1 Petro 2 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Jiwe lenye uzima na taifa takatifu

1Basi, mutupilie mbali matendo yote maovu na ya udanganyifu pamoja na wivu na masingizio ya kila namna.

2Kama vile watoto wachanga wanaotamani maziwa, na ninyi vilevile mukuwe na hamu ya kunywa maziwa safi ya kiroho, kusudi mupate kukomaa na kuokolewa.

3Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mumetambua kwamba Bwana ni mwema.”

4Mumwendee Bwana. Yeye ni jiwe lenye uzima. Jiwe lile lilitupiliwa na watu lakini lilichaguliwa na Mungu, nalo linahesabiwa kuwa la bei kali mbele yake.

5Nanyi vilevile, kama mawe yenye uzima mutumiwe kwa kujenga hekalu la kiroho. Na mule mutafanya kazi takatifu ya ukuhani kwa kutoa sadaka za kiroho zinazomupendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.

6Kwa kuwa imeandikwa hivi katika Maandiko Matakatifu:

“Nimesimika jiwe kubwa la pembe katika Sayuni,

jiwe lile ni la bei kali.

Ni mimi niliyelichagua.

Yule anayelitumainia hatapata haya.”

7Basi jiwe lile linahesabiwa kuwa la bei kali kwa wale wanaoamini. Lakini kwa wale wasioamini ni:

“Jiwe lililotupiliwa na wajengaji,

lakini sasa linakuwa jiwe kubwa la pembe.”

8Tena imeandikwa kwamba:

“Jiwe lile ni la kukwalisha watu,

nalo ni la kuwaangusha.”

Wamejikwaa kwa sababu hawakuamini neno la Mungu, na hivi ndivyo walivyopanga kwa ajili yao tangu mwanzo.

9Lakini ninyi ni watu wa kizazi kilichochaguliwa na Mungu na wa ukuhani wa kifalme. Ninyi ni taifa takatifu na watu wa pekee wa Mungu. Mumechaguliwa kusudi mutangaze matendo makubwa ya yule aliyewaita kutoka katika giza na kuwaingiza kwenye mwangaza wake wa ajabu.

10Zamani ninyi hamukukuwa watu wa Mungu, lakini sasa munakuwa watu wake; zamani ninyi hamukuhurumiwa na Mungu, lakini sasa mumehurumiwa naye.

Maisha ya watumishi wa Mungu

11Wapendwa wangu, ninawasihi ninyi, kama vile wageni na wasafiri hapa katika dunia, muepuke tamaa za mwili zinazopigana na roho.

12Mukuwe na mwenendo muzuri kati ya wapagani, kusudi wakiwasingizia kwamba mumefanya mabaya, wapate kuona matendo yenu mema na wamutukuze Mungu siku ile ya kuja kwake.

13Kwa ajili ya utukufu wa Bwana, mutii mamlaka yote ya watu: ikiwa ni mufalme anayekuwa na uwezo juu ya vyote,

14au ikiwa maliwali waliosimikwa naye kwa kuwaazibu watenda mabaya na kuwapa zawadi wale wanaotenda mema.

15Na hayo ndiyo mapenzi ya Mungu, anayetaka munyamazishe usemi wa ujinga wa wapumbafu kwa njia ya kutenda mema.

16Muishi kama watu wanaokuwa na uhuru, lakini musitumie uhuru wenu kwa kufunika ubaya, lakini muishi kama watumwa wa Mungu.

17Muwaheshimu watu wote. Muwapende wandugu zenu waamini. Mumwogope Mungu, mumuheshimu mufalme.

Mufano wa mateso ya Kristo

18Ninyi watumishi, muwatii wabwana wenu na kuwapa heshima yote, si wale wanaokuwa wema na wapole tu, lakini hata wale wanaokuwa wakali vilevile.

19Kwa maana mukivumilia mateso musiyostahili kwa ajili ya kumuheshimu Mungu, yeye atawabariki.

20Kuna sifa gani kama mukivumilia mapigo kwa sababu mulitenda mabaya? Lakini mukivumilia mateso kwa sababu mulitenda mema, jambo hilo linamupendeza Mungu.

21Ni kwa ajili ya shabaha hiyo Mungu aliwaita kumufuata, kwa sababu Kristo vilevile aliteswa kwa ajili yenu, akiwaachia mufano, kusudi mufuate njia yake.

22Yeye hakutenda zambi, wala neno la udanganyifu halikutoka ndani ya kinywa chake.

23Wakati walipomutukana, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakutisha watu hata wamwogope. Lakini alijiachilia katika mikono ya Mungu anayehukumu watu kwa haki.

24Kristo yeye mwenyewe alibeba mizigo ya zambi zetu ndani ya mwili wake alipoteswa juu ya musalaba, kusudi tupate kuachana na zambi kabisa na kuishi maisha ya haki. Kwa ajili ya mapigo yake ninyi muliponyeshwa.

25Kwa maana mulikuwa kama kondoo wanaopotea, lakini sasa mumerudi kwa yule anayekuwa muchungaji na mwangalizi wa roho zenu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help