1Katika siku za utawala wa Ahazi mwana wa Yotamu na mujukuu wa Uzia, wa inchi ya Yuda, Resini, mufalme wa Aramu, na Peka mwana wa Remalia, mufalme wa Israeli, walienda kuushambulia Yerusalema, lakini hawakuweza kuunyanganya. , kukutana na mufalme Ahazi. Utamukuta katika barabara pahali wafuaji wa nguo wanapofanyia kazi, mwisho wa mufereji unaoleta maji kutoka kwenye birika la juu.
4Umwambie akuwe macho, atulie na asiogope wala asivunjike moyo, kwa sababu ya hasira kali ya mufalme Resini wa Aramu, na ya mwana wa Remalia. Hao wawili ni kama tu moshi wa kuni zinazozimika.
5Waaramu na vilevile Peka pamoja na jeshi lake la Efuraimu wamefanya mupango mubaya juu yako. Wamesema:
6Tuende kushambulia inchi ya Yuda, tuwaogopeshe watu wake, tuitwae inchi na kumuweka mwana wa Tabeali kuwa mufalme wao.
7Lakini Bwana wetu Yawe anasema hivi:
Jambo hilo halitatukia. Haitakuwa vile.
8-9Maana muji mukubwa wa Aramu ni Damasiki,
na huyo Resini ni mukubwa wa Damasiki tu.
Muji mukubwa wa Efuraimu ni Samaria,
na mwana wa Remalia ni mukubwa wa Samaria tu.
Katika miaka makumi sita na mitano utawala wa Efuraimu utavunjwa;
Efuraimu halitakuwa taifa tena.
Kama hautaamini, hautaimarika.
Alama ya kuzaliwa kwa Emanueli10Tena Yawe akamwambia Ahazi:
11Umwombe Yawe, Mungu wako, akupe kitambulisho; kikuwe ni kutoka chini kuzimu au juu mbinguni.
12Ahazi akajibu: Sitaomba kitambulisho! Sitaki kumujaribu Yawe.
13Basi, Isaya akamujibu: Musikilize basi, enyi watu wa ukoo wa Daudi! Haitoshi kuwachokesha watu hata sasa munataka kumuchokesha Mungu wangu vilevile?
14Basi, Bwana mwenyewe atawapa kitambulisho: bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume na kumwita jina lake “Emanueli – Mungu Yuko Pamoja Nasi”. Ang. Mat 1.23
15Atakula maziwa na asali mpaka atakapojua kukataa mabaya na kuchagua mema.
16Maana, mbele mutoto huyo hajajua kukataa mabaya na kuchagua mema, inchi za wafalme hao wawili unaowaogopa zitakuwa ukiwa.
17Yawe atakuletea wewe pamoja na watu wako na jamaa yote ya kifalme siku za taabu kuliko zile zote zilizotokea tangu wakati watu wa Efuraimu walipojitenga na watu wa Yuda; ni kusema, atawaletea ninyi mufalme wa Asuria.
18Wakati huo, Yawe atawapigia muunzi watu wa Misri wakuje kama mainzi toka vijito vya mito Nili; na watu wa Asuria wakuje kama nyuki kutoka inchi yao.
19Watakuja makundi kwa makundi na kuyajaza mabonde yenye miinuko, mapango ndani ya mawe, miiba, vichaka vyote na mashamba yote ya kukulishia nyama.
20Wakati ule, Bwana atalipa wembe kutoka ngambo ya muto Furati, ni kusema mufalme wa Asuria. Atawanyoa vichwa vyenu, miili yenu na ndevu zenu vilevile.
21Wakati ule, mutu atafuga ngombe mumoja muchanga na kondoo wawili;
22nao watatoa maziwa kwa wingi hata aweze kula siagi. Watu watakaobaki katika inchi watakula maziwa na asali.
23Wakati huo, kila pahali palipokuwa mizabibu elfu moja iliyopata vikoroti vya feza elfu moja, patakuwa michongoma na miiba mitupu.
24Watu watakwenda kule kuwinda kwa pinde na mishale, maana inchi yote itakuwa imejaa michongoma na miiba.
25Nayo milima yote iliyokuwa ikilimwa itakuwa imejaa michongoma na miiba, hata hakuna mutu atakayejaribu kwenda kule. Pahali pake itakuwa tu nafasi ya kukulishia ngombe na kondoo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.