Kumbukumbu la Sheria 9 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Kutotii kwa watu

1“Musikilize enyi Waisraeli! Hivi leo mumekaribia kuvuka muto Yordani, kwenda kurizi inchi ya mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi. Miji yao ni mikubwa na ina kuta zinazofika katika mawingu.

2Watu wenyewe ni warefu na wenye nguvu; ni Waanaki ambao kama vile munavyojua na kama vile mulivyosikia watu wanasema juu yao: ‘Nani anayeweza kuwashambulia?’

3Mujue leo hii kwamba anayewatangulia kama vile moto unaoteketeza miti ni Yawe, Mungu wenu. Atawaangamiza na kuwashinda mbele yenu, kwa hiyo mutawafukuza na kuwaangamiza mara moja, kama vile Yawe alivyowaahidi.

4“Yawe, Mungu wenu akiacha kuwafukuza watu hao mbele yenu, musiseme ndani ya moyo wenu kwamba: ‘Ni kwa sababu ya uhaki wetu Yawe ametuleta tuirizi inchi hii’, ambapo Yawe amewafukuza watu hawa mbele yenu kwa sababu wao ni waovu.

5Munaweza kuirizi inchi yao si kwa sababu ninyi ni watu wa haki wenye mioyo ya usawa; lakini Yawe, Mungu wenu, anawafukuza watu hao mbele yenu kwa sababu ni waovu na anataka kuweka imara lile neno alilowaapia babu zenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo.

6Basi, mujue kwamba Yawe, Mungu wenu, anawapa inchi hii nzuri muirizi si kwa sababu munastahili kuirizi, maana ninyi ni watu wagumu.

7“Mukumbuke na musisahau jinsi mulivyomukasirikisha Yawe, Mungu wenu, kule katika jangwa. Tangu siku ile mulipotoka katika inchi ya Misri mpaka siku mulipofika pahali hapa, ninyi mumekuwa mukimwasi Yawe.

8Hata huko kwenye mulima Horebu, mulimukasirikisha Yawe, naye alikasirika sana, kiasi cha kutaka kuwaangamiza.

9Nilipopanda juu ya mulima kupokea vibao vya mawe ambavyo kuliandikwa agano ambalo Yawe alifanya nanyi, nilikaa huko siku makumi ine, usiku na muchana; sikukula wala kunywa chochote.

10Kisha Yawe akanipa vibao viwili vya mawe vilivyoandikwa kwa kidole cha Mungu. Vilikuwa vimeandikwa maneno yote ambayo Yawe aliwaambia kwenye mulima kutoka kwenye moto siku ya mukutano.

11Hakika, nyuma ya siku hizo makumi ine, usiku na muchana, Yawe akanipa vibao hivyo viwili vya mawe ambavyo kuliandikwa agano.

12“Basi, Yawe akaniambia: ‘Ondoka, ushuke chini ya mulima upesi, kwa sababu watu wako uliowatoa Misri wamepotoka. Wameacha upesi njia niliyowaamuru wafuate na wamejifanyia sanamu ya kuyeyushwa’.

13“Vilevile, Yawe akaniambia: ‘Nimewaona watu hawa, ni watu wagumu sana.

14Uniache niwaangamize, nifute jina lao toka katika dunia. Nami nitakufanya wewe kuwa taifa lenye nguvu na kubwa kuliko wao.’

15“Basi, nikageuka, nikashuka kutoka kwenye mulima, nikiwa nimebeba vile vibao viwili vya agano, nao moto ulikuwa unawaka juu ya mulima.

16Niliangalia, nikaona kwamba mumekwisha kutenda zambi mbele ya Yawe, Mungu wenu. Mulikwisha kujitengenezea sanamu ya mwana-ngombe ya kuyeyushwa. Bila kukawia mulikwisha kuacha njia ya Yawe ambayo aliwaamuru.

17Hivyo, nikashika vile vibao viwili nikavitupa chini, nikavivunja mbele yenu.

18Kisha nikalala uso mpaka chini mbele ya Yawe, kama vile mbele, kwa muda wa siku makumi ine usiku na muchana. Sikukula chakula wala kunywa maji, kwa sababu ya zambi muliyokuwa mumetenda kwa kufanya maovu mbele ya Yawe kwa kumukasirikisha.

19Niliogopa kwamba hasira na kasirani ya Yawe juu yenu ingewaangamiza, lakini Yawe akanisikiliza vilevile wakati huo.

20Yawe alikuwa amemukasirikia sana Haruni, kiasi cha kumwangamiza. Hivyo, nikamwombea Haruni wakati huohuo.

21Kile kitu kiovu, ni kusema yule mwana-ngombe muliyejitengenezea, nilikitwaa, nikakiteketeza ndani ya moto, nikakipondaponda na kukisagasaga, kikakuwa mavumbi laini. Halafu nikayatupa hayo mavumbi kwenye kijito kilichotiririka chini ya mulima huo.

22“Tena mulimukasirikisha Yawe, Mungu wenu, huko Tabera, Masa na Kiburoti-Hatawa.

23Na Yawe alipowatuma kutoka Kadesi-Barnea, akisema ‘Muende murizi inchi ambayo nimewapatia’, hamukufuata amri ya Yawe, Mungu wenu. Hamukuamini wala hamukutii yale aliyowaambia.

24Ninyi mumekuwa waasi mbele ya Yawe tangu siku nilipowajua.

25“Kwa hiyo, nikalala uso mpaka chini mbele ya Yawe siku hizo makumi ine, usiku na muchana, kwa sababu Yawe alikuwa amesema atawaangamiza.

26Nikamwomba Yawe, nikisema: Ee Yawe, usiwaangamize watu wako na urizi wako, watu uliowakomboa na kuwatoa katika inchi ya Misri kwa uwezo na nguvu yako kubwa.

27Uwakumbuke watumishi wako, Abrahamu, Isaka na Yakobo, wala usijali ugumu, uovu na zambi za watu hawa.

28Watu wa kule ulikotutoa wasiseme: ‘Yawe aliwatoa kusudi awaue katika jangwa kwa sababu hakuweza kuwaingiza katika inchi aliyowaahidi na kwa sababu aliwachukia’.

29Maana, hawa ni watu na urizi wako, watu ambao uliwatoa kwa nguvu na uwezo wako mukubwa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help