yangu, lakini waliyakataa masharti yangu, wakazikufuru Sabato zangu na kuziabudu sanamu za miungu ya wazee wao.
25Tena niliwapa masharti mabaya na maagizo ambayo hayawezi kuwawezesha kuishi.
26Nikawaacha wajichafue kwa sadaka zao za kuwatoa wazaliwa wao wa kwanza sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Hili lilikuwa pigo lao la azabu ya kutisha kusudi watambue kwamba mimi ni Yawe.
27Sasa, wewe mwanadamu, uwaambie Waisraeli kwamba:
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Wazee wenu walinikufuru kila mara kwa kukosa uaminifu.
28Maana nilipowapeleka katika ile inchi niliyoapa kuwapa, kila mara walipoona kilima kirefu au miti ya majani mengi, walianza kutoa matambiko na sadaka zao na kunichokoza. Kulekule walitoa sadaka za harufu nzuri na kutoa sadaka za kinywaji.
29(Mimi nikawauliza: Pahali hapo palipoinuka munapokwenda panaitwa namna gani? Wao wakapaita Pahali Palipoinuka mpaka leo.)
30Basi, uwaambie Waisraeli kwamba:
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mutajichafua kwa kufuata desturi za wazee wenu na kuviabudu vitu vinavyonichukiza?
31Munapoendelea kutoa sadaka zenu na kuwateketeza watoto wenu kwa moto munajichafua mpaka leo hii. Nitaulizwa shauri nanyi, enyi watu wa Israeli? Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– sitakubali kuulizwa shauri nanyi.
32Ninyi munasema ndani ya mioyo yenu: Tutakuwa kama mataifa mengine, kama makabila ya inchi ingine na kuabudu miti na mawe. Hayo munayofikiri ndani ya mioyo yenu hayatafanikiwa hata kidogo.
Mungu anaazibu na kusamehe33Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– nitawatawala kwa mukono wenye nguvu, kwa ukali na kuwamwangia kasirani yangu.
34Nitawatoa kutoka mataifa na kuwakusanya kutoka katika inchi mulimosambazwa kwa mukono wangu wenye nguvu, kwa ukali na kwa kasirani yangu.
35Nitawapeleka kwenye jangwa la mataifa; na huko nitawahukumu moja kwa moja.
36Kama nilivyowahukumu wazee wenu kule katika jangwa katika inchi ya Misri, ndivyo nitakavyowahukumu ninyi.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
37Nitawalazimisha mukuwe chini ya uchungaji wangu kila mumoja, na kuwaongoza mupate kutii agano langu.
38Nitaondoa kati yenu waasi na wale wanaonikosea; nitawaondoa katika inchi walikokaa kama wakimbizi, lakini hawataingia hata kidogo katika inchi ya Waisraeli. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.
39Na sasa, enyi Waisraeli, Bwana wenu Yawe anawaambia hivi: Muendelee kuziabudu sanamu zenu za miungu, kama hamunisikilizi; lakini mutalazimishwa kuacha kulikufuru jina langu takatifu kwa sadaka na sanamu zenu.
40Maana, katika mulima wangu mutakatifu, mulima murefu wa Israeli, ninyi wote watu wa Israeli mutanitumikia kule.
–Ni ujumbe wa Yawe.–
Huko mimi nitawapokea na kungojea muniletee sadaka na matoleo yenu bora na matoleo iliyotakaswa.
41Kisha kuwatoa toka katika inchi ambako mumesambazwa na kuwakusanya pamoja, nitazipokea sadaka zenu zenye harufu nzuri. Nami nitaonyesha utakatifu wangu kati yenu mbele ya mataifa mengine.
42Nanyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe, wakati nitakapowarudisha mpaka katika inchi ya Israeli, inchi niliyoapa kuwapatia wazee wenu.
43Huko ndiko mutakapokumbuka mwenendo wenu na matendo yenu mabaya ambayo yaliwachafua; nanyi mutachukizwa kabisa kwa sababu ya maovu yote muliyotenda.
44Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe, wakati nitakapowatendea ninyi sio kulingana na mwenendo wenu na matendo yenu mabaya, lakini kwa heshima ya jina langu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.