Zaburi 39 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mwanadamu mbele ya Mungu

1Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa Yedutuni. Zaburi ya Daudi.

2Nilisema: “Nitayachunga maisha yangu,

kusudi nisitende zambi kwa usemi wangu.

Nitafunga midomo yangu waovu wanapokuwa karibu nami.”

3Nilikuwa kama bubu, bila kusema kitu,

nilinyamaza lakini sikupata faida.

Mateso yangu yalizidi kuwa makali,

4mahangaiko yangu yakaniunguza katika moyo.

Kadiri nilivyowaza ndivyo nilivyotaabika,

kisha maneno haya yakanitoka:

5“Ee Yawe, unijulishe mwisho wangu,

siku zangu za kuishi zimenibakia ngapi,

nijue namna maisha yangu yanavyopita upesi!”

6Kumbe umenipimia maisha mafupi sana!

Maisha yangu si kitu mbele yako.

Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!

7Kweli, kila mutu anapita kama kivuli;

masumbuko yake yote ni bure tu;

anakusanya mali, hajui atakayeipata!

8Na sasa, ee Bwana, ninatazamia nini?

Tumaini langu ni kwako wewe!

9Uniokoe katika makosa yangu yote;

usikubali wapumbafu wanichekelee.

10Niko kama bubu, sisemi kitu,

kwa maana wewe ndiwe uliyetenda hayo.

11Usiniazibu tena;

ninamalizika kwa mapigo yako.

12Unapomwazibu mutu zambi zake kwa kumwadibisha,

unaharibu kama nondo kile anachokipenda.

Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!

13Usikie maombi yangu, ee Yawe,

usikilize kilio changu,

usikae kimya ninapolia.

Maana, mimi ni kama mugeni tu anayepita,

ni musafiri kama vile babu zangu wote walivyokuwa.

14Uache kuniangalia nipate kufurahi kidogo,

mbele sijaaga dunia na kutoweka kabisa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help