1Daudi alipokuwa muzee wa miaka mingi, akamuweka Solomono mwana wake kuwa mufalme wa Israeli. Kazi ya Walawi
2Mufalme Daudi akawakusanya wakubwa wote wa Israeli, makuhani na Walawi.
3Walawi wote wanaume wenye umri wa miaka makumi tatu na zaidi, wakahesabiwa. Jumla yao ilikuwa elfu makumi tatu na nane.
4Halafu, Daudi akawagawanya: elfu makumi mbili na nane kati yao wakuwe wasimamizi wa kazi ya nyumba ya Yawe, elfu sita wakuwe wakubwa na waamuzi,
5elfu ine wakuwe walinzi wa milango, na elfu ine wakuwe waimbaji, wakimusifu Yawe kwa ala za muziki mufalme alizotengeneza mwenyewe kwa ajili ya kazi hiyo.
6Daudi akawagawanya Walawi katika makundi matatu kulingana na ukoo za kabila la Lawi: ukoo wa Gersoni, ukoo wa Kohati na ukoo wa Merari.
7Wana wa Gersoni walikuwa: Ladani na Simei.
8Wana wa Ladani walikuwa watatu: Yehieli mukubwa wao, Zetamu na Yoeli.
9Wana wa Simei walikuwa watatu: Selomoti, Hazieli na Harani. Hawa walikuwa viongozi wa ukoo wa Ladani.
10Wana wengine wane wa Simei walikuwa: Yahati, Zina, Yeusi na Beria.
11Yahati ndiye aliyekuwa mukubwa wao, akifuatwa na Zina. Lakini Yeusi na Beria, kwa vile hawakukuwa na wana wengi, walihesabiwa kama vile ukoo mumoja.
12Wana wa Kohati walikuwa wane: Amuramu, Isari, Hebroni na Usieli.
13Wana wa Amuramu walikuwa: Haruni na Musa. Haruni alichaguliwa kwa kazi inayoelekea vitu vitakatifu kabisa, hata wazao wake siku zote wafukizie ubani mbele ya Yawe, wakimutumikia na kuwabariki watu katika jina la Yawe milele. Ang. Kut 28.1
14Lakini wana wa Musa, mutu wa Mungu wanatajwa katika kabila la Lawi.
15Wana wa Musa walikuwa: Gersoni na Eliezeri.
16Mukubwa kati ya wana wa Gersoni alikuwa: Sebueli.
17Mwana wa pekee wa Eliezeri alikuwa: Rehabia.
Rehabia alikuwa na wana wengi sana.
18Mwana wa Isari alikuwa: Selomiti, kiongozi wa kabila zima.
19Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria, mukubwa wao; Amaria, wa pili; Yahazieli, wa tatu; na Yekameamu, wa ine.
20Wana wa Uzieli walikuwa: Mika mukubwa wao, na Isia wa pili.
21Wana wa Merari walikuwa: Mali na Musi.
Wana wa Mali walikuwa: Eleazari na Kisi.
22Eleazari alikufa bila mwana, lakini wabinti tu. Wabinti wale wakaolewa na binamu zao, wana wa Kisi.
23Wana wa Musi walikuwa watatu: Mali, Ederi na Yeremoti.
24Hao ndio wana wa Lawi kulingana na ukoo zao. Kila mumoja wao aliyetimiza umri wa miaka makumi mbili na zaidi, aliandikishwa kwa jina, na alishiriki katika kazi ya kujenga nyumba ya Yawe.
25Daudi akasema: “Yawe, Mungu wa Israeli, amewapa watu wake amani, naye ataishi Yerusalema kwa milele.
26Kwa hiyo, Walawi hawatahitaji tena kubeba hema takatifu au vyombo vyake vya ibada.” Ang. Kumb 10.8
27Kulingana na maagizo ya mwisho Daudi aliyotoa, Walawi wote waliofikia umri wa miaka makumi mbili waliandikishwa.
28Kazi yao ilikuwa ni kuwasaidia makuhani wa ukoo wa Haruni katika kazi ya kujenga nyumba ya Yawe, kutunza viwanja na vyumba, kusafisha vyombo vitakatifu vyote na kufanya kazi zinazoelekea kujenga nyumba ya Yawe. Ang. Hes 3.5-9
29Pamoja na hayo, walisaidia katika kazi kutayarisha mikate mitakatifu, unga safi na sadaka ya vyakula, maandazi yasiyotiwa chachu, sadaka ya mikate iliyokaangwa, sadaka ya mikate iliyochanganywa na mafuta, na sadaka katika kazi ya upimaji wa wingi wa sadaka na ukubwa wake.
30Walisimama kwa kumushukuru na kumusifu Yawe kila siku asubui na magaribi,
31na wakati wa siku za Sabato, mwandamo wa mwezi na sikukuu zingine, pale sadaka za kuteketezwa kwa moto zilipotolewa kwa Yawe. Sheria ziliwekwa kuelekea hesabu ya Walawi walioagizwa kufanya kazi zile siku zote mbele ya Yawe.
32Kwa hiyo, ilikuwa ni kazi yao kutunza hema la kusanyiko na Pahali Patakatifu, na kuwasaidia wandugu zao makuhani, wazao wa Haruni, kwenye ibada katika nyumba ya Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.