1Ninawatumia dada yetu mwamini Foibe, anayekuwa musaidizi wa kanisa la Kenkurea.
2Mumupokee kwa ajili ya Bwana, kama vile watu wa Mungu wanavyopaswa kufanya. Mumusaidie katika kila jambo atakalohitaji toka kwenu, maana yeye amewasaidia watu wengi na hata mimi peke yangu vilevile.
3Munisalimie Prisila na Akila, watumishi wenzangu katika kazi ya Yesu Kristo.
4Wao walijitolea kufa kwa kuokoa maisha yangu. Ninawashukuru, wala si mimi peke yangu tu, nayo makanisa yote ya inchi za watu wa mataifa wanawashukuru vilevile.
5Munisalimie vilevile kanisa linalokusanyika katika nyumba yao. Munisalimie mupendwa wangu Epeneto, anayekuwa mwamini wa kwanza wa Kristo katika jimbo la Azia.
6Munisalimie Maria, aliyewashugulikia sana.
7Munisalimie wanainchi wenzangu Androniko na Yunia, waliofungwa pamoja nami katika kifungo. Wao wanasifiwa sana kati ya mitume, nao walikuwa katika Kristo mbele yangu.
8Munisalimie Ampuliato, mupendwa wangu katika Bwana.
9Munisalimie Urbano, mutumishi mwenzetu katika kazi ya Kristo, na Staki, mupendwa wangu.
10Munisalimie Apele, aliyehakikisha uaminifu wake katika Kristo. Munisalimie watu wanaoishi katika nyumba ya Aristobulo.
11Munisalimie Herodio, mwanainchi mwenzangu. Munisalimie watu wanaoishi katika nyumba ya Narkiso, wanaomwamini Bwana.
12Munisalimie Tirifena na Tirifosa, wale wanawake wanaomushugulikia Bwana, na mupendwa wangu Persi, aliyemushugulikia sana Bwana.
13Munisalimie Rufo, mutumishi hodari katika kazi ya Bwana, na mama yake ninayemuhesabu kama mama yangu vilevile.
14Munisalimie Asinkristo, Fulego, Herme, Patroba, Herma, na wandugu wanaoshiriki pamoja nao.
15Munisalimie Filologo na Yulia, Nereo na dada yake, na Olimpa, na watu wote wa Mungu wanaoshiriki pamoja nao.
16Musalimiane kwa upendo wa kikristo. Makanisa yote ya Kristo yanawasalimia.
17Wandugu zangu, ninawasihi, mufanye angalisho na wale wanaoleta matengano na mambo ya kuwapotoa wengine wakipinga mafundisho muliyopokea. Mujitenge mbali nao.
18Kwa maana watu wa namna hii hawamutumikii Bwana wetu Kristo, lakini wanatumikia tu tumbo yao wenyewe. Tena kwa maneno yao matamu na ya kujipendekeza wanadanganya watu wasiokuwa na makosa.
19Watu wote wanajua namna munavyomutii Bwana, na kwa sababu hii ninafurahi kwa ajili yenu. Lakini ninataka mukuwe wenye hekima kwa kutenda mema, na mukuwe safi mukijitenga na mambo mabaya.
20Mungu, anayeleta amani, atamupondaponda sasa hivi Shetani chini ya miguu yenu.
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo ikuwe pamoja nanyi.
21Timoteo, mutumishi mwenzangu anawasalimia, nao Lukio, Yasoni, na Sosipateri, wanainchi wenzangu wanawasalimia vilevile.
22Mimi Tertio, niliyeandika barua hii, ninawasalimia kwa jina la Bwana.
23Gayo, aliyenikaribisha na anayekaribisha kanisa zima kwa kukusanyika kwake, anawasalimia. Erasto, mulinzi wa mali ya muji, pamoja na ndugu yetu Kwarto, wanawasalimia.
[
24Tunawatakia ninyi wote neema kutoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Amina.]
25Mungu asifiwe! Yeye yuko na uwezo wa kuwaimarisha katika imani juu ya Habari Njema ninayotangaza kwa kuhubiri ujumbe juu ya Yesu Kristo, kufuatana na ufunuo wa siri iliyofichwa tangia zamani za kale na kale.
26Lakini sasa yamefunuliwa na maandiko ya manabii kufuatana na amri ya Mungu wa milele, kusudi mataifa yote yapate kumwamini na kumutii.
27Basi Mungu anayekuwa peke yake mwenye hekima atukuzwe milele na milele kwa njia ya Yesu Kristo! Amina.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.