Waamuzi 19 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mulawi na habara yake

1Wakati ule hakukukuwa bado mufalme katika Israeli.

Kulikuwa Mulawi mumoja aliyeishi kama mugeni mbali katika eneo la milima ya Efuraimu. Mutu yule alitwaa habara kutoka Betelehemu katika inchi ya Yuda.

2Lakini habara yule akamukasirikia yule Mulawi, akamwacha na kurudi katika nyumba ya baba yake kule Betelehemu, akakaa kwa muda wa miezi mine.

3Siku moja, mume wake akakwenda kumutafuta. Alikusudia kuongea naye vizuri na kumurudisha kwa nyumba yake. Akakwenda pamoja na mutumishi wake na punda wawili. Basi yule mwanamuke akamupeleka ndani kwa baba yake, naye baba mukwe alipomwona akamupokea kwa furaha.

4Baba mukwe akamukaribisha, naye akakaa kule kwa muda wa siku tatu. Yule Mulawi na mutumishi wake wakakula, wakakunywa na kulala kule.

5Siku ya ine, wakaamuka asubui mapema, wakajitayarisha kuondoka; lakini baba wa yule mwanamuke akamwambia: “Kwanza kula chakula kidogo upate nguvu, kisha uondoke.”

6Basi hao watu wawili wakaikaa, wakakula na kunywa pamoja. Kisha baba mukwe akamwambia: “Tafazali, ulale hapa usiku huu na kufurahi.”

7Yule mutu aliposimama akitaka kuondoka, baba mukwe akamusihi abaki, naye akabaki.

8Siku ya tano yule mutu akaamuka asubui, akataka kuondoka. Lakini baba ya yule mwanamuke akamwambia: “Kwanza upate nguvu kwa kula, ungoje mpaka jua litakaposhuka, halafu uondoke.” Basi wote wawili wakakula pamoja.

9Yule Mulawi na habara yake pamoja na mutumishi wake waliposimama kwenda zao, baba mukwe wake akamwambia yule Mulawi: “Sasa muchana umekwisha na magaribi imekaribia. Ulale hapa, na kufurahi. Kesho asubui utaamuka mapema kuanza safari yako ya kurudi kwako.”

10Lakini yule mutu akakataa kulala kule usiku ule. Basi, akasimama, akaondoka, akafika karibu na muji wa Yebusi, ni kusema Yerusalema. Alikuwa na wale punda wake wawili waliotandikwa tayari, pamoja na habara yake.

11Walipokuwa wanakaribia muji wa Yebusi, siku ilikuwa karibu imekwisha, naye mutumishi akamwambia bwana wake: “Sasa heri tuingie katika muji huu wa Wayebusi tulale mule usiku huu.”

12Bwana wake akamujibu: “Hatutageuka na kuingia katika muji wa wageni ambao si Waisraeli. Tutaendelea na safari mpaka Gibea.

13Tuende tukaribie sehemu hizo na kulala kule Gibea au Rama.”

14Basi, wakaendelea na safari yao mpaka jua likatua wakiwa karibu na muji wa Gibea ambao ni muji wa kabila la Benjamina.

15Wakaingia ndani ya muji wapate kulala mule usiku. Walipoingia katika muji, wakaenda kukaa kwenye kiwanja cha makutano cha muji, maana hakuna mutu aliyewakaribisha ndani ya nyumba yake.

16Walipokuwa kule muzee mumoja akafika kutoka kwa shamba lake. Muzee huyo alikuwa mutu wa inchi ya milima ya Efuraimu na alikuwa akiishi kule Gibea kama mugeni. Wakaaji wa muji wa Gibea walikuwa wa kabila la Benjamina.

17Muzee yule alipoangalia na kumwona yule musafiri akiwa kule katika kiwanja, akamwuliza: “Umetoka wapi na unakwenda wapi?”

18Naye akamujibu: “Tunatoka Betelehemu katika inchi ya Yuda na tunaelekea sehemu za mbali za eneo la milima ya Efuraimu. Kule ndiko ninakoishi na sasa ninarudi katika safari toka kule Betelehemu katika Yuda na kurudia kwangu; hakuna mutu hapa aliyetukaribisha katika nyumba yake.

19Lakini sisi watumishi wako tuna nyasi na malisho kwa ajili ya punda wetu. Vilevile nina mukate na divai; hivyo vinanitosha mimi, habara wangu na mutumishi wangu. Hatukosewi kitu chochote.”

20Huyo muzee akamwambia: “Amani ikuwe nanyi! Nitawapa mahitaji yote. Lakini musilale huku katika kiwanja.”

21Hivyo akawapeleka katika nyumba yake na kuwapa punda wao malisho. Hao wasafiri wakanawa miguu yao, wakakula na kunywa.

22Walipokuwa wanajifurahisha, kumbe wanaume watenda maovu wa muji ule wakakuja wakaizunguka nyumba ile na kugonga kwa mulango. Wakamwambia muzee mwenye nyumba: “Umutoshe inje yule mwanaume aliyekuja kwako, tulale naye.”

23Lakini yule muzee mwenye nyumba akatoka inje, akawaambia: “Sivyo wandugu zangu. Ninawasihi musitende uovu ule. Huyu ni mugeni wangu. Musimutendee ubaya ule.

24Ningali na binti yangu ambaye ni bikira na kuna vilevile yule habara wa mugeni wangu. Muniruhusu niwatoshe inje, muwakamate na kuwatendea kama munavyotamani, lakini mutu huyu musimutendee jambo hilo la kipumbafu.”

25Lakini wanaume hao hawakumusikiliza. Kwa hiyo Mulawi yule akamutwaa habara yake na kumutoa kwao kule inje. Nao wakamutwaa na kulala naye kwa kinguvu usiku kucha mpaka asubui. Karibu na mapambazuko, wakamwacha aende zake.

26Asubui, yule mwanamuke akakuja mpaka kwenye mulango wa nyumba ambamo bwana wake alikuwa, akaanguka chini pale kwenye mulango na kubakia pale mpaka kulipopambazuka kabisa.

27Bwana wa mwanamuke yule alipoamuka asubui, akafungua milango ya nyumba, akatoka inje kusudi aendelee na safari. Kwa rafla akamukuta habara yake amelala chini mbele ya mulango, mikono yake ikishika kizingiti cha mulango.

28Akamwambia: “Simama tuende.” Lakini yeye hakujibu kitu. Akamukamata, akamuweka juu ya punda wake na kumupeleka mpaka kwake.

29Alipofika kwake akatwaa kisu na kumukatakata yule habara vipande kumi na viwili. Kisha akavipeleka vipande hivyo katika maeneo yote ya inchi ya Israeli.

30Wale wote walioona jambo hilo wakasema: “Jambo kama hili halijatukia wala kuonekana tangu siku ile Waisraeli walipotoka katika inchi ya Misri mpaka leo. Tufikiri juu yake, tushauriane na kuamua.”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help