1Daudi akasimama na kwenda zake, naye Yonatani akarudi katika muji.
Daudi anamukimbia Saulo2Daudi alikwenda kwa kuhani Ahimeleki kule Noba. Ahimeleki akaenda kumupokea akiwa anatetemeka, akamwuliza: “Kwa nini umekuja hapa peke yako?”
3Daudi akamujibu: “Niko hapa kutokana na amri ya mufalme. Aliniambia nisimwelezee mutu yeyote juu ya kile ambacho amenituma. Nimeagana na watu wangu kwamba tukutane pahali fulani.
4Uko na kitu chochote? Ninakuomba mikate mitano au chochote kinachokuwa.”
5Kuhani Ahimeleki akamwambia: “Hapa sina mukate wa kawaida. Niko tu na ile mikate mitakatifu. Munaweza kupewa mikate hiyo ikiwa watu wako wamejitenga na wanawake siku hizi.”
6Daudi akamwambia: “Kwa hakika, ninapokwenda kwa ajili ya shuguli kubwa, wanawake wanatengwa mbali nasi! Ikiwa miili ya vijana wangu inakuwa mitakatifu na safi tunapokuwa kwenye shuguli za kawaida, basi, si zaidi katika shuguli hii kubwa?”
7Kwa hiyo kuhani Ahimeleki akamupa mikate mitakatifu, maana hapakukuwa mikate mingine isipokuwa ile ambayo inaondolewa mbele ya Yawe na kubadilishwa na mikate mipya kutoka kwenye jiko.
8Basi siku ile pale kulikuwa mutumishi mumoja wa Saulo ambaye alikuwa amezuiliwa mbele ya Yawe. Mutumishi yule aliitwa Doegi Mwedomu, aliyekuwa musimamizi wa wachungaji wa nyama wa Saulo.
9Basi, Daudi akamwambia Ahimeleki: “Una upanga au mukuki ambao unaweza kunipatia? Kwa maana shuguli za mufalme zilinilazimisha niondoke haraka, nami niliondoka bila upanga wangu wala silaha nyingine yoyote.”
10Ahimeleki akamujibu: “Upanga wa Goliati Mufilistini uliyemwua kwenye bonde la Ela uko nyuma ya efodi, unafungwa katika kitambaa. Ikiwa unataka kuukamata basi, uukamate maana hakuna upanga mwingine hapa.”
Daudi akamwambia: “Hakuna upanga mwingine kama huo; unipe.”
11Siku hiyo, Daudi alimukimbia Saulo, akaenda kwa mufalme Akisi wa Gati.
12Watumishi wa mufalme wakamwambia Akisi: “Huyu si Daudi, mufalme wa inchi ya Israeli? Si huyu ambaye walikuwa wakiimbiana juu yake katika ngoma, wakisema: ‘Saulo ameua maelfu yake na Daudi ameua elfu makumi yake?’ ”
13Daudi akafikiri sana juu ya maneno yale, akaanza kumwogopa sana Akisi mufalme wa Gati.
14Hivyo, akabadilisha tabia yake, akijifanya mwenda-wazimu, akakuwa anakwaruzakwaruza kwenye milango ya muji, na kuacha mate yake yatiririke kwenye ndevu zake.
15Akisi akawaambia watumishi wake: “Munajua kwamba mutu huyu ni mwenda-wazimu. Kwa nini mumemuleta kwangu?
16Ninawahitaji wenda-wazimu zaidi? Kwa nini munaniletea mwenda-wazimu akuje kunisumbua na vitendo vya wenda-wazimu? Mutu huyu ataingia katika nyumba yangu?”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.