1Zambi ya watu wa Yuda, haiwezi kufutikana, imeandikwa kwa kalamu ya chuma; kwa chongo ya almasi. Imechorwa ndani ya mioyo yao na kwenye pembe za mazabahu yao.
2Watoto wao wanakumbuka mazabahu zao na sanamu za mungu muke, Ashera, zilizowekwa kando ya miti mibichi, juu ya vilele vya vilima
3na juu ya milima katika mbuga. Mali yenu na akiba zenu zote nitazitoa zitekwe kwa kulipia zambi zenu mulizotenda kila pahali katika inchi yenu.
4Itawabidi kuiacha hiyo inchi yenu niliyowapa, nami nitawafanya muwatumikie waadui zenu katika inchi musiyoijua, kwa sababu hasira yangu imewaka kama moto usiozimika hata milele.
Misemo mbalimbali5Yawe anasema hivi:
Alaaniwe mutu anayemutegemea mwanadamu,
mutu ambaye anategemea nguvu za mwanadamu,
mutu ambaye moyo wake umegeuka mbali nami Yawe.
6Huyo ni kama kichaka katika jangwa,
hataona mazuri yoyote.
Ataishi pahali penye kukauka katika jangwa,
kwenye udongo ulioharibiwa na chumvi,
na usiokaliwa na watu.
7Abarikiwe mutu anayenitegemea mimi Yawe,
mutu ambaye mimi Yawe ndiye tegemeo lake.
8Huyo ni kama muti uliopandwa kando ya maji,
unaopenyeza mizizi yake karibu na chemichemi.
Hauogopi wakati wa jua kali,
majani yake yanabaki mabichi.
Hauhangaiki katika mwaka wa ukosefu wa mvua,
nao haukosi kuzaa matunda.
9Moyo wa mutu ni mudanganyifu kuliko vitu vyote;
hauwezi kuponyeshwa, hakuna anayeweza kuuelewa!
10Mimi Yawe ninapima akili
na kuchunguza moyo wa mutu.
Na hivyo ninamutendea kila mumoja,
kulingana na mwenendo wake,
kadiri ya matendo yake.
11Mutu anayepata mali isiyokuwa ya usawa
ni kama kwale anayelalia mayai ambayo hakutaga.
Mali yanamwishia angali kijana,
na kwa mwisho anageuka sawa mupumbafu.
12Kuna kiti cha kifalme chenye utukufu
kinachoinuka juu tangu mwanzo wa vyote,
ndipo pahali petu patakatifu.
13Ee Yawe, tumaini la Waisraeli,
wote wanaokukataa wafezeheshwe.
Wanaokuacha wewe watatoweka,
kama majina yaliyoandikwa chini katika mavumbi,
kwa maana wamekuacha wewe Yawe,
unayekuwa chemichemi ya maji ya uzima.
Maombi ya Yeremia14Uniponyeshe, ee Yawe, nami nitapona;
uniokoe, nami nitaokoka;
maana, wewe ndiwe sifa yangu.
15Angalia jinsi watu wanavyoniambia:
Vile vitisho vya Yawe viko wapi?
Vifike basi!
16Sikukukaza kutenda mabaya,
wala sikutamani ile siku ya hasara ifike.
Wewe mwenyewe unajua maneno niliyosema mbele yako.
17Usiniletee hofu;
maana wewe ndiwe kimbilio langu siku ya hasara.
18Uwapatishe haya wale wanaonitesa,
lakini usiniache mimi kupata haya.
Uwafezeheshe watu hao,
lakini usiniache mimi kufezeheka.
Uwaletee ile siku ya hasara,
uwaangamize kabisakabisa!
19Yawe aliniambia hivi: Kwenda usimame kwenye Mulango wa Wanainchi, ambako wafalme wa Yuda wanapitia wanapoingia au kutoka Yerusalema. Uende vilevile kwenye milango yake yote ingine na kutangaza hivi:
20Musikie neno la Yawe, enyi wafalme wa Yuda, ninyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema ambao wanaopitia kwenye milango hii.
21Uwaambie kwamba:
Yawe anasema hivi: Mufanye angalisho kwa ajili ya maisha yenu. Musibebe muzigo siku ya Sabato, au kuingiza muzigo katika Yerusalema kupitia kwenye milango ya muji.
22Musibebe muzigo kutoka nyumba zenu siku ya Sabato wala kufanya kazi yoyote. Lakini muihesabu siku ya Sabato kuwa takatifu kama nilivyowaamuru babu zenu.
23Ingawa hivyo babu zenu hawakunisikiliza wala kunitegea sikio, lakini walifanya vichwa vyao kuwa vigumu, wakakataa kusikia na kufuata maagizo yangu.
24Lakini ninyi munisikilize mimi. Muache kuingiza muzigo wowote kupitia kwenye milango ya muji huu siku ya Sabato, muihesabu kuwa takatifu na kutofanya kazi.
25Halafu, wafalme na wana wao watakaotawala nyuma juu ya kiti cha kifalme cha Daudi, wanaopanda juu ya farasi na magari yenye kukokotwa pamoja na watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema, wataendelea kuingia ndani ya muji huu wakipitia kwenye milango hii. Nao muji huu utaikaliwa na watu siku zote.
26Watu watakuja kutoka miji ya Yuda na maeneo ya kandokando ya Yerusalema, kutoka inchi ya kabila la Benjamina, kutoka Shefela, kutoka inchi ya milima na kutoka Negebu, wakileta sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine za kawaida, sadaka ya mavuno na ya ubani wenye harufu nzuri pamoja na matoleo ya shukrani. Hivyo vyote watavileta katika nyumba ya Yawe.
27Lakini musiponisikiliza na mukiacha kuihesabu siku ya Sabato kama siku takatifu, musipoacha kubeba mizigo na kuingia nayo kupitia milango ya Yerusalema siku ya Sabato, basi nitawakisha moto katika milango yake, nao utateketeza nyumba zote nzuri za Yerusalema, wala hautazimika.
–Ni ujumbe wa Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.